Ajali ya basi la magereza yaua 10, ni wafungwa na askari, picha hizi hapa…
Basi lililokuwa limebeba wafungwa Texas,
Marekani kuwapeleka gerezani, wakiwa njiani basi liliteleza kutoka
kwenye barabara kutokana na barafu na kuangukia kwenye reli ambako
liligongana na treni ya mizigo.
Katika ajali hiyo wafungwa nane na Askari Magereza wawili walifariki, taarifa kutoka Idara ya Magereza Texas inasema kuwa gari hilo lilikuwa na jumla ya wafungwa 12 na maafisa Magereza watatu ambapo wengine watano walipata majeraha kwenye mkasa huo na kupelekwa Hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Hizi ni pichaz za eneo la tukio.
Iko hapa video ya taarifa ya ajali hiyo.
Nakuhakikishia kwamba nitakufikishia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,tangakumekuchablog
No comments:
Post a Comment