Thursday, January 15, 2015

WAKENYA WAPIGA HATUA SEKTA YA USAFIRISHAJI



Huduma ya dharura kwa watumishi wa umma Kenya imeboreshwa, kwa sasa zinatumika na ndege mtu wangu!

150114163803_president_kenyatta_1Vifaa vya uokoaji ni vitu muhimu katika jamii hasa pale matatizo yanapotokea, ni  vizuri msaada ukapatikana mapema pale ambapo unahitajika, Serikali ya Kenya imeamua kufanya hili kama moja ya njia za kuboresha huduma ya dharura kwa watumishi wa huduma za kiafya.
Tumesikia malalamiko mengi kutoka kwa watumishi wa Serikali kuhusu huduma mbaya wanazopatiwa mbali na kuwa wanakatwa kodi kubwa kila mwezi.
Kenya wamezindua huduma za dharura kwa kutumia Ndege na magari ya kisasa kwa watumishi wa umma, uzinduzi wa huduma hiyo uliohudhuriwa na Rais Uhuru Kenyatta.
Huduma hiyo imezinduliwa kwa ushirikiano na Shirika la Bima ya Afya, Shirika la Msalaba Mwekundu na kundi la madaktari wanaosafiri kwa ndege la AMREF.
Huduma hiyo inafanya Kenya kuwa nchi ya pili baada ya Afrika Kusini kutoa huduma ya aina hii.
150114163803_president_kenyatta_3
.
Rais Uhuru Kenyatta akipewa maelekezo namna gari ya dharura inavyofanya kazi.

.
Rais Kenyatta akipewa maelekezo namna huduma inavyotolewa ndani ya ndege.

150114163803_president_kenyatta_1Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia, tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment