Tuesday, November 7, 2017

SIMULIZI, TAMAA MBELE MAUTI NYUMA SEHEMU YA 10

AMAA MBELE, MAUTI NYUMA 10

ILIPOISHIA

“Halafu nitoke naye?” Herieth akamuuliza Sara.

“Toka naye, kwani kuna tatizo gani! Atakuchuukua nyumbani kwake”

“Lakini pesa yake haina tabu?”

“Haina tabu kabisa. Dhamana yako ni mimi”

Saa tatu usiku jamaa huyo akawasili. Alikuwa Njoroge. Sara akamkutanisha na Herieth, wakayazungumza na kukubaliana kuwa usiku ule Herieth akalale kwa Njoroge.

Kutoka saa tatu usiku Njoroge aliendelea kunywa bia hadi saa sita baa ilipofungwa. Akaondoka na Herieth kwa teksi kuelekea nyumbani kwake.

Kutoka siku hiyo Herieth na Njoroge wakawa wapenzi. Mapenzi yaliponoga Herieth akahamia kwa Njoroge. Baada ya kuishi kwa mwaka mmoja wakakubaliana kuwa wachumba.

SASA ENDELEA

Wakati huo Herieth hakuwa Herieth yule aliyetoka Kiambu. Alikuwa Herieth mwingine aliyenawiri na kujisikia. Alikuwa mrembo ambaye shida ndogo ndogo zilimpitia mbali.

Sara alihisi kwamba Njoroge alikuwa mwanaume makini aliyeweza kutunza mwanamke kuliko alivyokuwa  akimdhania. Aliamini kuwa yeye ndiye aliyebadili maisha ya Herieth.

Akajiambia laiti angempata yeye angeweza kuyabadili maisha yake na kuwa bora zaidi. Akaona kwamba alifanya kosa kumpeleka mwanaume huyo kwa rafiki yake badala ya kubaki naye yeye.

Ndipo alipoanza kufikiria kumnyang’anya Herieth mwanaume huyo. Alianza kwa kumrembulia macho Njoroge na kumfanyia dhihaka za makusudi ili Njoroge amuone kuwa alikuwa na kitu ndani ya moyo wake.

Wakati huo Herieth hakuwa ametambua kilichokuwa ndani ya mawazo ya mwenzake. Aliuchukulia mzaha wa Sara kwa mwanaume wake ni wa ushemeji tu.

Kulikuwa na siku moja ambayo Herieth na Sara walikuwa kwenye mapumziko. Njoroge alifika hapo baa na kukuta ujumbe kuwa amfuate Sara nyumbani kwake kwa vile alikuwa na shida naye muhimu.

Kutokana na wito huo Njoroge baada  ya kupata chupa tatu za bia alindoka akapanda matatu na kwenda nyumbani kwa Sara.

Si unajua matatu ya Kenya hususani ya Mombasa yako na misemo kila aina na utachoka wewe mwenyewe kusoma na kila moja ni zuri zaidi ya mwenzake, mie matatu niliyopanda ilikuwa na jina lililoandikwa "Mpende akupendae"

Alipoingia chumbani kwake alikuta mambo ambayo hayakuwa ya kawaida. Juu ya meza alikuta chupa kadhaa za bia, nyingine zikiwa tupu na nyingine zikiwa hazijanywewa.

Sara mwenyewe alikuwa amejilaza kitandani akiwa amelewa chakari.

Siku hiyo Sara alikuwa amemtega Njoroge. Alikuwa amevua nguo na kubaki na nguo ya ndani halafu alilala kifudi fudi.

Njoroge alianza kuutupia macho mwili wa Sara akiulinganisha na wa Herieth. Alianzia kwenye miguu, akaona ilikuwa miguu ya bia. Macho yake yakapanda taratibu na kufika kwenye magoti. Yalikuwa magoti ya mfuto.

Macho yaliendelea kwenda. Sasa rangi ya ngozi libadilika, ilikuwa ngozi laini nyeupe kama ya mtoto mchanga. Macho yalizidi kwenda…

Mpaka anafika kwenye kiuno Njoroge alikuwa hoi. Alimeza funda la mate akahisi mwili ukimsisimka.

Zile bia tatu alizokunywa zikawa zimewasha moto ndani ya mwili wake.

Akasogea karibu na kitanda akamuwekea mkono kwenye bega na kumuita.

“Sara! Sara!”

Sauti ya Sara ikasikika kwa mbali ikimuitikia lakini hakuinuka wala kugeuka.

“Mbona uko hivyo?”

“Unasema nini…?”  Sara ikamuuliza kilevi. Alikuwa bado ameuficha uso wake kwenye mto.

“Hebu geuka basi…umelewa kiasi hiki!”

“Nani wewe…?”

“Mimi Njoroge, niliambiwa unaniita”

Sara akaugeza uso wake na kumtazama Njoroge. Macho yake yalikuwa mekundu na hayakuwa yamefumbuka sawa sawa.

