Thursday, January 15, 2015

HEKAHEKA YA KUMEKUCHABLOG HII HAPA

Nimekuwekea Hekaheka ya leo Jan 15, inahusu mtoto anayeteswa na Mama yake

Beasts-Quvenzhane-sadKama hukusikiliza Hekaheka ya leo Jan 15 inatokea Kunduchi, Dar inahusu mama ambaye inasemekana amekuwa akimtesa mtoto wake kwa kumpiga kitendo kilichowachosha majirani na kuamua kumchukua mtoto huyo.
Mtoto huyo amesema kuwa mama yake amekuwa akimpiga kwa banio la kupigia ugali,  chupa na waya ambapo mara ya mwisho alimpiga  kwa kumtuhumu kumuibia fedha baada ya kumtuma dukani.
Mama huyo alipoulizwa amesema mtoto huyo alikuwa na tabia za ajabu toka akiwa mdogo na amekuwa akimpiga kwa fimbo ili ajirekebishe japo majirani hawakukubaliana na utetezi wa mwanamke huyo.
Baba  ambaye ni jirani aliyemchukua mtoto huyo amesema tayari amepeleka suala hilo Polisi na amepeleka barua kwa mjumbe ili aweze kukaa na mtoto huyo kwa kufuata utaratibu unaotambulika.

No comments:

Post a Comment