Sio Obama peke yake!! hawa ni viongozi wengine waliowahi kumwaga machozi hadharani..
Wiki iliyopita Rais wa Marekani
Barack Obama aliingia kwenye headlines baada ya kutokwa machozi wakati
akizungumzia hali ya matumizi ya silaha Marekani, machozi
yalimtoka alipokuwa akisimulia kuhusu shambulio la ufyatuaji risasi
katika shule ya msingi ya Sandy Hook mwaka 2012.
Lakini kiongozi huyu hayuko peke katika kutokwa na machozi hadharani…Wafahamu na hawa wengine.
Rais wa zamani wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva
Rais wa zamani wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva
alibubujikwa na machozi mwaka 2009 baada ya mji wa Rio de Janeiro
kutangazwa ungekuwa mwenyeji wa Michezo ya Olimpiki ya mwaka 2016…hata
hivyo machozi yake yalikuwa ni ya furaha.
Mwanasiasa mkongwe wa Japan Ryutaro Nonomura
Video ya mwanasiasa mkongwe wa Japan Ryutaro Nonomura alilia
baada ya kuulizwa maswali na wanahabari kuhusu matumizi yake ya pesa,
ilivuma sana mtandaoni Julai 2014 ambapo alisisitiza zilikuwa ziara za
kikazi na baadaye alijiuzulu.
Rais wa Urusi Vladimir Putin
Machozi yake yalikuwa kinyume kabisa na sifa zake kama mtu mwenye roho ngumu na asiyetekwa na hisia. Baadaye, msemaji wa Putin alisema Putin alikuwa amezidiwa na upepo na baridi na wala si hisia zilizomteka.
Hillary Clinton
Waziri huyo wa zaman wa mambo ya nje wa Marekani aliutaka urais 2008 lakini akashindwa na Rais Barack Obama mbio za kumsaka mgombea wa chama cha Democratic.
Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Margaret Thatcher
Rais wa zamani wa Afghanistan Hamid Karzai
Rais wa zamani wa Afghanistan Hamid Karzai aligonga vichwa vya habari duniani alipolia kuhusu hali ya nchi yake wakati akitoa hotuba mwaka 2010 kuhusu mapigano.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa Tangakumekuchablog
No comments:
Post a Comment