Itazame hii ya mbuni aliyetia kizaazaa katika foleni ya magari
Mvua kubwa ilikuwa imenyesha, katikati
ya barabara alionekana mbuni huyo anakatisha akikimbia akiongozana na
magari, baada ya kufika mbele taa za kuongozea magari zilisimamisha
magari ya upande huo lakini kwa kuwa mbuni huyo hakujua utaratibu huo,
aliendelea na safari yake ambapo ilibaki kidogo asababishe ajali.
Msemaji wa manispaa ya Herzliya, Dorit Basman amesema
ndege huyo alikuwa ametoroka kutoka katika bustani ya mtu binafsi,
ambapo walinzi walifanikiwa kumkamata na kumrudisha salama kwa mmiliki
wake.
Tumia sekunde 43, kutazama video hii kwa kubonyeza play mtu wangu.
Nakuhakikishia kwamba nitakufikishia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupiti,kumekuchablog
No comments:
Post a Comment