Mengine kutoka Afrika Kusini pamoja na picha 12 hali ilivyokua
Mitandaoni kumekuwa na picha na video
nyingi zimesambaa zikionesha hali ilivyokuwa Afrika Kusini kwa zaidi ya
wiki moja, tumesikia na kuona mashambulizi ambayo wamefanyiwa watu ambao
sio raia wa Afrika Kusini ndani ya nchi hiyo, video nyingi na picha
zinasikitisha.. watoto wanauawa, wanajeruhiwa.. vurugu ilikuwa kubwa
sana.
Hapa
ni ndani ya Kambi ya muda ambayo wamehifadhiwa wageni, yani walikuwa na
maisha yao kawaida tu mtaani baadae wanajikuta ni wakimbizi.
Cha mwisho kilichonifikia ni kuhusu ishu ya Waziri wa Usalama wa South Africa, Nosiviwe Mpisa-Nqkula kutangaza
kwamba sasa wanaoingia kupambana na watu wanaofanya vurugu hizo ni
wanajeshi baada ya kuonekana kama Polisi wameelemewa nguvu na hali
ilivyo mitaani, watu saba waliripotiwa kufariki pia.
Mtaani
hali haikuwa sawa, hili ni sehemu ya kundi kubwa la watu waliokuwa
wanaandamana kupinga Xenophobia, ubaguzi wa kutaka wageni waondoke
Afrika Kusini.
Akina
mama na watoto wao, wako kwenye foleni kusubiri chakula cha msaada
ndani ya Kambi ya wakimbizi ambayo wamehifadhiwa kwa muda.
Mfalme wa Wazulu, Goodwill Zwelithini.
Analaumiwa kusababisha machafuko yaliyotokea Afrika Kusini kutokana na
kauli yake aliyoisema kwamba wageni wanatakiwa warudi kwao. Jumatatu
April 22 amekanusha kushinikiza machafuko hayo
Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe alisema kuna Watanzania waliouawa lakini mauaji hayo hayakutokana na vurugu hizi za kuwakataa wageni.
Pole kwa watu wetu wote ambao wameathirika kutokana na vurugu hizi.
No comments:
Post a Comment