Ibada ya Hajj yafika kilele chake mlima Arafat
Ibada ya Hajj
nchini Saudia imefika kilele chake huku takriban Waislamu milioni 1.5
wakikongamana katika mlima Arafat ili kufanya maombi ya siku nzima
mbali na kusoma Quran.
Mahujaji hao walikongamana katika mlima huo wakati wa macheo ambao uko takriban kilomita 15 kutoka mji wa Mecca.Waislamu wanaamini kwamba mtume Muhammad alitoa hotuba yake ya mwisho katika eneo hilo.
Nguzo ya Hajj ni mojawapo ya nguzo tano za kiislamu ambayo Waislamu hutakiwa kuitekeleza ijapokuwa mara moja.
No comments:
Post a Comment