Aliyeingia ndani ya kasri la Malkia akamatwa
Mshukiwa huyo ambaye hakuwa na silaha yoyote alikamatwa kwa kushukiwa kuingia eneo linalolindwa na sasa yuko kizuizini.
Inafahamika kuwa Malkia alikuwa ndani ya kasri wakati wa kisa hicho.
Kumeshuhudiwa utata mara kadha kwenye ulinzi wa kasri la Buckingham miaka ya nyuma, kikiwemo kisa cha Michael Fagan ambaye aliingia hadi chumba cha kulala cha Malkia mwaka 1982, na kukaa kwa muda wa dakika 10 akizungumza na malkia kabla ya Malkia kufanikiwa kupiga king'ora wakati mtu huyo alipoomba sigara.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog
No comments:
Post a Comment