Taarifa kubwa kutoka Kenya zilizosikika kwenye vyombo mbalimbali vya habari jana Jan 5
Walimu saba raia wa Kenya wamejeruhiwa
baada ya kulipukiwa na bomu lililokuwa limetegwa kando ya barabara
Somalia, mtu mmoja alifariki kutokana na mlipuko huo uliokuwa umelenga
basi la shule.
Watu watatu wamefariki na majeruhi
wametajwa kuongezeka kutoka na kuanguka kwa jengo la ghorofa saba huko
Nairobi, Mkurugenzi wa CID Ndegwa Muhoro ameagiza wahusika wote kujisalimisha kituo cha Polisi.
Rais Uhuru Kenyatta ameitembelea familia ya Raila Odinga kuwapa pole ya kufiwa na mtoto wa kwanza wa Odinga, Fidel Odinga ambaye alifariki usiku wa kuamkia juzi Jumapili katika mazingira ya kutatanisha nyumbani kwao.
No comments:
Post a Comment