Upinzani wasitisha maandamano Kenya
Muungano huo wa Coalition for Reforms and and Democracy (CORD) umeipa serikali makataa ya siku 10 la sivyo urejelee maandamano hayo.
Viongozi wa CORD wanataka maafisa wakuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (IEBC) wajiuzulu wakisema tume hiyo haiwezi kuandaa uchaguzi mkuu huru na wa haki mwaka ujao.
Walikuwa wameandaa kuandamana hadi afisi za tume hiyo miji mbalimbali nchini Kenya hadi maafisa hao wajiuzulu.
Maandamano hayo yamekuwa yakikumbwa na vurugu huku polisi wakishutumiwa na mashirika ya kutetea haki za kibinadamu kwa kutumia nguvu kupita kiasi.
Msemaji wa serikali Eric Kiraithe Jumanne aliambia wanahabari kwamba maafisa 29 wa polisi walijeruhiwa wakati wa maandamano hayo.
Serikali hiyo imesema maandamano hayo ni haramu.
BBC
No comments:
Post a Comment