Monday, January 5, 2015

MBUNI ALETA KIZAA AKIKATISHA BARABARA


Itazame hii ya mbuni aliyetia kizaazaa katika foleni ya magari

Kruger-National-Park-2-ostrichesWanyama pori wanapoingia mjini lazima itokee tafrani, hii inaonyesha mbuni aliyekatisha barabarani katika mataa ya kuongozea magari huko Israel.
Mvua kubwa ilikuwa imenyesha, katikati ya barabara alionekana mbuni huyo anakatisha akikimbia akiongozana na magari, baada ya kufika mbele taa za kuongozea magari zilisimamisha magari ya upande huo lakini kwa kuwa mbuni huyo hakujua utaratibu huo, aliendelea na safari yake ambapo ilibaki kidogo asababishe ajali.
cegrab-20150105-125754-139-2-2048x1152-20150105-140520-698
Msemaji wa manispaa ya Herzliya, Dorit Basman amesema ndege huyo alikuwa ametoroka kutoka katika bustani ya mtu binafsi, ambapo walinzi walifanikiwa kumkamata na kumrudisha salama kwa mmiliki wake.
Tumia sekunde 43, kutazama video hii  kwa kubonyeza play  mtu wangu.

Nakuhakikishia kwamba nitakufikishia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupiti,kumekuchablog

No comments:

Post a Comment