HADITHI
KISIWA CHA HARISHI (26)
ILIPOISHIA TOLEO LILILOPITA
“Yasmin tumeepuka kifo cha
aina moja, sasa tunakabiliwa na kifo cha aina nyingine” nikamwambia Yasmin.
“Kifo gani tena?”
“Tutaondokaje kwenye kisiwa
hiki?”
“Usijali. Mungu mkubwa”
Tukarudi katika lile jumba.
Tulipofika tulioga maji baridi. Yasmin alinitolea “Ni kwa nguo za kiume
alizokuwa akiletewa na Harishi, akaniambia nivae.
Kwa vile kulikuwa
kumeshakucha alipikauji aliouchanganya na asali, tukanywa. Kwa sababu moyo
wangu ulikuwa umetulia nilikunywa vikombe vitatu.
Wakati nakunywa kikombe cha
tatu Yasmin akaniambia.
“Leo umekunywa uji mwingi
kuliko siku zote!”
sababu nina njaa na roho
yangu imetulia”
“Yasmin akacheka.
“Jana hukutaka kula kabisa!”
akaniambia.
“Ni kwa sababu ya yule
mshenzi, alinisababishia hofu sana”
“Sijui ulipata wapi akili ya
kufunga kile kizibo?”
“Niiona tu akili yangu
ikinituma nikifunge nilipoona ule moshi”
“Pengine ni kwa sababu ya
zile dua ulizokuwa ukiomba tangu juzi”
“Pengine”
SASA ENDELEA
Wakati tunajadiliana na
Yasmin tulishituka tulipoona wazungu wawili wanaume namtu mweusi mmoja
wakiingia ndani ya ile nyumba.
Nguo zao zilikuwa zimeroa
maji. Walionekana walikuwa wamatoka baharini.
Tukapatwa na uoga kwa vile
hakukuwa na watu waliokuwa wakifika katika kisiwa kile.
Tulikuwa tumekaa pale ukumbini
Yasmin akanyanyuka na kuwauliza kwa Kiswahili.
“Nyinyi ni kina nani”
“Samahani jamani. Tumekuja
kuomba msaada” Yule mtu mweusiakatuambia.
“Mnatoka wapi?”
“Tunatoka Zanzibar. Chombo
chetu kilipigwa na dharuba kimepinduka. Tumeogelea hadi tumetokea katika kisiwa
hiki”
“Nyinyi ni kina nani” Yasmin
akawauliza tena.
“Hawa wenzangu ni watalii
wanatoka Ufaransa. Mimi ni Mzanzibari. Nilikuwa nawatembeza kwa boti kwenye
Bahari ya Hinndi ndio tukapatwa na ajali”
“Mimi pia najua Kifaransa,
ngoja niwaulize” Yasmin akasema na
kuwageukia wale wazungu. Aliwauliza maswali kwa kutumia lugha ya Kifaransa.
Wazungu hao walimjibu na kufurahi kuona Yasmin alikuwa akizungumza lugha yao.
“Karibuni make” Yasmin
akawambia kwa Kifaransa.
Watu hao watatu wakakaa
chini.
“Kwanza tunawapa pole sana kutokana na mkasa
uliowafika. Mmesema kuwa mnaomba msaada, mtufahamishe mnaomba msaada gani?”
Yasmin aliwauliza.
Msaada wowote tu unaostahili
kwa binaadamu kwani tumezunguka sana
katika kisiwa hiki hatukuona mtu yeyote. Tulichoona ni nyumba tupu na kwingine
tulikuta mafuvu na mifupa ya bianaadamu” Mzanzibari alisema.
“Ni kweli” Yasmin alimjibu.
“Ni kwanini?”
“Kwanza mlitakiwa mshukuru
kuwa mmefika katika kisiwa hiki katika muda mzuri, vinginevyo na nyinyi
mngekuwa kama yale mafuvu mliyoyaona”
“Kwa niaba ya wenzangu nasema
kuwa tumeshukuru lakini tuna shauku ya kutaka kujua kilichotokea mpaka mkabaki
nyinyi peke yenu”
“Nitawaeleza”
Ndipo Yasmin alipoanza
kuwaeleza kisa cha kisiwa hicho. Alianza kwa kujitambulisha kuwa yeye ni binti
wa Rais wa Comoro na jina lake
ni Yasmin. Akawambia
kwamba alisoma elimu yake nchini Ufaransa na ndiyo sababu akawa anajua
kuzungumza Kifaransa.
Akaeleza alivyoposwa na mwana
wa mkuu wa majeshi nchini mwao lakini siku ile ya harusi akakumbwa na jini
anayeitwa Harishi ambaye alimpeleka katika kisiwa hicho na kumgeuza mke wake.