“Kaa hapa” Sara akamwambia Njoroge katika hali ya ulevi.

“Nikae wapi?”

“Kaa hapa”

Sara alimuonesha kwenye kitanda alichokuwa amelala. Njoroge akaketi pembeni mwa kitanda. Sara akaliweka paja lake juu ya paja la Njoroge.

“Unasema unatoka wapi?”  akamuuliza.

“Natoka kazini kwako. Nimekuta ujumbe kuwa unaniita”

“Ndio nilikuachia ujumbe huo. Nilitaka tuje tunwe nyumbani”

“Una maana bia zote hizi ulikuwa unakunywa peke yako”

“Ni chache tu. Nyingine nimekuachia wewe”

“Mbona uko hivyo, kwanini umevua nguo?”

“Joto. Nilikuwa nasikia joto sana. Halafu nasikia…”

“Unasikia nini?”

Badala ya kumjibu Sara aliupeleka mkono wake akalipapasa tumbo la Njoroge kisha akaushusha mkono huo taratibu huku akiendelea kupapasa....

Usaliti wa Sara kwa Herieth ulianzia hapo. Baada ya kumtega Njoroge kama alivyoweza kumtega alifanikiwa kumpata siku ile.

Kinyume cha matarajio yake, Njoroge aliondoka nyumbani kwa Sara jua likiwa limeshakuchwa.

Tangu siku ile yeye na Herieth wakawa wanagawana penzi kwa Njoroge bila Herieth kujua.

Siku moja wakati Njoroge na Sara wamekaa nyumbani kwa Sara, Sara alimwambia Njoroge.

“Kwanini huachani na yule mshamba?”

“Kwanini?”

“Sasa wa kazi gani yule, hata halingani na hadhi yako. Huoni aibu kuwa na mwanamke kama yule?”

“Wewe si ndiye uliyenitafutia?”

“Nilikutafutia mbanjuke kwa siku moja tu. Naona mwenzangu sasa unataka uoe kabisa!”

“Nina mpango huo. Nimegundua Herieth ni msichana mtulivu sana”

“Na aende zake, ana utulivu gani, malaya mkubwa! Au ni kwa vile sijakwambia siri zake”

“Siri zake zipi?”

“Hebu achana naye bwana!”

“Siwezi kumuacha Herieth”

“Utamuacha tu, nitahakikisha unamuacha”

Wambeya wa pale baa walikuja wakamwambia Herieth kuwa rafiki yake alikuwa akimsaliti kwa Njoroge. Kwanza Herieth hakuamini lakini kulikuwa na siku moja Herieth alipigiwa simu na mmoja wa marafiki zake aliyemwambia kuwa aende nyumbani kwa Sara akajionee mwenyewe.

Siku hiyo Herieth alikwenda nyumbani kwa Sara kwa teksi. Aliona akipanda matatu angechelewa.

Alipofika alikuta mlango wa chumba cha Sara ulikuwa umefungwa kwa ndani. Akabisha.

Alibisha mara kadhaa hadi aliposikia sauti ya Sara ikitokea chumbani.

“Wewe nani?”

Herieth hakujibu, aliendelea kugonga tu. Hatimaye mlango ukafunguliwa. Sara akatoa kichwa.

Herieth akajitumbukiza ndani ghafla na kumkuta Njoroge akiwa kitandani. Alikuwa na suruali yake lakini hakuwa na shati.

Sara naye alikuwa amevaa khanga moja tu.

Ulikuwa ni mshituko uliotokea mle chumbani.

Mshituko ulianzia kwa Herieth baada ya kumkuta Njoroge akiwa kitandani chumbani kwa rafiki yake huku rafiki mwenyewe akiwa amevaa khanga moja.

Mshituko huo ulimkumba  Njoroge baada ya kumuona Herieth akiingia mle chumbani hali iliyodhihirisha kuwa amefumaniwa.

Sara hakutarajia kuwa Herieth angetokea na angeingia mle chumbani kinguvu. Akawa ameshituka kwa kukutwa na mchumba wa rafiki yake.

Akapigwa na butwaa kwenye mlango.

“Za mwizi ni arobaini. Leo arobaini yenu imefika, nimewafuma. Nilikuja hapa kwa ajili ya kuwafumania nyinyi” Herieth aliwambia kwa hasira kabla ya kumtazama Sara.

“Sikutegemea rafiki yangu kuwa ungeweza kunisaliti kiasi hiki. Asante sana”

Njoroge na Sara walikuwa wamenyamaza kimya. Fumanizi hilo hawakuwa wamelitegemea.

“Nawaacha muendelee na starehe zenu lakini wewe bwana uchumba wetu unaishia hapa”

ITAENDELEA kesho usikode uhondo huu hapahapa kumekucha.com

No comments:

Post a Comment