Thursday, January 15, 2015

MAJERUHI WAZIDI KUONGEZEKA ARSENAL

Majeruhi ya wachezaji hawa yanawaweka kwenye wakati mgumu Arsenal kwa sasa…

Mikel Arteta
Klabu ya Arsenal imekumbwa na janga lingine la majeruhi baada ya ripoti kuhusu wachezaji wake wawili muhimu kuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitatu wakiuguza majeraha tofauti.
Arsenal itawakosa kiungo mkongwe ambaye pia ni nahodha wa timu, Mikael Arteta ambaye amefanyiwa upasuaji wa kuondoa mfupa mdogo kwenye kifundo chake cha mguu na atahitaji miezi mitatu ya kupumzika kabla ya kurudi uwanjani.
Nahodha wa Arsenal Mikel Arteta atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitatu baada ya kufanyiwa upasuaji wa kifundo cha mguu .
Nahodha wa Arsenal, Mikel Arteta.
Ukiachilia mbali Arteta, the Gunners pia watamkosa beki wa kushoto Matthieu Debuchy ambaye amefanyiwa upasuaji wa kurekebisha bega lake baada ya kuteguka kwenye  mchezo dhidi ya Stoke City uliopigwa jumapili ya wiki iliyopita.
Beki wa kushoto wa Arsenal Mfaransa Mathieu Debuch naye atakaa nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuumia bega .
Beki wa kushoto wa Arsenal Mfaransa Mathieu Debuch naye atakaa nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuumia bega .
Hii ni mara ya pili kwa Debuchy kuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitatu baada ya nyota huyo wa Ufaransa ambaye yuko kwenye msimu wake wa kwanza ndani ya Arsenal kuumia kifundo cha mguu hapo awali ambapo alikaa nje ya uwanja kwa kipindi kama hiki.
Hii ni mara ya pili kwa Debuch kuwa nje ya uwanja kwa miezi mitatu baada ya kuumia enka hapo awali .
Debuchy amefanyiwa upasuaji wa kurekebisha bega lake   lililoteguka.
Debuchy baada ya kupata majeraha uwanjani.

No comments:

Post a Comment