Wasanii Bob Junior, Ney Wamitego,Witness ni kati ya waliosikika kwenye 255 ya leo jan 15.
Ile collabo kati ya msanii Bob Junior na Jose Chameleone tayari imeshapikwa katika studio mbili, Sharobaro Record na Island Record ambapo Bob Junior amefunguka kwenye 255 kuwa ni ngoma kubwa ingawa imechelewa kutoka kutokana na burdget ya video kuwa kubwa, wimbo utakuwa tofauti na wa Kiafrika zaidi.
Bob Junior amekanusha tetesi za kutoka na mwigizaji Wema Sepetu na kusema ni mtu ambaye wanashirikiana kwenye mambo mengi.
Msanii Ney Wamitego amezungumza kuhusu msanii wa Afrika Kusini, Zola kukataa kufanya remix ya ‘Akadumba’ na badala yake alimshauri wafanye wimbo mpya ambao tayari wamesharekodi.
Witness na mpenzi wake Ochu Sheggy
ambao wameachia wimbo wao mpya, wamepiga story na 255 kutokana na
kuonekana kuongozana muda wote na kuwauliza mastaa gani
wanaowa-inspire jinsi wanavyoishi, wawili hao walisema wanavutiwa na Brad Pitt na Angelina Jollie kutokana na kwamba wanafanya kazi kwa pamoja ingawa ni wapenzi lakini wanaheshimiana, upande wa mastaa wa muziki wanavutiwa na Jay Z na Beyonce.
Jarida la International Business Times 2013 liliripoti kuwa utajiri wa Jay Z na Beyonce unakadiriwa kufika dola bilioni moja na kuwafanya kuwa Pop First Billionaire Couple.
No comments:
Post a Comment