Friday, January 16, 2015

SOMA HABARI KUU ZILIZOPEWA UZITO KATIKA KURASA MAGAZETI YA LEO,TZ

Stori kubwa muhimu zilizopewa Headlines kwenye Magazeti ya leo Tanzania January 16, 2015

OLYMPUS DIGITAL CAMERA
MWANANCHI
Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali, PAC imeitaka Menejimenti ya Mamlaka ya bandari TPA kurejesha nyongeza ya fedha zote za malipo za safari zilizowalipa watendaji wake tangu mwaka 2011 baada ya kubaini kuwa zililipwa bila kuidhinishwa na msajili wa Hazina.
Ukaguzi maalum uliofanywa katika mamlaka hiyo na Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali CAG mwaka 2011/12, unaonyesha kuwa TPA iliomba nyongeza ya malipo ya safari lakini kabla ya kupewa kibali na msajili wa Hazina, ilianza kuwalipa watendaji wake nyongeza hiyo.
Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe alisema malipo ya safari kwa wafanyakazi wa ngazi za chini wa Mamlaka hiyo kwa siku awali walikua wakilipwa 94,000 na sasa ni 123,000 na watendaji wa juu awali walikua wakilipwa 270,000 na sasa ni 500,000.
Alisema malipo kwa safari za nje watendaji wa ngazi za chini kwa siku ni dola za Marekani 296 na wale wa ngazi za juu ni dola 600 awali na sasa dola 800.
Tunataka mrejeshe fedha hizi tangu mlipoanza kuzilipa mwaka 2011 kwa sababu mlifanya makosa kwani mmelipa bila kupewa kibali na msajili wa hazina” alisema Zitto.
MWANANCHI
Jumuiya wa wanataaluma wa chuo kikuu cha Dar es salaam UDASA na ITV, Radio One wamesaini makubaliano ya kuandaa mdahalo wa wagombea wa Urais kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
Mwenyekiti wa UDASA, Prof. Kitila Mkumbo alisema katika nchi za kidemokrasia midahalo hufanikisha uchaguzi ulio huru, haki na uwazi.
Pia alisema midahalo hiyo hutoa fursa muhimu kwa wagombea kueleza falsafa, sera na mikakati yao ya kutatua matatizo mbalimbali yanayowakalibi wananchi.
Aidha alisema midahalo watakayoendesha haitaegemea upande wowote na kwamba mgombea atakayekataa kushiriki hawatamlazimisha.
MWANANCHI
Wanafunzi watatu wa mwaka wa tatu ambao ni viongozi wa Chuo kikuu cha Dodoma UDOM wametimuliwa kwa madai ya kuwa chanzo cha migogoro chuoni hapo.
Makamu Mkuu wa UDOM, Prof. Idris Kikula alisema jana waliwafukuza wanafunzi hao kwa kosa la kuwa kinara wa kushinikiza migomo.
Kwa upande mwingine wanafunzi 84 wa programu maalum ya Stashahada ya ualimu chuoni hapo waliofanya mgomo na kushinikiza kulipwa madai yao, jana walipandishwa kizimbani katika mahakama ya Mkoa wa Dodoma kwa kosa la kukusanyika bila kibali.
Hakimu mkazi Kabate Richard alisema dhamana ipo wazi kwa wanafunzi hao ambao walijidhamini wenyewe kwa shilingi 20,000 na sasa kesi hiyo itasikilizwa tena February 16-19 mwaka huu.
MWANANCHI
Jeshi la Polisi Kibaha limewakamata raia 14 wa Ethiopia kwa tuhuma za kukutwa katika moja ya vichaka lililopo eneo la TAMCO wakiwa hawana vibali vya kuingia nchini.
Kamada wa Polisi Pwani Ulrich Matei alisema wahamiaji hao waliingia nchini wakitokea Kenya na walisafiri kwa kutumia gari aina ya fuso hadi Wilaya ya Bagamoyo walipotelekezwa kwenye moja ya mapori katika barabara ya TAMCO.
Alisema Polisi kwa kushirikiana na Idara ya Uhamiaji waliwabaini wahamiaji hao baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema.
Katika maelezo yao raia hao walisema wamekimbia njaa na vita nchini mwao na walikua wakijiandaa kusafiri kimya kimya hadi Afrika Kusini kutafuta kazi.
MTANZANIA
Kamati ya Nishati na Madini imeonyesha hofu juu ya Jiji la Dar es salaam kuteketea kwa moto kutokana na uwezekano wa kulipuka kwa mabomba ya kusafirishia mafuta unaohusisha utoboaji wa mabomba hayo.
Kutoka na hali hiyo Wabunge wameomba vyombo vya ulinzi hususani JKT na JWTZ kupewa jukumu la kuimarisha miundombinu ya kusafirisha mafuta huku baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo wakijiandaaa kuhamisha familia zao Dar.
Hofu ya Wabunge hao ilitokana na taarifa iliyosomwa mbele yao na meneja mkuu wa Makampuni yanayoingiza mafuta nchini, Michael Minja kwa ajili ya kutolea ufafanuzi punguzo la bei ya mafuta katika soko la dunia.
Katika sehemu ya taarifa hiyo Minja alisema mafuta yanapotea njiani baada ya kuibiwa yanakuwa yameshalipiwa kodi hali inayofanya waagizaji wabebe hasara hiyo.
Mbali na kuibwa,hatuombi litokee lakini kwa namna miundombinu ya kusafirisha mafuta ilivyo,jiji lote litaangamia“alisema Minja.
MTANZANIA
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magessa Mulongo anaishi katika hoteli ya utalii yenye hadhi ya nyota nne kwa miezi miwili sasa kutokana na nyumba yake kuhitaji ukarabati.
Tangu alipowasili Mwanza mara baada ya mabadiliko yaliyofanywa na Rais Kikwete, Mkuu huyo wa Mkoa amekua akiishi katika hotel ya kitalii ya Malaika yenye hadhi ya nyota nne ambayo chumba kimoja kwa siku hutozwa sh 425,000 au milioni 25.5 kwa mwezi.
Mulungo alisema nyumba aliyokua akiishi inahitaji kufanyiwa ukarabati mkubwa kutokana na kutofanyiwa kwa muda mrefu kwa sababu ya uhaba wa fedha hivyo kuwa katika hali mbaya.
Nimesikua mengi yanasemwa kuhusu jambo hili lakini sitaki kuingia katika malumbano yasiyo na tija,unaweza kuwasiliana na watu wa TBA ambao ni wakala wa majengo“alisema Mulongo.
HABARILEO
Mamlakaya Udhibiti wa Nishati ya maji, EWURA imebainisha kuwa hadi kufikia March mwaka huu bei ya mafuta nchini itaendelea kushuka kulingana na kushuka kwa bei ya mafuta kwenye soko la dunia.
Hata hivyo Mamlaka hiyo imeonya bei hiyo ya mafuta haitaweza kupungua kwa kiasi kikubwa kutokana na kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola ya Marekani pamoja na kutobadilika kwa ushuru mbalimbali wa ndani wa mafuta.
Akiwasilisha taarifa ya ukokotaji wa mafuta kwa kamati, Mtaalamu kutoka EWURA,  Lorivii Long’idu alikiri ni kweli kwa sasa bei ya mafuta katika soko la dunia imekua ikishuka kwa kasi ikilinganishwa na kipindi cha nyuma.
Bei hizi zimeshuka kutoka sola 100 hadi kufikia dola 60 kwa pipa ambayo ni sawa na asilimia 40 kutokana na kudorora kwa uchumi wa bara la Ulaya katika kipindi hiki na kuwepo kwa tofauti za mitazamo ya kisiasa hasa katika nchi za Marekani na Urusi,”alisema Long’idu.
NIPASHE
Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa imeandikia barua Chama cha Tanzania Labour Party TLP, kukitaka kifanye uchaguzi wa viongozi na kwamba endapohakitafanya hivyo kitafutiwa usajili.
Msajili wa vyama vya siasa, Sisty Nyahoza alisema sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992 kifungu cha 9 inavitaka vyama hivyo kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano lakini chama hicho kimepitisha muda bila kufanya uchaguzi.
Alisema ofisi ya msajili ilipokea maombi kwa chama hicho mara tatu kikiomba kusogezewa mbele muda wa kufanya uchaguzi huo kutokana na sababu mbalimbali.
Sababu ya kwanza ilikuwa Mwenyekiti wake, Augustine Mrema  kuwa nje ya nchi kwa matibabu, sababu ya pili ilikuwa kupisha Bunge maalum la Katiba na nyingine ilikua uchaguzi wa Serikali za Mitaa
Nakuhakikishia kwamba nitakufikishia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment