Monday, August 31, 2015

ALLINCE FOR DEMOCRATIC CHENGE (ADC) TANGAMANO , TANGA

  Wafuasi wa Chama Cha Allince For Democratic Change wakiwa katika mkuatano wa ufunguzi wa kampeni za Urais uliofanyika katika uwanja wa Tangamano Tanga jana.




 Mgombea Urais wa Zanzibar, Hamadi Rashid akimtambulisha mgomea Urais wa Jam,huri ya Muungano wa Tanzania kupitia cha cha Allince For Democratic Change, (ADC), Lutalosa Yemba katika mkutano wa ufunguzi katika uwanja wa Tangamano Tanga jana.
 Mgombea Urais kupia chama cha Allince For Democratic Change (ADC) Lutalosa Yemba akiwahutubia wafuasi wa chama hicho jana katika ufunguzi wa kampeni za Urais uliofanyika katika uwanja wa Tangamano jana.



WANAOTUMIA MITANDAO YA KIJAMII VIBAYA CHA MOTO HIKI HAPA

Matusi mitandaoni Tanzania mwisho ilikua jana saa tano na dk 59 usiku ! fahamu mengine ya sheria mpya hapa

Huu ndio utakua mwisho wa makosa ya kimtandao Tanzania??? sababu sheria hii imepitishwa na kuanza kutumika leo mahususi kwa wote wanaotumia vibaya mtandao.
Unaambiwa mwisho wa yote ulikua jana August 31 2015 sababu leo September 1 2015 sheria hii ndio imeanza kutumika rasmi baada ya kupitishwa na Bunge mapema 2015 na kusainiwa na Rais Kikwete ikiwa ni miongoni mwa sheria zilizopitishwa na bunge kwa hati ya dharura.
Unafahamu sehemu ya makosa ambayo yanaweza kukufanya ushtakiwe?
  • Kuweka mtandaoni picha za kingono za watoto
  • Kuweka mtandaoni picha za ngono au za utupu
  • Kuweka taarifa za uongo mtandaoni
  • Kuweka taarifa za uchochezi mtandaoni
  • Kutukana au kumdhalilisha mtu
  • Kuweka mtandaoni tetesi zisizothibitishwa
  • Kutukana au kumdhalilisha mtu kwa misingi ya udini/ukabila.
Innocent Mungi kutoka Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) anasema >>>Ambaye atakua anachukua maamuzi ni jeshi la Polisi ambaye kwa mfano mtu akitukana kwenye mtandao au kufanya chochote kinyume na sheria yule aliyetendewa anao wajibu wa kulalamika kwa Polisi, watafanya uchunguzi alafu mwendesha mashtaka ataifikisha hiyo kesi kwa Jaji ambaye ndio atafanya maamuzi kutokana na kesi yenyewe
Sisi kama TCRA tunaweza kuitwa kama mashahidi kwenye hizo kesi, kwahiyo kuanzia August 31 2015 yale maswala ya mazoea ya NATUMA KAMA NILIVYOPOKEA au NINALETA KAMA NILIVYOIOKOTA HUKO, jihadhari sana kwa mfano yule aliyetengeneza amempelekea mtu mmoja lakini wewe umesambaza kwenye group lako la Whatsapp mko 100, utashtakiwa‘ – Innocent Mungi

DE GEA AKWAA KISIKI REAL MADRID

Sababu ya kushindwa kusajiliwa De Gea Real Madrid na maamuzi ya klabu hiyo kwa FIFA viko hapa…

Golikipa wa kimataifa wa Hispania ambaye anaichezea klabu ya Manchester United David De Gea, alikuwa akihusishwa kujiunga na klabu ya Real Madrid ya Hispania, hivyo kila kitu kilikuwa kimesha kuwa sawa ikiwemo maslahi binafsi ya mchezaji.
Football - Manchester United v Arsenal - Barclays Premier League - Old Trafford - 17/5/15 Manchester United's David De Gea applauds fans as he walks down the tunnel after being substituted after sustaining an injury Reuters / Phil Noble Livepic EDITORIAL USE ONLY. No use with unauthorized audio, video, data, fixture lists, club/league logos or "live" services. Online in-match use limited to 45 images, no video emulation. No use in betting, games or single club/league/player publications. Please contact your account representative for further details.
De Gea ambaye aliripotiwa usiku wa August 31 kuwa karibu na kujiunga na Real Madrid timu aliyokuwa akihusishwa kujiunga nayo tokea zamani, mpango wa De Gea kujiunga na timu hiyo ulikwama baada ya viongozi wa Man United kuchelewa kutuma mikataba katika klabu ya Real Madrid, hivyo walituma dakika moja baada ya dirisha la usajili kufungwa.
1415622744685_wps_11_David_De_Gea_of_Mancheste
Tatizo la kuchelewa kwa documents za mikataba hiyo ni mfumo wa usajili wa FIFA ndio umefanya documents kutoka klabu ya Man United kuchelewa kufika kwa Real Madrid, kutokana na Real Madrid kuwa na ushaidi wa hizo documents watakata rufaa FIFA ili wapewe nafasi ya kumsajili De Gea nje ya muda wa usajili kwani mfumo wa FIFA ndio uliochelewesha usajili huo.
51940-lsh
Klabu ya Real Madrid ya Hispania na Man United walikuwa wamekubaliana kuuziana golikipa huyo kwa ada ya pound milioni 29 pamoja na kupewa golikipa Keylor Navas, kama rufaa yao haitashinda watalazimika kusubiri hadi dirisha dogo mwezi January, dirisha la usajili kwa upande wa Hispania na Ufaransa tayari yashafungwa.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

SOMA HABARI KUBWA ZILIZOANDIKWA MAGAZETI YALE LEO, AUG 31 TZ

Uchambuzi huu wa magazeti unaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha  Elimu Cha Candle Education Centre Tanga, Kituo kipo mkabala na bank ya CRDB na kufundisha fani mbalimbali za kielimu na kiufundi simu 0715 772746


MWANANCHI
Mgombea urais wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa, Edward Lowassa amesema kama Watanzania watashindwa kufanya mabadiliko kwa kupiga kura kuing’oa CCM madarakani mwaka huu, hawataweza kufanya hivyo tena, huku akihoji kama vyama tawala mbalimbali katika nchi za bara la Afrika vimeng’oka madarakani: “Kwa nini isiwe CCM”.
Lowassa aliyeambatana na Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye alisema vyama tawala vilivyokuwa rafiki na CCM vimeshang’oka madarakani na kwamba hivi sasa ni zamu ya chama hicho tawala kuondolewa.
“Nataka kura nyingi ili hata wakiiba tushinde, asilimia 90 ziwe zetu hizo 10 waache waibe. Msipoiondoa CCM mwaka huu hatutaiondoa tena, CCM na Tanu walikuwa na marafiki zao lakini karibu wote wameondoka.
“Chama cha Kanu cha nchini Kenya kimeshaondoka madarakani, kile cha Malawi (Malawi Congress Party)  nacho kimeondoka, UNIP (The United National Independence Party cha Zambia) nacho imeondoka na kile chama cha Mzee Obote (Dk Militon) cha Uganda kimeondoka, tunaona pia jinsi Rais wa Zimbabwe (Robert Mugabe) anavyohangaika,Lowassa.
Katika mkutano huo, Lowassa alirudia vipaumbele vya ilani ya uchaguzi ya Ukawa, huku akimponda mgombea ubunge wa Jimbo la Iringa Mjini kwa tiketi ya CCM, Frederick Mwakalebela kuwa hawezi kushinda kwa maelezo kuwa amepanda gari bovu.
Sumaye alieleza ufisadi mbalimbali uliotokea tangu Lowassa alipojiuzulu mwaka 2008, huku akihoji yalipo majina ya wauza dawa za kulevya na majangili ambayo alidai kwa nyakati tofauti Rais Jakaya Kikwete amenukuliwa akisema kuwa anayo.
Mkutano huo ulihudhuriwa na idadi kubwa ya wananchi ambao walianza kufika uwanjani saa nne asubuhi kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa huo. Baada ya kumalizika kwa mkutano huo saa 11.58 jioni, baadhi ya wananchi hao walilisukuma gari la Lowassa na mgombea ubunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya Chadema, Mchungaji Peter Msigwa hadi katikati ya mji huo kabla ya magari hayo kushika kasi na kuwaacha wakiendelea kukimbia barabarani huku wakiimba nyimbo mbalimbali.
Baadhi yao walionekana kubeba kitu mfano wa jeneza na kukivisha bendera ya CCM huku wakisema mwisho wa chama hicho tawala ni Oktoba 25.
Akiwa Mafinga Mjini, Lowassa alisema anahitaji Watanzania wampigie kura si chini ya milioni 10.2 ili awe rais na kumaliza kilio cha wakulima nchini.
Lowassa aliwaeleza wananchi wa Mafinga kuwa amechoshwa na manyanyaso ambayo wakulima wanaendelea kuyapata ikiwamo kukopwa mazao yao na kutozwa ushuru na Serikali bila ya wao kupata faida yoyote.
Lowassa alisema mara atakapochaguliwa kuongoza nchi, kitu kikubwa atakachokifanya kuwasaidia wakulima ni kufuta ushuru wote wa mazao na kuhakikisha wananufaika na jasho wanalolitoa wakati wa kilimo.
Sumaye aliwataka wananchi wa Mafinga kutokuwa na shaka na Ukawa kwa sababu wamejipanga vizuri kuhakikisha wanapata ushindi katika uchaguzi wa Oktoba 25, licha ya CCM kujipanga kupata ushindi wa goli la mkono.
“Tunawaomba Watanzania wachague Ukawa kwa sababu umefika muda wa mabadiliko, tunataka tupate wabunge 300, hizo nafasi nyingine wagawane vyama vingine vilivyo nje ya Ukawa,”Sumaye.
Alisema Serikali ya sasa ni dhaifu kwa sababu wamekuwa wakipeana nafasi ya uongozi kindugu na ushikaji, hali inayofanya wananchi kuendelea kupata shida.
Katika mkutano huo, Waziri wa zamani, Joseph Mungai alipanda jukwaani kumnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, William Mungai ambaye ni mwanaye.
Waziri Mungai aliyewahi kuwa mbunge kwa miaka 35 kupitia CCM na alishika nafasi ya uwaziri katika wizara za Kilimo, Mambo ya Ndani na Elimu, alisema wananchi wa jimbo hilo wanatakiwa kumchagua William kwa sababu mbunge aliyemaliza muda wake hakuweza kuongoza kama alivyofanya yeye.
Alipoulizwa baadaye kuhusu nafasi yake kisiasa, Mungai alisema tangu aliposhtakiwa baada ya kura za maoni mwaka 2010, uanachama wake ndani ya CCM aliuweka kando na kadi yake hajawahi kuilipia.
“Kwa hivyo mimi ni mwanasiasa mstaafu, siko katika chama chochote,” alisema.
MWANANCHI
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa amesema amechoshwa na manyanyaso wanayoendelea kuyapata wakulima hapa nchi kwa kukopwa mazao yao na kutozwa ushuru na serilkali bila ya wao kupata faida yoyote.
Lowassa alisema punde atakapochaguliwa kuongaza nchi kitu kikubwa atakachokifanya kuwasaidia wakulima ni kufuta ushuru wote wa mazao kuhakikisha wakulima wananufaika na jasho wanalolitoa wakati wa kilimo.
Lowasa ameyasema hayo leo wilayani Mufindi alipofanya mkutano wa  hadhara wa kampeni katika Uwanja wa Shule ya Msingi Wambi, mjini Mafinga.
Lowassa alisema watu wamekuwa wakizungumza kuwa CCM ni wezi wa kura kwasababu ni wajanja sana katika kufanya michezo michafu katika chaguzi na maneno hayo si yakuyabeza wala kuyafumbia macho.
“Mimi nataka kila mtu akihifazi vizuri kichinjio chake (kadi ya kupigia kura) na siku ya kupiga kura ikifika nawaomba wanawake na wanaume wajitokeze kwenda kupiga kura ila wakina baba nawaomba mkishapiga kura fanyeni kazi ya kuzilinda kura zenu” Lowassa
NIPASHE
Siku moja baada ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kuzindua kampeni zake wakati wakimtambulisha mgombea urais wao, Edward Lowassa, kwa kishindo jijini Dar es Salaam, mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, ameiponda ilani yao.
Dk. Magufuli amesema CCM ndicho chama chenye ilani inayoeleweka na imetaja mambo yanayogusa Watanzania, na siyo sawa na vyama vingine ambvyo havina ilani na vimeshindwa kuweka vipaumbele vyao.
Akihutubia mkutano wa kampeni wilayani Ludewa, mkoa wa  Njombe na Ruvuma, Dk. Magufuli alisema:
“Hadi sasa hakuna ilani ya Ukawa, leo mnawapa nchi watu ambao ni vyama vinne hadi sasa havijaweka ilani.”
Dk. Magufuli aliahidi kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Njombe hadi Ludewa, ambayo imeshafanyiwa upembuzi yakinifu na michoro kwa ajili ya ujenzi kuanza mwakani.
Mgombea huyo alisema serikali ya awamu ya tano itakuwa ya viwanda kila wilaya na kwamba itaboresha huduma za umeme, majisafi na salama, dawa mahospitalini, barabara za lami na wakulima kutokopwa mazao yao.
Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa jimbo la Ludewa mkoani Njombe na Madaba wa Ruvuma, alisema pia kila kijiji kitakopeshwa Sh. milioni 50 kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vijana na wanawake zikiwa ni jitihada za kujikwamua na umaskini.
Alisema pia serikali ya awamu ya tano itapunguza kama siyo kumaliza kabisa kero mbalimbali katika jamii kama waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda kubughudhiwa na askari wa kikosi cha usalama barabarani na mama lishe kunyang’anywa mali zao.
“Serikali yangu itakuwa ya watu wanyonge, nitahakikisha huduma muhimi za jamii zinapatikana kwa wakati, mawaziri wangu watakuwa wa kuhudumia wanyonge,” alisema.
Alisema alipokuwa waziri alikuwa anaagizwa, lakini kwa sasa atagiza na akimwagiza waziri kupeleka maji sehemu fulani ni lazima afanye hivyo, vinginevyo atafutwa kazi haraka.
Kwa mujibu wa Dk. Magufuli,  kila awamu ya uongozi ina mambo yake na kufafanua kuwa  yaRais wa awamu ya kwanza, Mwalimu Julius Nyerere, ilikuwa na kazi ya kuleta Uhuru na kuwaunganisha Watanzania na leo wamekuwa kitu kimoja.
Alisema awamu ya pili, tatu na nne zimeliwezesha Taifa kupiga hatua kubwa kimaendeleo na serikali yake ya awamu ya tano itakuwa ni ya mchakamchaka wa maendeleo kwa kuwa mazingira mazuri yalitengenezwa na watangulizi wake.
Aliahidi kuwa serikali yake itafanyakazi na vyama vyote, kwa kuwa hakuna anayezaliwa na chama isipokuwa kinachoangaliwa ni maendeleo na kwamba vyama si msingi wa maendeleo.
Alisema kazi kubwa itakayofanywa na serikali yake ni kuufuta umaskini na uchumi kumilikiwa na wanyonge.
NIPASHE
Mgombea udiwani wa Kata ya Bomang’ombe wilayani Hai kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Livingstone Nkya maarufu kama Ferefere, amefariki dunia ghafla muda mfupi baada ya kuzindua kampeni zake za kuwania nafasi hiyo.
Ferefere alifariki jana jioni baada ya kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC ya mjini Moshi, kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Katibu wa CCM Wilaya ya Hai, Allan Kingazi, alilithibitishia Nipashe kwa njia ya simu jana kuwa, mgombea huyo aliaga dunia baada ya kuzindua kampeni za uchaguzi kwenye kata hiyo.
Alisema Ferefere alianza kuhisi afya yake inabadilika na kumfanya kushindwa kuendelea na jukumu la kujieleza, hivyo aliamua kuondoka baada ya mkutano huo na kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi, kabla ya kuhamishiwa KCMC.
Kata ya Bomang’ombe ni miongoni mwa kata mpya tatu zilizogawanywa katika Jimbo la Hai, lililokuwa likiwakilishwa bungeni na Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe.
“Ni kweli mgombea wetu amefariki jana usiku katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC majira ya jioni; na hivi sasa tuko kwenye taratibu za kuandaa mazishi yake. Tunasubiri majibu ya daktari kujua amefariki dunia kutokana na tatizo gani, lakini sisi kama CCM tutasimamisha mgombea mwingine ili kutwaa kata hiyo, Kingazi
Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Hai, Said Mderu alipotafutwa ili kutoa ufafanuzi iwapo uchaguzi huo utaahirishwa au laa, alisema,” Mimi sina taarifa za kifo hicho na kwa sasa nipo njiani, siwezi kuzungumza lolote. Nitafute kesho (leo) nitakuwa na majibu.
Ferefere ambaye pia ni mfanyabiashara maarufu wa maduka ya vileo na vinywaji baridi mjini hapa, alikuwa akigombea kiti hicho, akishindana na mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joe Nkya ambaye naye ni mfanyabiashara wa maduka ya pembejeo za kilimo.
NIPASHE
Aliyewahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Chiligati, amewapiga kijembe makada wanaohama CCM na kujiunga upinzani kuwa ni magamba yanayojivua yenyewe na kukiacha chama hicho kikiwa kisafi na kinachosimamia misingi yake ya kujali  wakulima na wafanyakazi.
Samia Suluhu Hassan, katika Jimbo la Manyoni Mashariki jana, Chiligati alisema CCM miaka ya nyuma iliwahi kuwataka makada waliokuwa na kashfa mbalimbali ambayo walipewa jina la magamba wajiondoe wenyewe na kwamba sasa ndiyo kazi hiyo imeanza kufanyika.
Chiligati ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki na  ametangaza kustaafu siasa, alisema baada ya magamba hayo kujivua na kumalizika, CCM kitabaki kuwa cha wafanyakazi na wakulima kama kilivyokuwa tangu kinaasisiwa.
Alisema CCM kina wanachama zaidi ya milioni saba lakini kuna watu wachache wanakiharibia sifa yake nzuri na kuonekana kama chama cha mafisadi na kimetekwa na  watu wenye fedha nyingi.
Samia aliahidi kwamba ikiwa chama hicho kitashinda uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu, serikali yake itajenga kiwanda cha chokaa katika jimbo hilo ili kiweze kutoa ajira kwa vijana.
Pia aliahidi ujenzi wa barabara mbalimbali, kutatua matatizo ya maji na kulipa fidia wananchi ambao ardhi yao ilichukuliwa na serikali kwa shughuli mbalimbali bila kulipwa.
Samia aliahidi kwamba CCM kikishinda kitaendelea kujenga minara ya simu katika maeneo mbalimbali. Akiomba kura kwa wananchi, mgombea ubunge wa Jimbo la Manyoni (CCM), Yahaya Masare, alisema jimbo hilo lipo nyuma kimaendeleo lakini yeye amejipanga kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi.
Alisema shida ya maji katika jimbo hilo ni kubwa na kuwaahidi wananchi kwamba atashughulikia tatizo hilo ili kulimaliza.
HABARILEO
Aliyewahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Chiligati, amewapiga kijembe makada wanaohama CCM na kujiunga upinzani kuwa ni magamba yanayojivua yenyewe na kukiacha chama hicho kikiwa kisafi na kinachosimamia misingi yake ya kujali  wakulima na wafanyakazi.
Samia Suluhu Hassan, katika Jimbo la Manyoni Mashariki jana, Chiligati alisema CCM miaka ya nyuma iliwahi kuwataka makada waliokuwa na kashfa mbalimbali ambayo walipewa jina la magamba wajiondoe wenyewe na kwamba sasa ndiyo kazi hiyo imeanza kufanyika.
Chiligati ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki na  ametangaza kustaafu siasa, alisema baada ya magamba hayo kujivua na kumalizika, CCM kitabaki kuwa cha wafanyakazi na wakulima kama kilivyokuwa tangu kinaasisiwa.
Alisema CCM kina wanachama zaidi ya milioni saba lakini kuna watu wachache wanakiharibia sifa yake nzuri na kuonekana kama chama cha mafisadi na kimetekwa na  watu wenye fedha nyingi.
Samia aliahidi kwamba ikiwa chama hicho kitashinda uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu, serikali yake itajenga kiwanda cha chokaa katika jimbo hilo ili kiweze kutoa ajira kwa vijana.
Pia aliahidi ujenzi wa barabara mbalimbali, kutatua matatizo ya maji na kulipa fidia wananchi ambao ardhi yao ilichukuliwa na serikali kwa shughuli mbalimbali bila kulipwa.
Akizungumzia tatizo la mawasiliano, Samia aliahidi kwamba CCM kikishinda kitaendelea kujenga minara ya simu katika maeneo mbalimbali.
HABARILEO
Chama cha ACT Wazalendo kimezindua kampeni zake jijini Dar es Salaam kwa kuahidi kitakapopewa ridhaa ya kuongoza nchi, kitaunda serikali ya Umoja wa Kitaifa.
Aidha katika uzinduzi huo ambao viongozi mbalimbali wa chama hicho walihutubia, Mgombea Urais wa chama hicho Anna Mghwira alisema wananchi wakimpa ridhaa, waziri mkuu wake atakuwa Zitto Kabwe.
“Nitakapounda serikali, katika katiba, mtu wa kwanza kusaidiana na rais licha ya makamu, ni Zitto Kabwe, atakuwa Waziri Mkuu katika serikali ya kwanza,” Anna Mghwira ambaye pia alisema atahusisha viongozi waadilifu kutoka CCM, Chadema na vyama vyote vya siasa na taasisi zote kiraia.
Akihutubia mkutano huo uliofanyika viwanja vya Mbagala Zakhem, mgombea huyo, katika kuelekeza nia yake ya kuunda serikali hiyo ya umoja, alisema linapokuja suala la kitaifa, hakuna haja ya kuangalia masuala ya itikadi. “Mimi ni mama, hukusanya watoto wake.
Hata mama wa vifaranga hukusanya vifaranga pamoja na kuviweka kwenye mbawa zake…mimi nina mbawa za moyo…nitaunda serikali ya umoja wa kitaifa itakayotokana na sekta binafsi lakini kutoka watu wazalendo, wenye utu, waadilifu, taasisi za kijamii, mashirika ya kidini, makundi ya umma ili kuunda taswira ya nchi yetu.”
Mghwira alisema taifa linahitaji mabadiliko si ya tu kifikra na kisera, bali pia ya kijinsia kwa kumchagua yeye kuwa Rais wa nchi. Alisema chama chake kinatilia mkazo utu, uzalendo na uadilifu.
Makao makuu Dodoma Aidha alisema, Serikali itakapoundwa itaapishwa Dodoma na watahakikisha wanarudisha kazi kubwa aliyoifanya Rais wa Kwanza, Julius Nyerere ya kuifanya Dodoma kuwa makao makuu ya nchi na serikali lakini siyo makao makuu ya chama.
Alisema kuweka mji huo makao makuu, maana yake ni kuleta watu wote kutoka pande zote za nchi. Vipaumbele Alitaja vipaumbele vyake ni kuwa na mfumo imara na endelevu wa hifadhi ya jamii unaojengea uwezo wananchi kukabiliana na majanga. Alisema asilimia sita pekee ya Watanzania wanafaidika.
“Tutatumia hifadhi ya jamii kama nyenzo ya kukuza akiba nchini ili kuwe na vyanzo vya mitaji ya uwekezaji wa ndani…tutapanua hifadhi ya jamii kufikia makundi yote katika jamii ikiwamo wakulima, wafugaji, mama lishe na bodaboda,” alisema. Kipaumbele kingine alichoahidi ni uchumi shirikishi wenye kuzalisha ajira nyingi na bora.
Alisema watu wengi hawana uhakika na maisha yao kimapato. Aidha alisema, watajikita kwenye uwekezaji wa kilimo na kusimamia uzalishaji wake. Aidha, aliahidi kuhakikisha ardhi na mashamba yote yaliyo chini ya mashirika ya umma, yanachukuliwa na kuwekwa chini ya uzalishaji mdogo.
Kwa upande wa viwanda, alisema atahakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini zinaongeza mapato ya fedha za kigeni. Chama hicho kupitia kwa mgombea, kimesema kitaweka msukumo kwenye bidhaa za nguo na vitakuwapo viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya kilimo na mifugo.
Vipaumbele vingine ni kuhakikisha madini, mafuta na gesi, vinakuwa mali ya wananchi kikatiba. Kuhusu Katiba Mpya, alisema wataruhusu Tume ya Jaji Warioba imalize kazi ya katiba ilikoishia. Mgombea huyo aliendelea kutaja vipambele vyake kuhakikisha anaboresha huduma za afya ikiwamo kudhibiti vifo vya mama na mtoto.
Aliahidi kuondoa tatizo la watoto wa mitaani. Misamaha ya kodi kwa mujibu wake, haitazidi asilimia moja ya pato la taifa na wakati huo huo atadhibiti mianya ya ukwepaji kodi hususani kwa kampuni za kigeni.
Sifa za rais Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kitila Mkumbo, alishauri wananchi kuangalia wagombea urais kama wanalinda haki za walio wengi au ni mateka wa matajiri. Mkumbo alisema, kiongozi mkuu wa nchi, kwa maana ya rais, ana kazi kuu nne ambazo ni fikra na kutoa dira ya nchi jambo ambalo anapaswa kuwa na uwezo wa kufikiri.
“Tatizo ni kufikiri na kutoa dira ya nchi…tunataka rais atakayetoa misingi ya nchi, atatuletea sera..,” alisema Kitila. Alisema kazi ya pili ya rais, ni kuwa mlinzi mkuu wa tunu za taifa huku akisisitiza katika tunu ya umoja, wananchi kuepuka mgombea mwenye tabia za kidini, kikabila na kikanda.
“Rais ndiye mlinzi wa usawa katika taifa…,” alisema na kushauri wananchi kuangalia wanaogombea kama wanaelekea kulinda haki za walio wengi au ni mateka wa matajiri. Alitaja tunu nyingine ni muungano kwa kusema anayeomba urais na kutaka kucheza na muungano lazima akataliwe.
Kuhusu uadilifu, alisema inapaswa aingie rais atakayekoleza vita ya ufisadi . “Kama kuna mtu anataka urais hata kutamka neno ufisadi anaogopa, huyu hatufai hata kidogo,” alisema Kitila.
Akizungumzia demokrasia, alisema nchi imepiga hatua katika demokrasia ambayo inahitaji rais atakayeipeleka mbele. Vile vile alisema katika kuchagua, ni lazima kuangalia mgombea ndani ya chama chake alipatikanaje.
“Kazi nyingine ya rais lazima awe mfano wa binadamu bora katika jamii. Hatumaanishi malaika, tunamaanisha kwamba popote atakapoenda, akisimama wajue huyu ni Mtanzania, awe sura ya utaifa,” alisema na kusisitiza sifa nyingine ya rais itokane na uadilifu wa chama chake.
Kitila alisisitiza, “Mtu asiye mlaghai lazima aliyotuambia jana, na leo yafanane. Akihubiri maji lakini yeye anakunywa wiski, yeye ni mlaghai. Akituambia ni nyeusi jana, leo nyekundu, kesho nyeupe, huyo ni mlaghai.” Alisisitiza kuwa ACT Wazalendo inazingatia misingi na sera huku akibeza vyama vingine kwamba vinauza mbwembwe na ulaghai.
Ukawa wasutwa Kwa upande wake, Meneja wa Kampeni, Habib Mchange, aliisuta Chadema na CUF kupitia viongozi wao akirejea mkutano wa Mwembe Yanga mwaka 2007, walipotaja orodha ya waliowatuhumu kuwa mafisadi papa. “Kipindi kile hawakuwa na Ukawa bali walikuwa na ushirikiano.
Walitaja watu wanaofilisi taifa hili ambao ni watu kumi na moja…kati ya watu hao waliotajwa kuwa ni mafisadi, namba tisa alikuwa ni Lowassa,” alisema Mchange. “Tulikubaliana 2007 kwamba tunapambana na CCM na wana mafisadi. Leo naomba mtafakari…ili tusiwe wajanja wajanja lazima tuseme ukweli.
Unayosema jana ndo hayohayo uyaseme leo,” alisema. Akinyoshea CCM pia vidole, Mchange alilinganisha mgombea wa Ukawa sawa na chupa yenye sumu iliyobandikwa jina la maji. Alinadi chama chake akisisitiza wananchi wakiamini kwa kuwa kimekuja katikati ya sumu mbili za CCM na Ukawa.
Amshangaa Sumaye, Lowassa Mchange alisema anachoona ni kwamba, ufisadi uliokuwa CCM, umezaliana na kutanuka na hatimaye kuhamia Ukawa. “Jana (juzi) Sumaye ametulaghai… Anasema anashangaa kwa nini CCM inaendelea kuaminiwa,” alisema.
Alikumbusha kuhusu mjadala wa kununua ndege ya rais ambayo ilipigiwa kelele, kwamba wakati huo Sumaye ndiye alikuwa Waziri Mkuu. Pia kuhusu ahadi ya Lowassa ya kumwachia huru mwanamuziki Nguza Viking maarufu kama Babu Seya, Mchange alieleza kushangazwa naye kutokana na kile alichosema, wakati anafungwa, ndiye alikuwa Waziri Mkuu.
Mchange alikuwa mkali zaidi katika hotuba yake hasa alipokuwa anazungumzia ufisadi na wizi. “ Kumbe unaruhusiwa kuwaibia Watanzania ukiwa CCM ukirudi upinzani ni msafi. Mwizi ni mwizi tu.
Fisadi ni fisadi tu…Wanatudanganya kwamba kuna Ukawa…waongo. Ukawa wanatafuta rais tu. Ukawa huku chini kwa wapiga kura haupo,” alisema Mchange. Alihoji ni namna gani mgombea urais ataweza kunadi wagombea wa vyama vinavyounda Ukawa ambao wamegoma kuachiana majimbo hususani Jimbo la Tabora Mjini, Serengeti na Segerea.
“Sasa tuwaulize Ukawa Lowassa akipita Tabora mjini atamnadi nani?,” alisema akimaanisha mgombea wa CUF na Chadema wanaogombea jimbo hilo. Zitto Kabwe Alisema ACT Wazalendo wanarejesha miiko ya uongozi.
Alisisitiza kuhusu utaratibu wa chama chake wa kiongozi kutangaza mali na madeni yake. Zitto alisema kila chama kinachogombea, kinasema kitapambana na rushwa na ufisadi bila kueleza ni namna gani watapambana tofauti na ACT Wazalendo ambacho kimesema kitapambana kwa kurejesha miiko ya uongozi.
HABARILEO
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na Mbunge wa Urambo aliyemaliza muda wake, Samuel Sitta ametaka uandaliwe mdahalo kwenye vyombo vya habari kati yake na mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa uelezwe ukweli juu ya ukweli wa sakata la Richmond.
Sitta ambaye alikuwa Spika wa Bunge wakati Lowassa alipojiuzulu kutokana na sakata hilo, alisema katika mdahalo huo, ataeleza ukweli juu ya uhusika wa Lowassa katika sakata hilo na atatoa vielelezo kueleza taifa ufisadi uliokuwa ukifanyika.
Alisema hayo jana kwenye ufunguzi wa kampeni za CCM mkoa wa Shinyanga katika mkutano uliofanyika mjini hapa ambao wagombea wa udiwani na ubunge wa majimbo yote ya mkoani hapa walitambulishwa.
Katika mkutano huo, alisema kujiuzulu kwa Lowassa mwaka 2008, kulitokana na Kamati Teule iliyoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe, kugundua kwamba fedha za walipa kodi zilikuwa zikipotea bure.
Alisema yuko tayari kusimulia kwa umma utajiri wa mgombea huyo wa Chadema. Makundi, urafiki Sitta ambaye ni Waziri wa Afrika Mashariki, ambaye pia alikuwa kwenye kinyang’anyiro cha kutaka kuteuliwa kugombea urais kupitia CCM, alisema wanamwamini Dk John Magufuli katika utendaji wake wa kazi na pia ni kiongozi asiye na makundi au urafiki.
Kweli lazima uwapime viongozi, kwani anayetaka urais lazima achaguliwe kwa kufuata utaratibu, achambuliwe usiogope moshi kama unapikia kuni…lakini mwenzetu Lowassa hakukubaliana na hayo, akaona kaonewa kwa madai anafaa kuwa rais mbona sisi tulikubali?,”Sitta.
Aliendelea kusema, “hali hiyo, ilionesha ndani ya CCM kulikuwa na vyama viwili ambavyo ni ‘CCM Katiba’ na ‘CCM Maslahi’ ambayo alikuwa anaongoza Lowassa na mfuasi wake, Mgeja (aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga ambaye pia alihamia Chadema hivi karibuni).”
Wanachama mapandikizi Sitta alisema CCM ilikuwa imejaa wanachama walio mapandikizi tofauti na sasa ambapo alidai wamekwisha jionesha na kimekuwa chama kizuri kama ilivyokuwa enzi za hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.
Alisisitiza kwamba kitazidi kuimarika na waliobaki wataendelea kutetea ilani na kuhakikisha chama kinaendelea kushika dola. Kwa mujibu wa Sitta, wakati wa mchakato, baada ya kumaliza vikao, Lowassa alikuwa akiitisha vikao vya kundi lake alilolibatiza CCM Maslahi na kuwaagiza wapambe wake kuitisha vyombo vya habari kushambulia watu ambao hawako kwenye mlengo wao.
HABARILEO
Mgombea Urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kupitia Chama Cha Demokrasia (CHADEMA) Edward Lowassa amesema kuwa endapo atafanikiwa kuwa Rais atahakikisha vituo vya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) vinakuwa vyuo vya ufundi Stadi.
Aliyasema hayo mjini Mafinga wilayani Mufindi mkoani Iringa jana wakati wa mkutano wa kampeni kupitia umoja huo na kusema kuwa mara vijana watakapotoka hapo watakuwa na uwezo wa kujiajiri.
Lowassa alisema kuwa kipaumbele chake kikubwa endapo atachaguliwa atakachopigania ni pamoja na elimu mbalimbali ikiwemo ya ufundi ambayo ni rahisi kwa kijana kupata ajira ikiwa ni pamoja na kujiajiri wao wenyewe.
“Umefika wakati sasa kwa kuwekeza kwenye sekta ya elimu hususani elimu ya ufundi ambayo itawasaidia vijana kukabiliana na wimbi la ukosefu wa ajira,” alisema Lowassa.
Aidha alisema kuwa elimu itagharimiwa na serikali kuanzia sekondari hadi chuo kikuu na anajua kuwa fedha za kuwasomesha wanafunzi kwa elimu za sekondari na chuo kikuu zipo.
Kwa upande wake aliyewahi kuwa Waziri Mkuu Frederick Sumaye alisema kuwa lengo kubwa la Ukawa ni kuhakikisha inapata majimbo mengi ya ubunge na udiwani ili waweze kuongoza halmashauri hapa nchini.
MTANZANIA
Mgombea urais wa Ukawa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Edward Lowassa, amesema anahitaji kura milioni 10.2  aweze kushinda uchaguzi mkuu.
Kutokana na hali hiyo amewataka Watanzania wajitokeze kwa wingi kupiga kura Oktoba 25 mwaka huu na   watakapomaliza kumpiga kura, wawe tayari kuzilinda   zisiibwe na Chama Cha Mapinduzi.
Lowassa aliyasema hayo mjini hapa jana alipohutubia maelfu ya wakazi wa Mji wa Iringa katika Uwanja wa Gangilonga.
“Mwaka huu ni lazima CCM waondoke madarakani kwa sababu vyama vikongwe vyote vyenye umri kama wa kwake vimeshaondoka.
“Angalieni Frelimo cha Msumbiji kimeshaondoka, kule Zambia nao chama chao kimeshaondoka, kile chama cha Obote (Milton Obote Rais wa zamani wa Uganda), kimeshaondoka, KANU cha Kenya nacho hakiko tena madarakani ila kimebaki ZANU P F cha Zimbabwe.
“Lakini kumbeni kwamba ili nishinde nahitaji kura milioni 10.2 na hizi zitapatikana tu kama mtajitokeza kupiga na kulinda kura zenu.
Kwa habari, matukio na ichezo ni hapahapa tangakumekuchablog

NUNDU TANGAMANO, TANGA


Tangakumekuchablog

Tanga,MGOMBEA Ubunge jimbo la Tanga mjini, Omari Nundu (CCM), amesema endapo atachaguliwa kuwa Mbunge atahakikisha kero ya upatikanaji  maji na umeme vijijini linapatiwa ufumbuzi na kudai kuwa kutokuwepo kw ahuduma hizo imekuwa chanzo cha umasikini.

Akihutubia katika ufunguzi wa kampeni kwa Wilaya ya Tanga jana, Nundu alisema maji na umeme ni kero kubwa kwa wakazi wa vijijini na hivyo kusema kuwa ndani ya Ubunge wake miaka mitano atahakikisha kero hiyo inamalizwa.

Alisema mbali ya jitihada za Serikali kupelekea umeme katika maeneo mengi ya vijijini lakini bado kuna vijiji huduma hiyo haijawafikia na kushindwa kufanya kazi za maendeleo ikiwemo ya kukoboa nafaka na kuhifadhi vyakula.

“Ndugu zangu na wanachama wenzangu wa chama cha mapinduzi nawaomba munipigie kura nyingi za ushindi ili niweze kukamilisha adhama yangu ya kupeleka umeme na maji vijijini” alisema Nundu na kuongeza

“Sote tunatambua kuwa huwezi kufikia maendeleo kama huna umeme na maji---vitu hivi ni muhimu sana kwa mustakabali wa maisha ya binadamu  kila siku hivyo nawaomba munichagua tuweze kufikia malengo yetu” alisema

Akimnadi mgombea huyo wa Ubunge, Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Henry   Shekifu aliwataka wananchi wa jimbo la Tanga kuhakikisha kura zao wanazipeleka kwa Nundu kwa madai kuwa uwezo wa kuwaletea maendeleo yuko nao.

Aliwataka  kupeleka kura zao kwa wingi  kwa mgombea wa Ubunge na Madiwani wa CCM na kusema uchaguzi huu chama hicho kinataka kuongeza idadi ya viti vya Udiwani kwa kunyakua kata ambazo zimeshikiliwa na wapinzani.

“Kura zetu zote tuzipeleke kwa mbunge na madiwani wa CCM kwani ndio chama ambacho kina sera nzuri zinazotekelezeka----mumeona mambo yaliyofanya na chama hivyo nawaomba mukipatie kura nyingi” alisema Shekifu

Aliwataka kuzitunza vitambulisho vya kupigia kura il kuweza kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Rais, Ubunge na Madiwani na kuacha kudanganywa na watu kuelekea uchaguzi na kukosa haki ya kupiga kura.

                                                   Mwisho







 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa, Henry Shekifu,akimnadi mgombea nafasi ya Ubunge jimbo la Tanga mjini , Omar Nundu, wakati wa uzinduzi wa kampeni zilizozinduliwa uwanja wa Tangamano.
 Washabiki wa Chama Cha Mapinduzi  (CCM) wakifurahia jambo  wakati wa uzindizi wa kampeni jimbo la Tanga za chama hicho uwanja wa Tangamano ambapo mgombea Ubunge Tanga mjini, Omar Nundu alihutubia .

Sunday, August 30, 2015

DE BRUYNE AVUNJA ROKODI YA RAHEEM STERLING

Kevin De Bruyne kavunja rekodi ya Raheem Sterling Manchester City

Klabu ya Manchester City ya Uingereza ambayo ilikuwa ni moja kati ya vilabu vingi vilivyo kuwa vikihusishwa na kumsajili kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Ubelgiji na klabu ya Vfl Wolfsburg ya Ujerumani Kevin De Bruyne, August 30 imetangaza kumsajili rasmi.
Kevin-De-Bruyne-signs-for-Manchester-City
De Bruyne ambaye ana umri wa miaka 24 alisajiliwa muda mchache baada ya kufanyiwa vipimo vya afya, amejiunga katika klabu hiyo kwa mkataba wa miaka sita, Kuwasili Etihad kwa Kevin De Bruyne kunaweka rekodi mpya ya klabu hiyo kwani ndio atakuwa mchezaji wa gharama zaidi katika klabu hiyo.
PAY-Kevin-De-Bruyne-signs-for-Manchester-City (1)
De Bruyne amejiunga na Man City kwa ada ya uhamisho wa pound milioni 54 na kuvunja rekodi ya usajili wa klabu hiyo kwani kabla ya kuwasili klabuni hapo, Raheem Sterling ndio alikuwa mchezaji aliyesajiliwa kwa pesa nyingi zaidi, dau la pound milioni 49 lilitosha kumtoa Liverpool na kumleta Etihad.
Kevin-De-Bruyn-on-his-way-to-Manchester-from-Germany
Uhamisho wa kiungo huyo wa kibelgiji bado unakuwa haujavunja rekodi ya usajili ya wachezaji Uingereza kwani hadi sasa Man United ndio klabu pekee ambayo bado inashikilia rekodi ya usajili kwa dau kubwa baada ya kutumia pound milioni 59.7 kumleta Angel di Maria akitokea Real Madrid ya Hispania msimu uliopita.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

MOPEROO YAKABIDHIWA PIKIPIKI 20 KUKOPESHANA

 Mgombea Ubunge jimbo la Tanga mjini, Omari Nundu, (CCM)  akijaribu moja ya pikipiki 20 zilizotolewa na Kampuni ya Tanzania Chinas Traders and Tourism Development kwa Umoja wa Madereva wa pikipiki na Bajaj (Moperoo Investment) lengo likiwa ni kukopeshana kwa gharama nafuu na  hafla kufanyika jana mtaa wa Mtupie kata ya Chumbageni Tanga.


  Mgombea Ubunge jimbo la Tanga mjini, Omari Nundu (CCM), akimkabidhi dereva wa pikipiki, Mohammed Khalfan moja ya kikipiki 20 zilizotolewa na kampuni ya Tanzania Chinas Traders and Tourism Development kwa Umoja wa Madereva na Bajaj  (Moperoo Investment ) lengo likiwa ni kukopeshana kwa gharama nafuu hafla iliyofanyika jana mtaa wa Mtupie kata ya Chumbageni Tanga.
 Madereva wa pikipiki maarufu kama Bodaboda Tanga, wakiwa wamepanda pikipiki zilizotolewa na kampuni ya Tanzania Chinas Traders and Tourism kwa Umoja wa Madereva na Bajaj Tanga (Moperoo Investment ) ikiwa lengo ni kukopeshana kwa gharama nafuu hafla iliyofanyika jana mtaa wa Mtupie kata ya Chumbageni Tanga.


WAFURAHIA KUICHAPA LIVAPOOL

Shabiki wa West Ham United kafanya hivi kusherehekea ushindi wa goli 3-0 dhidi ya Liverpool

Kwa mujibu wa John High shabiki wa klabu ya West Ham United ya Uingereza amekiri kupitia ukurasa wake wa twitter kuwa ni miaka 52 sasa klabu ya West Ham United haijawahi kuifunga klabu ya Liverpool katika uwanja wake wa nyumbani Anfield.
1
John ambaye ni shabiki wa damu wa West Ham United aliahaidi kupitia account yake ya twitter kuwa endapo West Ham itamfunga Liverpool katika uwanja wake wa nyumbani Anfield atachora tattoo ya matokeo hayo mwilini mwake hivyo baada ya ushindi wa goli 3-0 John amechora tattoo hiyo na majina ya walio funga magoli na muda.
2
Klabu ya West Ham United mara ya mwisho kuifunga klabu ya Liverpool katika uwanja wake wa nyumbani Anfield ni mwaka 1963 hivyo mashabiki wa klabu hiyo wengi wao August 29 ni siku ya kihistoria kwao.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

MANCHESTER YAMNYEMELEA NEYMAR KABLA DIRISHA KUFUNGWA

Siku 3 kabla usajili kufungwa – Neymar ameyasema haya kuhusu kujiunga na Man United 


Yakiwa yamebakia masaa takribani 72 kabla ya dirisha la usajili barani ulaya kufungwa, winga wa kibrazil Neymar ambaye amekuwa akihusishwa na kujiunga na Man United hatimaye ametoa kauli yake.
 
Akizungumza baada ya mchezo wa ushindi wa 1-0 wa Barcelona dhidi ya Malaga, Neymar alisema: ‘Ningependa na nataka kuendelea kubaki Barcelona, haijalishi ofa ya mamilioni mangapi ya paundi kutoka England,’ aliiambia TV3.
‘Watu wangu wa Barca wanaweza kutulia na kuwa na amani.
‘Pale ninaposikia tetesi za kuhama kwangu, huwa sifikirii chochote. Huwa nasikiliza kisha naendelea na shughuli zangu. Nina furaha sana kuwepo Barca na wachezaji wenzangu.’ 
Neymar, 23, anatarajia kuongezewa mkataba wa miaka 5 huku akiwa kipengele cha kuuzwa endapo timu inayomtaka italipa kiasi cha  €250million (£182m).

SOMA HABARI KUBWA ZILIZOPEWA UZITO MAGAZETI YA LEO, AUG 30 TZ

Uchambuzi huu wa magazeti unaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha Elimu Cha Candle Education Centre Tanga, kituo kinaongoza kufaulisha wanafunzi kidato cha pili hadi cha sta na wanaojiendeleza kielimu. Kituo pia kinatoa kozi mbalimbali za kielimu na kiufundi. Kituo kipo Tanga mkabala na Bank ya CRDB simu 0715 772746

MWANANCHI
Wakati Waziri Mkuu wa zamani, Fredrick Sumaye akitangaza kuihama CCM, alidokeza kuwa siku moja chama hicho kitaona umuhimu wake, na jana alianza kuonyesha hilo alipopangua hoja dhidi ya mgombea urais wa Ukawa, Edward Lowassa huku akianika uozo wa Serikali.
Sumaye, ambaye hadi sasa hajatangaza anajiunga na chama gani, jana alikuwa kivutio kwenye uzinduzi wa kampeni za urais za Ukawa, ambayo inaundwa na vyama vya CHADEMA, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD, kiasi cha maelfu ya watu waliofurika kutaka aendelee kuzungumza licha ya muda kuwa finyu.
Akizungumza mbele ya umati huo mkubwa kwenye viwanja vya Jangwani, Sumaye alirejea tena sababu zilizomfanya aingie Ukawa kuwa ni haja ya kufanya mabadiliko wanayotaka Watanzania ambayo alinyimwa nafasi na CCM.
“CCM wanawajaza Watanzania kitu kinaitwa woga wa usilolifahamu au woga wa usilolijua kwa hiyo kila siku wanawaambia Watanzania mkiwapa wapinzani nchi itaingia kwenye vita,”Sumaye.
“Baada ya Lowassa kuliona hilo, na kujiridhisha kuwa Watanzania wanamfahamu akienda kuwasaidia, woga huo hautakuwepo tena.
“Hata mimi nimeingia upinzani kwa ajili ya kushirikiana na Lowassa kuleta mabadiliko nchini ili wananchi waanze kufurahia maisha bora.”
Lakini kelele za shangwe ziliongezeka wakati alipoanza kujibu hoja mbalimbali zinazotolewa na makada wa CCM dhidi ya viongozi wa vyama vya upinzani.
Sumaye, ambaye alishika nafasi ya uwaziri mkuu kwa kipindi chote cha miaka 10 ya Serikali ya awamu ya Tatu, alisema Rais Jakaya Kikwete alimteua Lowassa kuwa Waziri Mkuu katika Serikali yake, akisema ni jambo la kushangaza kuona leo mkuu huyo wa anamwona hafai.
“Kuna mtu anamuweka Waziri Mkuu asiyefaa? Lakini ni Lowassa huyu huyu aliyemwingiza Kikwete Ikulu,” alisema na kusababisha mlipuko wa kelele za shangwe.
Kuhusu kumhusisha Lowassa na ufisadi na kula rushwa, Sumaye alisema kama mbunge huyo wa Monduli ni fisadi na mla rushwa, mbona hakukimbia nchi tangu alipotoka madarakani mwaka 2008.
“Angekuwa fisadi si wangeshamweka mahali? Lowassa amechukua ustaarabu wa kujiwajibisha baada ya tatizo kuingia katika Serikali. Hivi nani mkubwa wa Serikali? Tangu lini waziri mkuu akawa mkubwa wa serikali?” alihoji.
Sumaye alieleza kuwa baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere wakati fulani alitoa machozi kwenye kikao cha Halmashauri Kuu kuwa hajaona mtu mvumilivu kama Rashid Kawawa kwa sababu alikuwa akibeba mizigo ambayo ilipaswa kubebwa na Nyerere.
Lowassa alijiuzulu wadhifa huo mwaka 2008 baada ya Bunge kuunda kamati kuchunguza sakata la Serikali kuingia mkataba wa ufuaji umeme wa dharura na kampuni ya Richmond Development ya Marekani iliyobainika baadaye kuwa haikuwa na uwezo wa kufanya kazi hiyo.
MWANANCHI
Mgombea wa urais kupitia CCM, Dk John Magufuli amesema serikali yake itaimarisha masilahi ya wafanyakazi wote wakiwamo polisi, ili wasiwe wanalinda na kukosa fedha za kula nyumbani na hatimaye kusinzia vituoni na kunyang’anywa silaha.
Hii ni mara ya kwanza kwa Dk Magufuli kuzungumza kwa kina mpango wake wa kudhibiti wimbi la uvamizi wa vituo vya polisi, linalozidi kukua nchini na kuhatarisha maisha ya polisi na wananchi.
Akiwahutubia wakazi wa Makete, Dk Magufuli alisema anataka polisi wawe wanakwenda kazini wameshiba, hata jambazi akivamia wanamwua hapohapo bila kusubiri polisi jamii.
“Nazungumza kwa ukweli kwa sababu jeshi letu linatakiwa liheshimike, siyo mnakaa kwenye kituo watu wanachukua silaha wakati na ninyi mna silaha, “ alisema na kushangiliwa.
“Ninataka jeshi ambalo likimuona jambazi linamwasha kwa sababu yeye alikuja kuwawasha. Nataka iwe jiwe kwa jiwe, moto kwa moto, mguu kwa mguu, kichwa kwa kichwa, sikio kwa sikio, hayo ndiyo tunayoyataka.”
Dk Magufuli alisema maneno hayo huenda yakaonekana makali kwa baadhi ya watu lakini “hilo ndilo jibu”, na kwamba suala hilo linatakiwa kufanywa kwa kuzingatia sheria na utu wa binadamu.
Kauli hiyo aliirudia tena Njombe Mjini akisisitiza wakati wake “jambazi akija mchape risasi,” ili nchi iwe na amani na kuwafanya wananchi wafanye biashara zao kwa usalama kama nchi nyingine zilizoendelea.
Dk Magufuli aliahidi kujenga barabara ya lami kuanzia Njombe kupitia Makete hadi Mbeya, na kueleza kuwa usanifu na upembuzi yakinifu vimeshafanyika na kilichobaki ni kuanza ujenzi akiingia madarakani.
Pia, aliahidi kuboresha maisha ya wasanii nchini, akiahidi kuwaanzishia mfuko maalumu hivyo kuwataka wasihofu kuwa anawatumia tu kwa sasa wakati wa kampeni, bali atawajali hata baada ya kushinda.
Mgombea huyo aliyeingia mkoa wa tano wa kampeni zake alizungumzia ilani ya CCM, hasa suala la elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne, mikopo ya Sh50 milioni kwa kina mama na vijana kila kata, kuboresha huduma za umeme, afya, maji, pembejeo na kuimarisha masoko kwa wakulima.
Waziri huyo wa Ujenzi, jana alikutana na Naibu wake, Gerson Lwenge katika mkutano uliofanyika Makoga, Njombe Magharibi na kila mmoja kumnadi mwenzake.
Lwenge alisema Dk Magufuli kuwa amefanya naye kazi na kwamba ni mfanyakazi na “mkali kwelikweli anayetenda haki.”
Akizungumzia afya yake, aliwataka Watanzania kutohofia akisema yupo imara. Aliwaambia wakazi wa Makoga wilayani Wanging’ombe kuwa yuko timamu na atapambana hadi mwisho.
Alieleza kuwa kuna uzushi umezuka kwenye mitandao ya kijamii kuwa anaumwa na amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU), jambo ambalo siyo kweli.
MWANANCHI
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amesema baadhi ya kauli zinazotolewa na Umoja wa Vyama vya Upinzani (Ukawa), zinaashiria uvunjifu wa amani pindi matokeo ya kura yatakapoanishwa baada ya zoezi la upigaji kura Oktoba 25 mwaka huu.
Rais Kikwete alisema baadhi ya kauli hizo zimekuwa zikionyesha wazi viashiria vya uvunjifu wa amani na upotoshaji kwa kundi kubwa la vijana ambao wanapiga kura kwa mara ya kwanza.
Akizungumza wakati akizindua Kampeni ya Mama Ongea na Mwanao jijini Dar es Salaam Rais Kikwete alisema;
“Wamediriki kusema wazi bila kificho kwamba patakuwa hapatoshi, hizi ni kauli zinazoashiria uvunjifu wa amani. Tunachokisema CCM ushindi kwetu ni lazima na tutashinda kwa kishindo na kwenda nginja nginja mpaka Ikulu.”
Kikwete alisema CCM imejipanga kuhakikisha inapata ushindi katika Uchaguzi Mkuu ujao na kuongeza kuwa ili kufanikisha hilo wamepanga kikosi kazi ambacho kitatembea nyumba kwa nyumba, chumba kwa chumba, mtu kwa mtu ikiwa kwa sasa tayari wameshaanza kufanya kampeni zao kupitia mtandao ya simu za mkononi.
Katika hafla hiyo ya kuzindua kampeni hiyo inayoratibiwa na msanii wa filamu na Miss Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu, Rais  Kikwete aliwataka wanawake kaungalia mazuri yote yaliyofanywa na Serikali ya CCM katika kumuinua mwanamke.
JAMBOLEO
Chama cha ACT – Wazalendo leo kinazindua kampeni zake za uchaguzi kwa kuwatambulisha wagombea wote wa ubunge waliosimamishwa kwenye majimbo ya Tanzania –Bara na Zanzibar.
Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika katika Uwanja vya Zakhem Mbagala, wilayani Temeke kuanzia saa nne asubuhi.
Hivi karibuni, Katibu wa Mipango na Mikakati wa ACT – Wazalendo, Habibu Mchange aliwaambia waandishi wa habari kwamba hafla hiyo itahudhuriwa na viongozi wote wa kitaifa wa chama hicho wakiwamo Kiongozi wa Chama, Zitto Kabwe na Mwenyekiti wake, Anna Mghwira ambaye pia ni mgombea urais.
“Baada ya mwenyekiti wetu, Mama Mghwira kuchukua fomu ya kugombea urais, Watanzania wamekuwa na shauku ya kutaka kujua mustakabali wetu kuelekea Uchaguzi Mkuu,” alisema na kuongeza: “Hivyo basi tunawakaribisha wananchi wote siku hiyo waje kushuhudia kampeni za kisayansi. Ndiyo maana tumeamua kuwaita wagombea ubunge wote kuhudhuria na kuwatambulisha rasmi kwa Watanzania.”
Alisema ACT – Wazalendo imejipanga kuchukua dola na kuleta siasa safi, tofauti na vyama vingine akisisitiza kuwa kina nia ya dhati ya kuwaletea maendeleo ya Watanzania. Hivyo kuwataka wananchi kuhudhuria.
Alisema katika siku ya uzinduzi, kwa mara ya kwanza wabunge waliohama kutoka vyama vya CCM, CUF na Chadema watazungumza, pia wataendelea kuinadi ilani ya uchaguzi wa chama hicho. Alisisitiza kuinadi kaulimbiu ya chama hicho ya utu, uadilifu na uzalendo.
Katibu wa Fedha na Rasilimali ya chama hicho, Peter Mwambuja alisema pia kimejipanga kufanya siasa za malengo na masuala kwa maendeleo ya Watanzania siyo kupiga propaganda.
HABARILEO
Serikali ijayo, kama itaendelea kuongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) itajenga viwanda viwili kwa ajili ya kusindika mafuta ya alizeti na pamba katika mkoa wa Singida.
Mbali na kiwanda hicho, serikali ijayo ya CCM pia itajenga hospitali mkoani humo yenye ukubwa kama Hospitali ya Taifa ya Muhimbili itakayokuwa na uwezo wa kutoa huduma kwa wananchi wa Kanda ya Kati na mikoa ya jirani.
Ahadi hiyo ilitolewa jana na mgombea mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan wakati akizungumza na wananchi wa Iramba Magharibi waliojitokeza katika kijiji cha Kyengege. Samia alisema kila kiwanda kitaajiri zaidi ya vijana 600 hivyo kutoa fursa ya ajira kwa vijana.
Iramba Magharibi ni ngome ya mgombea kiti cha ubunge kwa tiketi ya CCM, Mwigulu Nchemba. Samia alisema hatua za awali za mradi huo wa ujenzi wa hospitali zimekwishaanza katika mkoa huo.
Akiwahamasisha wananchi kujitokeza kwa idadi kubwa kuipigia CCM kura, Samia alisema hiyo ndio itakuwa njia pekee ya kumpa fursa ya kutekeleza ilani ya CCM mkoani humo.
Akimzungumzia mgombea ubunge wa CCM katika jimbo hilo la Iramba Magharibi, Samia aliomba wapigakura walioandikishwa kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi na kupiga kura kwenye vituo husika.
“Nina uhakika wote waliojiandikisha kupiga kuwa mtaipigia kura CCM na yeyote atakayepiga kura upande mwingine, ngoja niwaambie mtakuwa mmepoteza kura zenu,” alisisitiza.
Aliongeza: “Hakikisheni mnakamilisha majukumu yenu ya kila siku mapema na muache siku ya kupiga kura kwa ajili ya kufanya kazi hiyo moja. “ Mapema mgombea huyo wa Urais kwa tiketi ya CCM alifanya mkutano wa kampeni Singida Vijijini, kata ya Msange ambayo mgombea ubunge katika jimbo hilo ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.
Akiwa Singida vijijini, Samia aliahidi kushughulikia matatizo ya maji na kuwezesha upatikanaji dawa mahospitalini, kwenye vituo vya afya na zahanati pamoja na kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa. Alisema Mfuko wa Taifa wa Maji utakaoanzishwa utaongeza nguvu katika juhudi za kupeleka maji vijijini na kukabiliana na matatizo ya maji.
Alisema serikali yake itajenga mabweni kwa ajili ya shule za sekondari, hasa kwa ajili ya wasichana ili kuwalinda dhidi ya wanaume wanaonyemelea mabinti wadogo na kuwasababishia mimba za utotoni.
Kwa upande wake, mgombea ubunge wa CCM katika Jimbo la Singida Vijijini, Nyalandu alisema jimbo lake limekuwa na maendeleo makubwa chini ya chama tawala. Alisema visima vya maji vimeongezeka kutoka 14 hadi 100 chini ya miradi ya maji inayotekelezwa na CCM, zahanati pia zimeongezeka hadi kufikia 40 kutoka 14.
Katika elimu, Nyalandu alisema kulikuwa na shule mbili tu za sekondari wakati anaingia madarakani lakini sasa kuna shule za sekondari 28. Nyalandu alisema jimbo jirani lililo mikononi mwa mpinzani lina maendeleo kidogo na kuongeza kuwa baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu mkoa wote wa Singida utakuwa mikononi mwa CCM.
HABARILEO
MgombeaUrais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli, amekanusha madai ya kuugua na kulazwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU), Katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya.
Dk Magufuli alisema hayo jana wakati akishukuru uongozi wa CCM wa mkoa huo, kwa mapokezi mazuri tangu alipoingia katika mkoa huo Alhamisi wiki hii akitokea Rukwa.
Madai ya kuugua na kulazwa kwa Dk Magufuli, yalianzia juzi katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya, alipokwenda kumjulia hali Meya wa Mbeya, Athanas Kapunga, aliyepata ajali Alhamisi wiki hii alipojiunga na msafara wake kwenda Makambako.
Meya huyo alipokuwa akitoka katika kijiji cha Nzoka kwenda Makambako baada ya kumpokea Dk Magufuli, akiwa nyuma ya msafara wa mgombea huyo, gari alilopanda liliacha njia na kupinduka ambapo mtu mmoja aliyekuwa amepewa lifti, alikufa na wengine akiwemo Meya huyo kujeruhiwa.
Kutokana na ajali hiyo, Dk Magufuli kabla ya kuanza ziara yake juzi mkoani Mbeya alikwenda kumjulia hali Meya huyo katika hospitali hiyo, ambako amelazwa Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU), ndipo kukasambaa uongo huo kwamba amelazwa.
Mbali na kukanusha uvumi huo, Dk Magufuli aliushukuru uongozi wa CCM Mkoa wa Mbeya na wananchi kwa ujumla kwa makaribisho mazuri.
Katika mkoa huo amekuwa akipokewa na maelfu ya wananchi katika mikutano mikubwa na mamia katika mikutano midogo, ambako amekuwa akisimamishwa mara kwa mara na wananchi njiani, ambapo Dk Magufuli alisema mapokezi hayo yameonesha kuwa Watanzania wengi wanataka mabadiliko bora na si bora mabadiliko.
Mbali na shukrani hizo, pia aliupa pole uongozi huo wa CCM Mbeya na wananchi kwa msiba wa kada mmoja wa chama hicho, aliyekufa katika ajali hiyo iliyomjeruhi Meya.
HABARILEO
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza sakata la zabuni ya mabilioni ya pesa iliyopewa kampuni ya kufua umeme ya Richmond, Dk Harrison Mwakyembe, ametoa siri za kilichofanyika wakati wa sakata hilo la kifisadi.
Akizungumza mbele ya maelfu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano wa kampeni za mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli katika Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe jana, Dk Mwakyembe alielezea kushangazwa na kauli ya mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, kuwa alipokea amri kutoka juu kuruhusu ufisadi wa Richmond.
Lowassa ambaye anaungwa mkono na vyama vya CUF, NLD na NCCR-Mageuzi katika Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ili awanie urais, alipozungumzia kisa cha kujiuzulu uwaziri mkuu, baada ya kashfa hiyo kumgusa moja kwa moja, alidai alitaka kusitisha mkataba na kampuni ya Richmond, lakini akasitishwa kutokana na amri kutoka juu.
Kwa mujibu wa madai ya Lowassa, aliitisha kikao cha wataalamu wa serikali na kueleza nia yake ya kuvunja mkataba na kampuni hiyo, lakini katibu mmoja akatoka nje kuzungumza na simu na kurejea kikaoni na ujumbe kwamba mkuu ameruhusu iendelee.
Akielezea kushangazwa kwake na kauli hiyo jana, Dk Mwakyembe alisema kama Katibu Mkuu kamletea amri Waziri Mkuu na akaikubali, basi hicho cheo cha Waziri Mkuu, kilikuwa kikimpwaya.
Siri zaidi Alisema wakati akiongoza Kamati Teule ya Bunge kuchunguza ufisadi huo, alimuomba Rais Jakaya Kikwete, nyaraka za Baraza la Mawaziri, ili afuatilie mwenendo wa suala hilo.
Kwa mujibu wa Dk Mwakyembe, katika nyaraka hizo, alibaini Rais alikataa katakata, kukiukwa kwa Sheria ya Manunuzi wakati wa mchakato wa kutoa zabuni ya uzalishaji umeme wa dharura, kwa wazabuni walioomba kazi hiyo.
Pamoja na Rais kukataa kukiukwa kwa sheria hiyo, Dk Mwakyembe alisema kampuni hiyo iliyokuwa ya 18 kwa sifa, ilitolewa chini na kupewa nafasi ya kwanza na kupewa zabuni hiyo ya mabilioni ya fedha.
Dk Mwakyembe alisema analizungumzia hilo ili Watanzania waelewe na kumpa kura zote mgombea urais wa CCM, Dk Magufuli kwa kuwa ufisadi huo umelinyonya Taifa mpaka leo.
Juzi mkoani Mbeya, Dk Mwakyembe alikumbusha kuwa walikwenda mpaka Marekani kuchunguza uwepo wa kampuni hiyo iliyodaiwa kutoka katika nchi hiyo, na kukuta ni kampuni ya kuchapisha kadi za harusi.
Kwa mujibu wa Dk Mwakyembe, baada ya kubaini ubadhirifu huo, Lowassa alishinikizwa kujiuzulu, lakini hatua ya kiongozi huyo kutaka kwenda Ikulu, wazalendo hawawezi kuikubali.
Kuhusu madai ya Ukawa kwamba kwa nini kama kuna ushahidi hakupelekwa mahakamani, Mhadhiri huyo wa Sheria alisema kosa la jinai, halina ukomo na wakati wowote linaweza kufunguliwa mashitaka, huku akiapa kuwa anaweza kumfungulia mashitaka hata kesho.
Dk Magufuli Akizungumza katika mkutano huo, Dk Magufuli alishukuru kuendelea kupata mapokezi ya wananchi wa vyama vyote, wakiwemo wa Chadema na vyama vingine vinavyounda Ukawa vya NCCR-Mageuzi, CUF na NLD.
Alisema anataka kuongoza Tanzania yenye umoja na amani, ndio maana anaomba kura kutoka vyama vyote, kwa kuwa sasa ushindani wa vyama hivyo umeanza kuelekea katika uadui jambo ambalo si sahihi.
NIPASHE
Vioja katika mikutano ya kampeni za uchaguzi mkuu vimezidi kujitokeza ambapo jana mgombea ubunge katika Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba, amejikuta akimwaga sera kwa kutumia lugha ya Kinyiramba badala ya Kiswahili kama Sheria za uchaguzi zinavyosema.
Nchemba alitumia lugha ya Kinyiramba kwa madai ya kuwa anaweka msisitizo kwa wapiga kura ambao walikusanyika katika kijiji cha Kengege katika jimbo la Iramba Magharibi mkoani Singida.
Akizungumza na wapiga wananchi hao, Nchemba alisema, atakayeacha kujitokeza kupiga kura wenzake watamsaka ili kujua kwa nini hakujitokeza siku ya kupiga kura.
Alisema mwaka huu idadi kubwa ya wapiga kura kuwa wamejitokeza kujiandikisha na kwamba atashangaa kama siku hiyo watu watalala majumbani mwao badala ya kwenda kupiga kura.
Mwigulu alisisitiza kwamba kila kitu amemalizana na wapiga kura wake na kwamba wanachosubiri ni kwenda kuichagua CCM siku ikifika.
Hata hivyo, alisema bado kuna tatizo kubwa la maji jimboni kwake jambo ambalo awamu ya tano ya serikali kama itakuwa ya CCM italimaliza.
Kwa upande wake, mgombea ubunge katika Jimbo la Singida Kaskazini, Lazaro Nyarandu, alitumia helikopta (Chopa) yenye namba za usajili, 5H-FCG, ambayo iliwavuta wananchi wengi kila ilipotua kwa kuikimbilia.
Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Msange jimbo la Singida Kaskazini,  Nyarandu alisema katika kipindi cha miaka mitano iliyopita mambo mbalimbali yalifanyika ikiwamo kuboresha huduma za maji, afya na shule.
Alitoa mfano katika kipindi chake cha miaka mitano ameweza kuongeza shule kutoka mbili hadi 28 pamoja na kusambaza huduma ya maji na vituo vya afya.
NIPASHE
Shirika la Umeme nchini (Tanesco), limetoa sababu ya kukatika kwa umeme katika baadhi ya maeneo jijini Dar es Salaam kuwa imetokana na uunganishaji wa mitambo katika gridi ya taifa.
Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Msemaji wa Tanesco, Adrian Severin, alisema Shirika hilo lilitoa taarifa kwa umma mapema kuhusu kukatika kwa umeme. Alisema katika eneo la Kinyerezi Wilaya ya Ilala, mkandarasi alikuwa akitengeneza mtambo wa umeme ambao utaunganishwa kwenye gridi ya taifa.
Alisema kukatika kwa umeme hakuhusiani na mkutano wa uzinduzi wa kampeni za mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa ambaye pia anaungwa na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
“Shirika letu halina uhusiano na siasa na wala halina nia ya kuhujumu Ukawa,” alisema.
Alisema mkandarasi alipewa muda wa kukamilisha kazi hiyo ifikapo Septemba, mwaka huu kinyume na muda huo, Shirika litaingia hasara.
NIPASHE
Mgombea ubunge wa Jimbo la Iringa Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Peter Msigwa, amesema hatavumilia propaganda zinazosambazwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ya kumchafua yeye na mgombea urais kupitia chama hicho, Edward Lowassa.
Msigwa alisema kuwa kuna watu wanaozusha kwenye mitandao ya kijamii kuwa amepewa pesa za kununua watu ili waweze kufika kwenye mkutano wa Chadema utakaofanyika leo mjini hapa.
Nasikitika kwa yaliyotolewa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kuwa mimi nimepewa milioni 200 kwa ajili ya kufanya maandalizi ya kununua, kusomba, kuwapatia madereva bodaboda ili waweze kufika kwenye mkutano wa hadhara wa Edward Lowassa utakaofanyika siku ya Jumapili Agosti 30, alisema.
Ni dhahiri kuwa maneno hayo yaliandikwa pengine na watu wanaotumiwa na wapinzani wangu kufifisha hali na moyo wa kujitolea kwa viongozi wa chama, wafuasi na wananchi na wapiga kura wetu wa jimbo la Iringa mjini, alisema Msigwa.
Aidha, alisema Chadema hakijawahi wala hakina mpango wa kusomba wananchi au kutoa fedha ili wahudhurie mikutano yao bali chama hicho  kimekuwa kikichangiwa fedha na wananchi na wamekua wakijitolea bila kulipwa hata senti tano.
Alisema kuwa chama hicho kimejipanga kufanya kampeni za kistaarabu zisizo na matusi na zinalenga na kujikita kwenye kuendeleza na kuwaambia wananchi ni kitu gani kinatakiwa kufanyika ili waweze kuondokana na umasikini na ndio imekuwa hoja yake kwa wananchi.
Alisema kuwa kwa sasa Chadema kimeshashinda na mbinu pekee waliyobaki nayo CCM ni kutaka kufanya kampeni chafu za kukichafua chama hicho na kilitahadharisha jeshi la polisi kuchukua hatua pindi watakapoona vurugu.
Alisema kuwa jimbo la Iringa Mjini litazindua kampeni zao rasmi Septemba 12 ili kueleza wananchi sera na dira ya jimbo la Iringa na taifa kwa ujumla.
Alisema kuwa jimbo la Iringa mjini limepewa fursa kubwa ya kutembelea na mgombea urais atawahutubia wananchi wa mkoa huo.
Alisema Lowassa ataanza kuhutubia wananchi wa Ilula, Mafinga, Pawaga, Kalenga na baadaye  Jimbo la Iringa Mjini.
NIPASHE
Rais wa Mahakama ya Afrika ya haki za binadamu, Jaji Agustino Ramadhani, amesema hajawahi kupatwa na wazimu wa kufikiria kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Aliyasema kuhusu taarifa zilizoenea kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, kwamba yeye na Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, wapo katika mipango ya kuhamia kambi ya upinzani.
Jaji Ramadhani ambaye alikuwa mmoja kati ya makada 42 waliojitokeza kuchukua fomu za kuwania nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya CCM, jina lake lilikatwa na Kamati ya Maadili kabla ya kufikishwa mbele ya Kamati Kuu (CC) ya chama hicho.
Jaji Ramadhani ambaye alikuwa kimya tangu mchakato huo umalizike, alisema taarifa hizo na yeye ameziona kwenye mitandao.
Hizo taarifa hata mimi niliziona kwenye mitandao ya kijamii, kwamba mimi na Mh. Bilal tutazungumza na vyombo vya habari kutangaza kuhama chama na kwamba tutasindikizwa na mzee Warioba (Jaji Joseph Warioba), wanaoeneza  hayo ni watu wasiyo na adabu, sijawahi kupatwa na wazimu wa kufikiria kuhama CCM, alisema.
Alisema yanayoenezwa kwenye mitandao dhidi yake, kuhusiana na kuhama chama hayana ukweli wowote.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

Saturday, August 29, 2015

UKANJANJA WAWAPELEKA JELA WAANDISHI WA HABARI MISRI

Hukumu ya waandishi hawa baada ya kutangaza habari za uongo…

aljazera
Mahakama ya Misri imewahukumu waandishi watatu wa kituo cha runinga cha Al jazeera kwenda jela miaka mitatu.
Hukumu hiyo ilitolewa baada ya waandishi hao Mohamed Fahmy, Peter Greste na Baher Mohamed kupatikana na hatia ya kutangaza habari za uongo na kulisaidia kundi la Muslim Brotherhood ambalo kwa sasa linatambuliwa kama kundi la kigaidi.
Baher Mohamed pia alihukumiwa kifungo kingine cha miezi sita.
Hata hivyo mmoja wa waandishi hao Peter Greste, yuko nje ya nchi hiyo baada ya kutimuliwa kutoka nchini kwake tangu mwezi Ferbruari.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

CHALSEA YADUNDWA

Kilichoikuta Chelsea vs Crystal Palace hiki hapa

Ligi kuu ya Uingereza maarufu kama Barclays Premier League imeendelea Jana  katika viwanja mbalimbali nchini humo.

Mchezo huo uliopigwa  katika dimba la Stamford Bridge umemalizika kwa Crystal Palace kuharibu rekodi ya Mourinho kutopoteza mechi katika dimba la nyumbani.
Mechi hiyo imemalizika kwa matokeo ya ushindi wa 2-1 kwa Palace inayofundishwa na kocha wa zamani wa Newcastle – Alan Perdew.
Sako alianza kuifungia Palace goli katika dakika ya 65, kabla ya Radamel Falcao kusawazisha katika dakika ya 79.
Dakika ya 81, James Ward aliifungia Palace goli la ushindi na kuzidi kuiharibu rekodi ya Mourinho katika uwanja wa nyumbani ambapo jan alikuwa anatimiza mechi ya 100 tangu alipoanza kuifundisha tena timu hiyo.

LIVAPOOL YALOWA KWA VIBONDE

Liverpool vs West Ham nimekuwekea hapa

Baada ya kuanza ligi vizuri kwa kushinda mechi mbili za mwanzo na kutoa sare moja, klabu ya Liverpool . Jana  imeanza kuonja joto ya jiwe katika Barclays premier league.
 
Wakicheza kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Anfield – Liverpool wamepoteza mchezo wao wa kwanza msimu huu baada ya kukubali kipigo cha 3-0 kutoka West Ham.
 
Magoli ya West Ham ambao walifungua ligi kwa kuifunga Arsenal – yalifungwa na Lanzini katika dakika ya 3, Noble akaongeza la pili dakika ya 29, Sakho akafunga biashara kwa kushindilia msumari wa mwisho dakika ya 90.
Vikosi vilipangwa hivi: Liverpool: Mignolet, Clyne, Skrtel, Lovren, Gomez (Ibe 78), Can (Moreno 45), Lucas, Milner, Firmino (Ings 61), Benteke, Coutinho.
Subs not used: Sakho, Origi, Bogdan, Rossiter.
Booked: Lucas, Ings, Clyne.
Sent off: Coutinho 52.
West Ham: Randolph, Tomkins, Reid, Ogbonna, Cresswell, Kouyate, Obiang, Noble (Oxford 81), Lanzini, Sakho (Cullen 90), Payet (Jarvis 88).

YASIKUPITE MATOKEO YA LIKU KUU ENGLAND

Nimekusogezea matokeo ya Arsenal vs Newcastle na Man City vs Watford

Ikiwa imeshinda mechi tatu mfululizo katika msimu mpya wa ligi kuu ya Uingereza, klabu ya Manchester City leo imeendelea kuilinda rekodi yake ya kushinda kwa 100% katika mfululizo wa mechi BPL.
 
Wakiwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Etihad, City wameibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya timu iliyopanda daraja la Watford.
 
Raheem Sterling aliyenunuliwa kwa ada ya £49m kutoka Liverpool jana alifunga goli la kwanza katika msimu mpya Barclays Premier League na Fernadinho akifunga goli lingine.
Arsenal vs Newcastle  
Goli pekee lilofungwa na Alexander Chamberlain lilitosha kuipa Arsenal ushindi dhidi ya timu ngumu ya Newcastle katika mchezo uliofanyika mapema leo mchana katika uwanja wa St James Park.

VIWANJANI LEO, AUG 29

Ninayo ratiba ya Ligi Kuu Uingereza na Hispania ya August 29 na 30 mtu wangu…..

Ligi Kuu mbili zinazopendwa zaidi ukanda wa Afrika Mashariki Ligi Kuu Hispania na Uingereza August 29 na 30 kuna michezo kadhaa inapigwa katika viwanja tofauti Hispania na Uingereza . Nakusogeza na ratiba za mechi zote za Laliga na EPL za weekend hii mtu wangu wa nguvu.
Fixtures
Hii ni ya Ligi Kuu Uingereza mtu wa
1
Huu ni muda wa mechi za Ligi Kuu Uingereza kwa saa za Afrika Mashariki
  1. Newcastle Vs Arsenal                14:45
  2. Aston Villa Vs Sunderland       17:00
  3. Bournemouth Vs Leicester      17:00
  4. Chelsea Vs Crystal Palace        17:00
  5. Liverpool Vs West Ham           17:00
  6. Man City Vs Watford               17:00
  7. Stoke Vs West Brom                17:00
  8. Tottenham Vs Everton           19:30
Jumamosi August 30
  1. Southampton Vs Norwich    15:30
  2. Swansea Vs Man Utd            18:00
Hii ni ratiba ya Ligi Kuu Hispania Mtu wangu
2

Huu ni muda wa mechi hizo kwa saa za Afrika Mashariki mtu wangu
  1. Real Sociedad Vs Sporting de Gijón    19:00
  2. Barcelona Vs Málaga                              21:30
  3. Celta de Vigo Vs Rayo Vallecano         23:00
  4. Real Madrid Vs Real Betis                    23:30
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog