Basi la kutagaa lazinduliwa China
Basi hilo linaloendeshwa kwa umeme linauwezo wa kubeba zaidi ya watu 300 .
Basi hilo kubwa lina urefu wa mita 21 na upana wa futi 25 .
Hii ndio mara ya kwanza kwa wabunifu kuonesha basi hilo hadharani baada ya video yake kuvuja katika mitandao mwezi Mei.
Basi hilo linauwezo wa kuhudumu kwa kasi ya Kilomita 60 kwa kila saa.
Takriban mabasi hayo manne yanawezwa kuunganishwa na hivyo kuwa na dereva mmoja.
''Inahudumu kama vile treni za kisasa za umeme ila gharama ya kuwekeza kujenga njia na ukarabati barabarani ikiwemo ujenzi wa vituo maalum vya TEB ni 1/5 ''
No comments:
Post a Comment