Wednesday, January 14, 2015

ANTI EZEKIEL AKANUSHA KUWA NA UJAUZITO


 Muigizaji wa Bongo Movie Aunty Ezekiel

Aunty Ezekiel Soudy Brown amepiga story na muigizaji Aunty Ezekiel kuhusiana taarifa kwamba ni mjamzito na ameonekana akinywa pombe, Soudy alimuuliza kama anafahamu athari za kunywa pombe huku akiwa na ujauzito, Aunty akasema hazijui na yeye sio mjamzito.
PhotoGrid_1420206423320
Soudy alimtafuta pia Dk Makongoro  kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili ambaye alielezea kuhusu matatizo ambayo mwanamke anaweza kuyapata iwapo ni mjamzito na anatumia pombe kali, daktari huyo amesema kuwa mama mjamzito anatengeneza mazingiza ya pombe kusafiri kutoka kwake kwenda kwa mtoto na kujitunza kwenye sehemu za ubongo kitendo kinachosababisha mtoto kuzaliwa akiwa na matatizo  kama mtindio wa Ubongo, Kuzubaa au matatizo ya macho.
Hutopitwa na habari yoyote inayonifikia na niko tayari wakati wowote kukupatia kinachijiri kila pembe ya nchini na ulimwenguni kote kupitia tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment