Thursday, January 15, 2015

VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KUPINGA VITENDO VYA KIKATILI



Tangakumekuchablog
Tanga,VIONGOZI wa dini Tanga wametakiwa kuzitumia nafasi zao kwa kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia majumbani na sehemu za kazi na kushauriwa kuunda sheria ndogondogo na kuzipeleka  katika mabaraza ya kata.
Akizungumza katika kikao cha Wadau wa Kupinga Ukatili wa Kijinsia jana, kilichoandaliwa na Asasi ya Kiraia ya Tree of Hope (TOH), Katibu Tawala Wilaya ya Tanga, Benedict Patrick, alisema viongozi wa dini wako na nafasi kubwa ya kutokomeza vitendo vya ukatili vya kijinsia.
Amewataka viongozi hao  kushirikiana na Tree of Hop kwani wameonyesha mfano na kuwa mstari wa mbele katika kukemea vitendo hivyo mbali ya changamoto ambazo wamekuwa wakikumbana nazo zikiwemo za kufanya kazi kwa kujitolea.
“ Suala la kutokomeza vitendo vya kikatili vya kijinsia ni letu sote na sio la Tree of hope peke yao----kuliacha kuwa la mtu pekee haitowezekana  kukomesha matendo haya maovu: alisema Patrik
“Kwa kulipa uzito niwaombe viongozi wa dini muliopo hapa na muwe mabalozi katika sehemu zenu za kazi kutunga sheria ndogondogo na kuzipeleka katika mabaraza ya kata lengo likiwa ni kutokomeza vitendo vya kikatili maeneo yetu” alisema
Katibu huyo aliwataja viongozi hao wa dini kuwa ni wenye ushawishi mkubwa kwa jamii  hivyo kuwataka kuhubiri kila wanapopata nafasi ili kuifanya jamii hiyo kuishi katika mazingira ya amani.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Tree of Hope, Fourtunasa Manyeresa, aliwataka viongozi wa Serikali za mitaa na vijiji kuunda mtandao wa kupambana na vitendo vya ukatili vya kijinsia katika maeneo yao.
Alisema kufanya hivyo kutawezesha kutokomeza vitendo vya kikatili ambavyo vimekuwa vikishamiri hasa majumbani na maofisini na hivyo kuwataka kuzitumia nafasi zao katika kulikomesha jambo hilo ambalo limekuwa likiota mizizi.
“Viongozi wa Serikali za mitaa wako na nafasi kubwa katika kuhakikisha ukatili wa kijinsia unakomeshwa----vitendo hivi vimekuwa vikifanyika hasa majumbani kwa watu kuwafungia ndani watoto na kuwatesa” alisema Manyeresa
“Kuwatumia viongozi hawa kutasaidia kwa kiasi kikubwa kwani wao ndio wanaojua idadi  ya kaya zao----kushikamana na kuwa kitu kimoja ni wazi kuwa vitendo vya kikatili vitakoma” alisema
Mkurugenzi huyo alisema Asasi yake iko na mpango wa kutoa elimu shuleni na kupita kila kijiji lengo ni kutoa elimu na kutokomeza vitendo vya kikatili vinakomeshwa na kila mtu kuwa mwanaharakati wa kupinga.
Alisema mpango huo unakusudia kuwajenga vijana mashuleni na vijijini kuwa kila mmoja kuwa balozi katika sehemu anayotoka wanawake na wanaume na hivyo kuitaka jamii kuwaunga mkono.
                                                             Mwisho

No comments:

Post a Comment