Wednesday, August 3, 2016

POLISI TANGA WAUWA MAJAMBAZI WAWILI



Tangakumekuchablog
Tanga, JESHI la Polisi Mkoani hapa  limewauwa  watu wawili  wanaodhaniwa kuwa majambazi kwa kuwapiga risasi wakati wa majibizano ya  risasi kwenye msitu wa Pongwe nje kidogo ya jiji la Tanga.
Majambazi hao ambayo kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Tanga, Leonard Poul, amesema kwa wiki mmoja mfululizo walikuwa wakifanya uporaji kwenye maduka makubwa na Raia wa kigeni.
Akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake, kamanda Poul amesema utupianaji wa risasi ulianzia mjini Tanga  baada ya majambazi hayo kukimbia baada ya kufanya uporaji wao kwa kutumia pikipiki.
Kamanda amewapongeza waendesha pikipiki maarufu kama Bodaboda kwa ushirikiano wao kwa kushiriki kikamilifu kuwafukuza majambazi hayo hadi kwenye msitu wa Pongwe na kufanikiwa kuwauwa.
Amesema kuuwawa kwa majambazi hayo kulitokana na kuishiwa kwa risasi walizokuwa na nazo na badala yake kujificha kwa kupanda katika miti na wakati wa msako huo walionekana wakiparamia juu ya miti.
                                                Mwisho


Kamanda wa polisi Mkoani Tanga, Leonard Poul, akiwaonyesha waandishi wa habari dawa ambayo vibaka wamekuwa wakiitumia kupuliza katika madirisha ya nyumba usiku na kwenye vioo vya magari na ambavyo hulainisha na kuweza kuiba kwa urahisi.


 Kamanda wa polisi Mkoani Tanga, Leonard Poul, akiwaonyesha waandishi wa habari kioo cha gari kilichopakwa dawa na kulainika na wizi kufungua mlango na kuiba vitu vilivyokuwemo ndani.


Mwalimu wa shule ya msingi ya Pongwe halmashauri ya jiji la Tanga, Dominica Tarimo akizungumza na waandisi baada ya watu wanaoaminika kuwa waizi kupaka dawa kwenye kioo cha gari yake kiliolainisha na kuweza kufungua mlango na kuiba vitu vyote vilivyokuwemo ndani.

No comments:

Post a Comment