Friday, October 2, 2015

VITENDO VYA KUUWANA KWA RISASI VYAZIDI KUSHAMIRI, MAREKANI

Mauaji mengine ya wanafunzi wakiwa chuoni Marekani, maneno ya Obama pia yapo hapa..

Matukio ya watu kupigwa risasi katika maeneo ya wazi yamekuwa yakiripotiwa kila wakati Marekani..Headlines za sasa ni kuhusu kijana mmoja kuvamia chuo cha Umpgua community na kuua wanafunzi 10 huku wengine saba wakijeruhiwa.
Polisi walipata taarifa hiyo baada ya mtuhumiwa huyo kufanya tukio hilo na kufika eneo la tukio..pia polisi walifanikiwa kumuua Harper Mercer ambaye anatuhumiwa kufanya mauaji hayo kwa kumpiga risasi akiwa bado eneo la tukio.
shoot
Mmoja wa mashuhuda ambaye alikua baba wa mmoja wa wanafunzi waliojeruhiwa  alisema kijana huyo aliyejulikana kwa jina la Harper Mercer kabla ya kufanya mauaji alikua akiwauliza watu hao wanatoka dini gani kisha kuwafyatulia risasi.
shoot2
Polisi bado wanaendelea na uchunguzi kujua muuaji huyo alikua na lengo gani na kutafuta nyumba aliyokuwa akiishi.
Rais wa Marekani Barak Obama amesema matukio ya watu kuua raia yamekuwa yakawaida sana na kuvitaka vyombo husika kuweka sheria ya udhibiti wa silaha za moto.
shoot3

shoot4
Harper Mercer mwenye miaka 26, kijana anayetuhumiwa kufanya mauaji hayo
Obama akizungumza baada ya tukio hilo…
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment