Kumekucha blogi
Pemba,WAKAZI wa kiwani cha Pemba wamelalamika nauli kubwa za usafiri wa meli kutoka Pemba kwenda
Unguja na hivyo kuitaka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuzirejesha meli zake za
Maendeleo na Mapinduzi ili kuwapa unafuu wakazi wa Visiwa hivyo.
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti jana na kumekucha blog wakazi hao walisema kutokuwepo kwa meli za Serikali
kama ilivyokuwa zamani kumewapa nguvu makampuni ya usafirishaji kuweka nauli za
juu na hivyo kuwanyima fursa baadhi ya watu kuwatembelea jamaa zao visiwani
humo.
Walisema
awali zilikuwepo meli ya Mapinduzi na Maendeleo na nauli zake kuwa nafuu na
hivyo watu wengi kukimbilia meli hizo jambo ambalo lilikuwa likiwapa unafuu
baadhi ya wazazi kuwapeleka likizo watoto wao nyakati za shule kufungwa.
“Sasa hivi
tunashindwa kuwapeleka watoto wetu likizo kuwatembelea jamaa zao baada ya meli
zilizopo nauli zake kuwa juu---hii tunadhani kama ni kukomoana ili watoto wetu
shule zikifungwa wasiende popote” alisema Said Sanani
“Nauli
kwenda Unguja ni zaidi ya shilingi elfu ishirini kwa sasa na hii ni kutokana
meli za mapinduzi na maendeleo ambazo zilikuwa zikimilikiwa na Serikali kupotea
machoni” alisema
Aliishauri
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuzirejesha meli zake ikiwa na pamoja na
kusimamia nauli kwa vyombo vya baharini na kuacha kung’ang’ani nauli za mabasi
na kusahau kuwa kuna wahanga wa vyombo vya baharini kuteseka.
Kwa upande
wake mkazi wa mji wa Wete, Faisal Maftah, amewataka wamiliki wa magari yaendayo
mjini na vijijini kuwakemea wakondakta wao kuacha kuwachukua wanafunzi kwa
madai kuwa wanalipa pesa pungufu.
Alisema
tabia hiyo imekuwa ikishamiri nyakati za shule kufungwa na kufunguliwa na hivyo madereva na makondakta wao wamekuwa
wakikaidi kuwachua wanafunzi mbali ya sheria kuwaruhusu.
“Vipindi vya
shule kufungwa na kufunguliwa watoto wetu wamekuwa wakinyanyasika
sana----wakiona kituo kimejaa watoto hawasimami au hubagua kwa kutangaza kuwa watoto
hawabebi” alisema Maftah
Alivitaka
vyombo vinavyohusika kukemea tabia hiyo na kuacha manyanyaso kwa wanafunzi na
kuweza kuwatembelea ndugu na jamaa zao vipindi vya shule kufungwa.
No comments:
Post a Comment