Wednesday, January 14, 2015

CHIKAWE KUWAIBUA WAPIGA RAMLI WANAOTUMIWA KUWAUWA ALBINO

Kauli ya Waziri Chikawe kuhusiana na Waganga wanaochangia mauaji ya Albino

albinoMatukio ya kuuawa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi ‘Albino’ bado yameonekana kuendelea kuchukua nafasi hasa katika Mikoa ya kanda ya Ziwa hali inayozidi kutishia amani ndani ya familia nyingi.
Waziri wa mambo ya ndani Mathias Chikawe ametoa tamko kuwa kutakua na operesheni ya kitaifa ya kuwasaka na kuwakamata waganga wa kienyeji maarufu kama wapiga ramli  ili kuwafikisha mahakamani.
byUamuzi wa Waziri huyo unatokana na kukithiri kwa vitendo vya unyanyasaji wa watu wenye ulemavu vikishika kasi kutokana na kuuawa kwa imani za kishirikina.
Chikawe alisema watashirikiana na Chama cha watu wenye ulemavu TAS kuwabaini wahalifu na kuwachukulia hatua ili kupunguza vitendo hivyo.
Nakuhakikishia kwamba nitakufikishia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment