TANGA KUMEKUCHA

Tuesday, May 10, 2016

HADITHI SITASAHAU NILIVYOGEUZWA PAKA







SIMULIZI ZA FAKI A FAKI 0655 340572
 
SITASAHAU NILIVYOGEUZWA PAKA 12
                                             
 
“Nimeshakupanda punda wangu. Sasa twende”  Bibi huyo alimwambia tena msichana huyo huku akimpiga kofi  kwenye makalio yake.
 
Msichana huyo akaanza kutembea kwa  kutumia magoti na mikono akiwa amembeba yule bibi mgongoni.
 
Kwa jinsi msichana huyo alivyokuwa mwembamba, ukilinganisha na uzito wa yule bibi, alikuwa akienda kwa taabu akiwa amekunja uso kuonesha kuwa alikuwa anaumia. Pale alipoonesha kusitasita, yule bibi alimpiga kofi la makalioni na kumuamrisha. 
 
“Twende! Twende!”
 
Wakati kitendo hicho kinafanyika, mke wangu alikuwa akicheka kuonesha kuwa kilikuwa kitendo kilichomfurahisha. Wakati mwingine yule bibi alikuwa akimsukuma yule binti makalioni mwake ili aende kwa haraka haraka.
 
Msichana huyo alipochoka kabisa alijibwaga chini puu! Yule bibi akanyanyuka na kumwambia mke wangu amuinue na amlaze kitandani. Chausiku akamuinua na kumlaza kitandani msichana huyo aliyeonekana kuwa taabani sana.
 
Kama haitoshi, Bi kikongwe na Chausiku wakamchezea ngoma kando ya kitanda pamoja na kumng’ong’a huku wakiwa wamemtolea macho. Baada ya kumfanyia hivyo walimrushia vitu visivyoonekana kisha mke wangu akageuka na kunishika mkono. Kufumba na kufumbua tukajikuta tuko nje ya dirisha. Baada ya sekunde chache tukamuona yule bibi naye ameibuka nje ya dirisha.
 
Msafara ukaongoza njia ya kurudi. Wakati tunarudi yule bibi alikuwa anabadilika badilika. Mara alikuwa anageuka mbwa, mara alikuwa anageuka paka. Tulitembea mpaka tukafika kwenye ule uwanja wetu tunapokutana. Safari ya kurudi pia ilikuwa fupi kama ile ya kwenda.
 
Tulikuta kundi la wenzetu waliokwenda mahali kwingine wakitusubiri. Hapo wachawi hao wakaanza kuhadithiana uchawi wao huku wakionekana kuridhika na vitendo walivyotenda.
 
Mimi tu ndio nilikuwa nimefadhaika. Nilikuwa nikimfikiria yule binti wa kiarabu alivyokuwa anateswa na yule bibi hadi kuanguka chini.
 
Kitendo kile kilinitambulisha kwamba uchawi unahitaji moyo wa ukatili na yule bibi alikuwa katili.
 
Vitendo vile vya kichawi sasa vilianza kunichukiza lakini kwa vile nilikuwa nimeshajiingiza katika kundi hilo sikuwa na budi kuendelea nalo. Mke wangu alishanitishia kuwa nisipokubali kuwa mchawi atakwenda kuniripoti polisi kuwa nimemuua mke wangu wa kwanza. Hivyo niliona ni bora niendelee na udhalimu huo kuliko kukamatwa na polisi na kwenda kushitakiwa kwa kosa la mauaji.
 
Baada ya wachawi hao kuhadithiana hiki na kile, walianza kuvaa nguo zao. Mimi sikuwa na nguo. Yule bibi akanigeukia.
 
“Tunakupa mazoezi ili upate ujasiri. Leo tumekupeleka Songe, kesho utaenda mahali kwengine”  Bibi huyo akaniambia.
 
“Sawa bibi”
 
“Yule msichana hatoolewa ng’o na atabaki kuwa mbovu kila siku” Bibi akaendelea kusema huku akiendelea kuvaa kaniki yake.
 
“Sisi tunakwenda” Mke wangu akamuaga bibi.
 
“Haya nendeni, kesho uje naye”
 
“Nitakuja naye” mke wangu akamwaambia
 
Wakati nimeongozana na mke wangu tukienda mahali alipoweka nguo zake, tulimsikia yule bibi akituambia huko nyuma. 
 
“Mwaambie aache uoga”
 
Mke wangu akaguna 
 
“Mh!.... bibi huyu nae hamalizi kusema!” kisha akamjibu  “Ataacha uoga tu, ndio mwanzo bibi”
 
Tukaenda kwenye kichaka ambako mke wangu aliweka nguo zake. Ulikuwa ni upande wa kaniki. Akajifunga nao kisha tukaondoka kurudi nyumbani.
 
Tulipofika barazani mwa nyumba yetu nilichukua ile shuka yangu nikaivaa kisha tukaingia ndani.
 
Kwa vile tulikuwa tumechoka tulipojilaza tu usingizi ukatuchukua.Tulipozinduka kulikuwa kumekucha. Siku ile nilipanga nisiende shamba.
 
Wakati tunakunywa chai na mke wangu nikamuuliza ni kwanini waliamua kunifuata usiku wakati nilimwambia nilikuwa najisikia kuumwa?.
 
“Ni bibi mwenyewe. Mimi nilimwambia kama ulivyoniambia wewe. Akaniambia mume wako ameanza uvivu. Ndio akaamua kukufuata” Mke wangu akanijibu. alipoona nilikuwa nimenyamaza huku nikimtazama akaendelea kuniambia.
 
“Siku nyingine ukiwa na dharura yako uende ukamwambie mwenyewe”
 
“Je ikitokea ukiumwa wewe itakuwaje? Atakufuata?” nikamuuliza.
 
“Mimi nikiumwa ninamueleza na hawaja nifuata hata siku moja”
 
“Tuseme na akiumwa yeye inakuwaje?”
 
“Yule bibi haumwi, anakula mizizi ya kwao kila siku. Usimuone vile mzee, ni mzima kweli. Hata kama akisafiri usiku anapaa kwenye ungo anakuja uchawini ”
 
“Ala! Kumbe anapaa?”
 
“Anapaa kwa ungo”
 
“Wewe pia unapaa?”
 
“Amenifundisha yeye”
 
“Huo ungo wako, ukowapi?”
 
“Uko chumba cha pili, nimeuweka”
 
“Mkipaa mnaenda wapi?”
 
“Kama tunataka kwenda kufanya uchawi Dar  es Salaam au Tanga tunapaa. Yule bibi wakati mwingine anataka kwenda kukutana na wachawi wenzake wa Sumbawanga na Mwanza, pia anapaa”
 
“Lakini mimi hajanifundisha uchawi huo”
 
“Wewe bado kwanza, lakini atakufundisha tu. Ngoja umalize angalau mwaka mmoja”
 
Tulipomaliza kunywa chai, mimi nilitoka kwenda kuzunguukazunguuka. Nilirudi nyumbani saa sita mchana. Mke wangu akaniuliza. 
 
“Una njaa, nipike ugali?”
 
 “Pika”
 
Akaenda jikoni. Na mimi nikajipunzisha kitandani. Hapohapo usingizi ukanichukua. Mke wangu alikuja kuniamsha majira ya saa nane na kuniambia. 
 
“Chakula kimeiva”
 
Tulipomaliza kula akaniambia anakwenda kumtembelea bibi. Mimi nikabaki pale nyumbani.
 
Chausiku alipoondoka hakurudi tena hadi saa moja usiku. Akapika chakula cha usiku. Milo yetu ya kijijini haina masharti. Mchana mnaweza kula ugali na matembere na usiku mnakula tena ugali huo huo.
 
Baada ya kula hatukukaa sana, tukaenda kulala. Kama kawaida yake mke wangu aliniamsha usiku wa manane.Tukatoka.
 
Tulipofika kiwanjani tuliwakuta baadhi ya wenzetu walikuwa wameshafika. Bibi akatupangia kazi. Vile vitendo vyetu vya kichawi tulivichukulia kama kazi.
 
Siku ile bibi alinipanga mimi na wanawake wawili twende nyumbani kwa mwalimu mkuu wa ile shule anakouzia mbaazi zake tukamchawie. Kisa, alimwambia yule bibi atamfukuza asipeleke mbaazi zake shuleni hapo  kwa vile wanafunzi na walimu wanaokula mbaazi hizo wanaharisha. Kauli hiyo ilimuudhi yule bibi.
 
Mke wangu na wenzake wengine walitumwa sehemu zingine zingine.
 
Nyumbani kwa mwalimu mkuu hakukuwa mbali sana na pale kwenye kiwanja chetu.Tukaenda.
 
Kama kawaida tulipofika, wachawi wenzangu wakapiga pindu kwenye mlango wa nyumba ya mwalimu mkuu huyo.Wakaniambia na mimi nipige pindu, nikapiga pindu. Kisha tukazunguka duara na kuanza kucheza ngoma ya kichawi barazani mwa ile nyumba. Zile pindu tulizopiga zilikuwa na malengo ya kufanikisha ile kazi ya kichawi iliyotupeleka hapo. Na ile ngoma ilikuwa ni ya kuwalaza usingizi watu wote waliokuwemo mle ndani.
 
Tulipomaliza kucheza ngoma hiyo ikafuatia kazi ya kujipenyeza kiuchawi ndani ya ile nyumba. Laiti ningejua ni kitu gani kitatutokea humo ndani, nisingekubali kuingia humo ndani.
 
Je ni nini kitakachotokea? Usikose hapo kesho hapa hapa tangakumekuchablog
Imechapishwa na Unknown kwa 2:39 AM
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Time

 Time in Tanga

Total Pageviews

My Blog List

Blog Archive

  • ►  2014 (563)
    • ►  November (97)
    • ►  December (466)
  • ►  2015 (3131)
    • ►  January (417)
    • ►  February (332)
    • ►  March (351)
    • ►  April (308)
    • ►  May (263)
    • ►  June (255)
    • ►  July (260)
    • ►  August (246)
    • ►  September (237)
    • ►  October (210)
    • ►  November (142)
    • ►  December (110)
  • ▼  2016 (1913)
    • ►  January (121)
    • ►  February (102)
    • ►  March (131)
    • ►  April (198)
    • ▼  May (196)
      • JAPAN KUIPIKU DUBAI KUJENGA MNARA MREFU ZAIDI DUNIANI
      • NI HISTORIA MAN UNITED
      • MAANDALIZI YA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI
      • BESIGYE NGANGARI, HATAKI WAKILI
      • AVUNJA RIKODI YA KUNUNUA ALMASI NDOGO KWA MABILION...
      • KIKONGWE APAMBANA NA MAMBA KATIKA MAJI NA KUJIOKOA
      • HADITHI SITASAHAU NILIVYOGEZUWA PAKA SEHEMU YA 18
      • ALAMBWA FAINI MAHAKAMANI KWA KUPEKUA SIMU YA MUMEWE
      • KIPENGA LIGI NGAZI YA WILAYA YA TANGA KUPULIZWA MA...
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • MTU MWENYE UMRI MREFU ZAIDI DUNIANI ATOA YA MOYONI
      • EGYPT AIR YAPOTEA ANGANI IKIWA NA ABIRIA 56
      • LIVEPOOL YACHAPWA KIPIGO CHA MWAKA YAACHIA KOMBE
      • SITOSAHAU NILIVYOGEUZWA PAKA SEHEMU YA 19
      • KLABU KUADHIBIWA LUNINGA KUONYESHA VITI VITUPU
      • SITASAHAU NILIVYOGEUZWA PAKA
      • BONDIA MANNY PACQUIAO ASHINDA USENETA
      • MABAKI YA NDEGE YA EGYPT AIR YAPATIKANA
      • SAKATA LA MATEKA WA BOKO HARAMU , MWENGINE APATIKANA
      • SAA YA HAILE SELASSIE ILIYOIBWA WAKATI WA MAPINDUZ...
      • ABAMBWA AKICHUPA UKUTA WA KASRI LA MALKIA WA UINGE...
      • KITWANGA ATWANGWA BUNGENI
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • SITOSAHAU NILIVYOGUZWA PAKA SEHEMU YA 21
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • MANCHESTER UNITED YATWA KOMBE LA FA YAIFIKIA RIKOD...
      • MELI KUBWA ZAIDI DUNIANI YAZINDULIWA
      • SITASAHAU NILIVYOGEUZWA PAKA SEHEMU YA 22
      • TUNAVUA KAMBARE
      • MOURINHO KUWA BOSI MPYA WA MAN U
      • PALE TAA ZA KUONGOZEA MAGARI ZINAPOZIMIKA, UDART N...
      • TIMU TATU ZA TANGA ZASHUKA DARAJA, NI HISTORIA
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUACTION CENTRE TANGA
      • BIASHARA BARABARANI
      • WASAFIRI MABASI YAENDAYO MIKOANI WALALAMIKA
      • SITASAHAU NILIVYOGEUZWA PAKA (MWISHO)
      • MAANDAMANO KENYA YAZIMWA
      • WATU ZAIDI YA 10 WAHOFIWA KUFA ZIWA NYASA
      • ATAKAYEHUSISHA DAWA ZA KULEVYA NA WATOTO JELA MIAK...
      • NDONDI, TUHUMA
      • MAROKETI YARINDIMA KAMA MVUA SYRIA
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • UJERUMANI YAZINDUA NDEGE INAYOTUMIA UMEME
      • MDEMU NAIBU MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI
      • DONALD TRUMP KUUZA MJENGO WAKE KUSAIDIA KAMPENI
      • PAPA FRANCIS AKUTANA NA KIONGOZI WA KIDINI MISRI
      • WANASAYANSI CHINA KUTUMIA NGURUWE KUTIBU UPOFU
      • ELIMU YA UTUMIAJI BARABARA YA JUU DAR ES SAALM BAD...
      • KUMEKUCHA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA
      • HELKOPTA ZA URUSI ZATEKETEA
      • MWANAMKE SEHEMU YA 1
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • MISA TANZANIA YAWAJENGEA UWEZO WA MATUMIZI YA INTE...
      • NDEGE INAYOTUMIA NGUVU YA JUA YAFANYA SAFARI YA MW...
      • HOSPITALI YA BOMBO TANGA YAPATA COMPUTER SYSTEM
      • WAPINZANI KENYA WASITISHA MAANDAMANO
      • POUL SCHOOL AMPIGIA CHEPUO MOURINHO
      • HADITHI, MWANAMKE SEHEMU YA 2
      • AKIRI MAHAKAMANI KUIBA PICHA CHAFU
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • CHEMBA LAWA KERO KWA WAKAZI WA MTAA WA USAGARA
      • VUTA NIKUVUTE HUAWEI NA SAMSUNG
      • KIFAA CHA KWANZA CHATUA EMIRATER
      • IBRAHIMOVIC AHUSISHWA KUJIUNGA NA MAN UNITED
      • HADITHI MWANAMKE SEHEMU YA 3
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • MOURINHO ATUA RASMI MAN UNITED
      • TRUMP AKOSOLEWA
      • MISA - TANZANIA YAWAWEZESHA WAANDISHI WA TANGA KUF...
      • JINO LA NYANGUMI ALIEISHI MIAKA MILIONI TANO LAPAT...
      • KALI YA DUNIA
      • MOURINHO RASMI OLD TRAFORD
      • ANG'ATWA NA NYOKA WAKATI AKIENDA HAJA CHOONI
      • HADITHI MWANAMKE SEHEMU YA 4
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • MISA - TANZANIA YAWAWEZESHA WAANDISHI WA HABARI WA...
      • PUNDA KUVALISHWA NEPI KULINDA USAFI WA MAZINGIRA
      • KOREA KUSINI NA KASKAZINI ZATUNISHIANA MISULI
      • WHO LAONDOA HAFU UGONJWA WA ZIKA OLIMPIC
      • MACHUNGWA YAOZA HAYANA SOKO , TANGA
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • REAL MADRID YATWAA KOMBE LA UEFA
      • HADITHI MWANAMKE SEHEMU YA 5
      • MAONYESHO YA BIASHARA TANTRADE YAFUNGULIWA TANGA LEO
      • SEIKALI YATANGAZA RASMI MWISHO WA MATUMIZI MATUMIZ...
      • WAJASIRIAMALI TANGA WAFUNDWA
      • WAHAMIAJI 700 WAHOFIWA KUFA MAJI ITALY
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • TRUMPH KUKOMESHA MALIPO KWA WAGENI
      • HADITHI MWANAMKE SEHEMU YA 6
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • UEFA YATAJA MAJINA 18 KIKOSI BORA 2016
      • HADITHI , MWANAMKE SEHEMU YA 7
      • TANGAZO LA UBAGUZI WA RANGI LAZUA UTATA CHINA
      • MAJAMBAZI TANGA WATIKISA TENA WAUWA WATU 8 FAMILIA...
      • KOMBORA LA KOREA KASKAZINI LAFELI
      • UVUTAJI SHISHA NI HATARI
      • AMKA NA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA
      • INDIA NA MIPANGO YA USAMBAZAJI CHAKULA NA MAJI KWA...
      • PICHA 10 KIJIJI CHA MABATINI KILICHOKUBWA NA MAAFA...
    • ►  June (197)
    • ►  July (197)
    • ►  August (186)
    • ►  September (159)
    • ►  October (160)
    • ►  November (138)
    • ►  December (128)
  • ►  2017 (562)
    • ►  January (134)
    • ►  February (106)
    • ►  March (113)
    • ►  April (77)
    • ►  May (72)
    • ►  June (11)
    • ►  September (1)
    • ►  October (36)
    • ►  November (10)
    • ►  December (2)
  • ►  2018 (1)
    • ►  February (1)
Picture Window theme. Powered by Blogger.