“Sikujua nilivyofika katika
kisiwa hiki. Nilijishitukia tu nikiwa ndani ya jumba hili nikiwa sijielewi”
Akasema.
Watu hao watatu, wazungu
wawili na Mzanzibari mmoja walishikwa na mshangao mkubwa kusikia habari ile.
Yasmin aliendelea kuwaeleza
kuwa jini aliyemkumba ndiye aliyekuwa akiua watu katika kisiwa hicho kwa
kuwafyonza damu na kula ubongo wao.
“Aliwamaliza watu wote
waliokuwa katika kisiwa hiki na kuacha majumba yakiwa matupu. Niliishi peke
yangu kwa karibu mwaka mzima” Yasmin alieleza.
Aliendelea kuwaeleza jinsi
tulivyofika katika kisiwa hicho na kumkuta yeye ndani ya jumba hilo na jinsi tulivyoanza kuuawa na Harishi
mmoja mmoja hadi nikabaki peke yangu.
Ni dhahiri kuwa maelezo ya
Yasmin yalikuwa yamewatia hofu watu hao kwani nyuso zao zilizidi kupata fadhaa.
“Mungu ni mkubwa” Yasmin
alisema kabla ya kueleza jinsi walivyofanikiwa kumfungia Harishi kwenye chupa
na kwenda kuizamisha baharini asubuhi ile.
“Hiki ni kisa cha ajabu kweli
kweli. Je tunaweza kwenda kuiona hiyo chupa? mzungu mmoja akauliza.
“Hatuwezi kujua tumeizamisha
wapi lakini kwa sasa Harishi yuko chini ya Bahari”
“Je hao watu waliouawa
tunaweza kuwaona?”
“Hao mnaweza kuwaona”
“Tunaomba mtupeleke tukawaone
kama hamtajali”
Yasmin akanitazama.
“Umeridhika twende
tukawaoneshe hawa wageni miili ya ndugu zako?” akaniuliza.
“Nimeridhika” nikamjibu.
Yasmin akawambia wale watu
“Twendeni”
Tukaondoka sote watu wanne.
Yasmin alianza kuwaonesha miili ya wenzetu waliouawa ambayo ilikuwa karibu na
lile jumba. Walikuwa ni wale wenzangu waliouawa mwanzo mwanzo.
Yasmin alikuwa akieleza jinsi
watu hao walivyokuwa wakiuawa kila siku mmoja baada ya mwingine.
Tukaenda mbali zaidi katika
ile nyumba aliyouawa Haji. Wazungu hao pamoja na Mzanzibari waliyekuwa naye
wakauona mwili wa Haji.
Mimi nilitakiwa kueleza
alivyouawa Haji. Nikaeleza kwa Kiswahili huku Yasmin akitafsiri kwa kKifaransa.
Baada ya hapo tulikwenda
katika nyumba aliyouawa Shazume.
Tuliwaonesha mwili wa Shazume
na nikawaeleza jinsi Shazume alivyouawa.
“Hapa ndipo nilipokata tamaa
kabisa. Nilijua na mimi ningeuawa leo” nilisema.
Yasmin akaeleza kuwa nay eye
alikuwa ameshajitolea kufa kwa ajili yangu.
“Nilisema kama atauawa basi
tuuawe sote” akasema na kuongeza.
“Niliona Hakuna haja ya
kuendelea kujificha. Nilimwambia mwenzangu twende kule ninakoishi. Harishi
akija atukute sote”
Wazungu hao walimsifu Yasmin
kuwa alikuwa msichana jasiri na mwenye moyo.
“Kumbe na sisi tungekuja
kufa!” Mzanzibari naye aling’aka.
“Ndiyo maana niliwambia
mwanzo kuwa mshukuru kwa kufika katika kisiwa hiki katika kipindi cha usalama”
Yasmin akawambia.
“Sasa kule nyumbani Comoro
wanajua uko wapi?” Yule Mzanzibari alendelea kumuuliza Yasmin.
“Wao hawajui niko wapi na kwa
sasa wanaamini kuwa nimeshakufa”
“Je wakikuona tena
itakuwaje?”
“Itakuwa mshangao mkubwa.
Wazazi wangu hawataamini”
“Ni mkasa wa kutisha kweli na
unastahili kuandikwa katika historia ya Comoro”
“Hapo ni kama tutanusurika na
nitarudi kwetu kwani kama niivyowambia mwanzo
hapa hatutarajii kupata msaada wowote. Hatima yetu tumemwachia Mwenyezi Mungu”
ITAENDELEA KESHO,USIKOSE NINI KITAJIRI KATIKA SEHEMU IFUATAYO KESHO
No comments:
Post a Comment