Wednesday, December 31, 2014

MAKOBAZI BEI POA

 Wakazi wa mji wa Chake Chake Wilaya Kusini Pemba wakinunua viatu aina ya Makobazi kwa muuzaji Fakihi Mansour eneo la njia ya kwenda kituo cha magari yaendayo Wilayani na katikati ya mji. Kobazi pea mmoja ilikuwa ikiuzwa kati ya shilingi  20,000, hadi 28,000.




KILIO CHA MAJI , WETE PEMBA

Kumekucha blog

Pemba, WAKAZI wa mji wa Wete Wilaya ya Kaskazini Pemba, wamesema kero ya upatikanaji wa maji safi majumbani haitoisha hadi Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) kukarabati miundombinu yake ambayo imezidi kuwa chakavu.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi nyakati tofauti, wakazi hao wamesema kero ya maji mjini humo imekuwa kero na kushindwa kuwafikia majumbani baada ya njia nyingi za  mabomba yanayopitisha maji  kupasuka.

Wamesema hali hiyo imekuwa ikiwalazimu kwenda mabondeni ambako pia upatikanaji wake umekuwa wa shida baada mabonde mengi kukauka maji kutokana na kiangazi.

“Sisi huku kizimbani maji hayafiki kabisa na tumeshazoea tukiamka tunakimbilia mabondeni---mabomba mengi yamepasuka na maji yanaishia njiani na hili tumelisema sana” alisema Amran Hamis

“Tumetoa taarifa kwa mamlaka yetu ya  maji kama inavyojulikana kwa jina la  zawa----lakini chakushangaza wao pia wanalitambua na kila siku wanatuambia watabadilisha mabomba” alisema

Akizungumzia kwa undani kero hiyo mkazi wa Chasasa, Said Bakar,  alisema wamekuwa katika wakati mgumu kuweza kukabiliana na shida hiyo hasa vipindi vya watoto kwenda shule baada kusongomana katika visima bondeni.

Alisema vipindi vya shule maeneo ya mabondeni watoto wamekuwa wengi na kila mmoja kutaka kuwahi shule na hivyo kusubiria hadi saa 2 jambo ambalo nao wamekuwa wakichelewa kwenda katika majukumu yao kwa wakati.

Aliishauri Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) kuifanyia ukarabati miundombinu yake ili kuweza kupata maji majumbani jambo ambalo maji mengi yamekuwa yakipotea baada ya mabomba kuwa chakavu.

“Nashauri tu mamlaka yetu ikafanya ukarabati taratibu angalau tuweze kupata maji kidogo kidogo vyenginevyo shida hii itatukondesha na kutuchosha” alisema Bakar

Alisema kwa muda mrefu wamekuwa walilalamika na kushindwa kilio chao kupatiwa ufumbuzi na hivyo kusema ni muda muafaka wa sasa kuweza kupatiwa ufumbuzi kwani limekuwa la muda mrefu.

                                         Mwisho

KISIWA CHA HARISHI (23)

HADITHI
 
KISIWA CHA HARISHI (23)
 
ILIPOISHIA TOLEO LILILOPITA
 
Kile kitendo cha kutoniona mimi inawezekana kilimpa hisia kuwa na mimi nilikuwa nimeuawa kama Shazume. Tatizo ni kuwa mwili wangu hakuuona. Bila shaka alitoka nje kuutafuta mwili wangu.
 
Alisimama mbele ya ile nyumba akaangalia kila upande kisha akarudi tena mle ndani. Mimi nikashuka kwenye ule mti.
 
Yasmin alipotoka tena akanikuta nimesimama mbele ya mlango. Akashituka na kuniuliza. “Ulikuwa wapi?”
 
“Nilikuwa nimepanda juu ya huu mti” nikamjibu.
 
Akaja kunikumbatia kifuani kwangu. Kumbe alikuwa analia. Nilipoona analia na mimi nikaanza kulia. Kama Yasmin alikuwa anaona uchungu jinsi tulivyokuwa tunauliwa na Harishi, mimi niliona uchungu nilipowaza nitakavyouliwa na Harishi hapo kesho.
 
“Buriani Yasmin, ndio tunaagana. Kesho hatutakuwa pamoja tena. Shazume ametutangulia leo” nikamwambia Yasmin.
 
Yasmin akajifuta machozi yake na kunitazama.
 
“Wewe hutaniacha, kama ni kufa tutakufa sote. Mwili wangu utalala juu ya mwili wako” Yasmin akaniambia kwa sauti nzito lakini ya kijasiri.
 
Akaongeza. “Ili uamini kuwa wewe utakufa na mimi turudi kule kule kwenye lile jumba,hatuna sababu yoyote ya kujificha. Akija Harishi nitamwambia atuue sote, Anitangulize mimi kisha wewe”
 
SASA ENDELEA
 
“Twende!” nikamwambia Yasmin bila kusita.
 
Yasmin akanishika mkono tukatembea kuelekea katikalile jumba. Hatukuzungumza kitu tena mpaka tulipofika katika jumba hilo Yasmin aliniuliza.
 
“Utakunywa uji?”
 
“Sitakunywa” nikamjibu kwa mkato
 
“Kwanini?”
 
“Roho yangu imefadhaika sana”
 
“Hata roho yangu imefadhaika lakini kama wanipenda tunywe kidogo”
 
Ilikumridhisha Yasmin nilimkubalia. Yasmin aliniacha ukumbini akaenda jikoni. Baaada ya muda kidogo alikuja na vikombe viwili vilivyojaa uji wa ngano uliotiwa asali.
 
Alinipa kikombe kimoja kisha aliketi nami.
 
“Yasmin kweli tumeshindwa kuondoka kwenye kisiwa hiki cha mauti” nikamuuliza Yasmin
 
“Tutaondokaje wakati tumezungukwa na bahari na hatuna chombo!”
 
“Nashangaa kwamba hakuna wavuvi wanaokuja katika kisiwa hiki!”
 
“Hiki kisiwa kiko mbali na pia kinajulikana. Hakuna wavuvi wanaoweza kufika hapa”
 
“Chombo chetu kilipotuharibikia tulipokiona kisiwa hiki tulidhani tumeokoka kumbe tumekuja kuangamia”
 
“Hata kama msingekiona hiki kisiwa pia mngeangamia. Mngekula nini? Mngekufa kwa njaa”
 
“Mimi naona bora kufa kwa njaa kwa sababu njaa itakuwa imekulevya, hutajijua. Kuliko kusubiri….” sikumalizia sentensi yangu.
 
Niliona nilikuwa najikumbusha kifo kibaya cha kutobolewa utosi kwa ncha ya upanga na kufyonzwa damu na ubongo1.
 
Siku zote tulizokaa hapa kisiwani niliweza kujikaza na kuondoa hofu licha ya wenzangu kuendelea kuuawa lakini kwa siku ile ambayo nilibakimimi na Yasmin peke yetu, sikuweza kuzuia hofu yangu.
 
Mawazo ya kifo cha kutobolewa utosi kwa ncha ya upanga na kufyonzwa damu na ubongo yalikuwa yametawala akili yangu.
 
“Harishi ni kiumbe na sisi ni viumbe. Huwezi kujua Mungu amepanga nini” Yasmin akaniambia.
 
“Namuamini Mungu na simkatii tamaa”
 
“Hapo umezungumza kitu cha maana sana. Haifai kukata tama. Nimeshakwambia kama ni kufa leo tutakufa sote. Na mimi ndio nitakufa kwanza”
 
“Unataka tuendelee kukaa humu hadi usiku”
 
“Ndiyo. Unafikiri utakwenda wapi?”
 
“Sioni pa kwenda”
 
“Basi tukae tu humu”
 
“Harishi akija atukute pamoja?”
 
“Ndiyo”
 
“Aniue mbele yako!”
 
“Hapana. Ataniua mimi kwanza”
 
“Mimi sipendi nikusababishie kifo, niache nife mwenyewe”
 
“Na mimi sitapenda nikusababishie kifo”
 
“Wewe hutanisababishia kifo, ni Harishi”
 
“Sikiliza kaka yangu. Sisi tukae hapa hadi usiku.Litakalotokea lolote na litokee lakini kama ni kufa nitatangulia mimi”   
 
Nilimuangalia tu Yasmin, sikumjibu kitu tena. Nikaendelea kunywa uji huku nikiwaza kama ni kweli alikuwa amejitolea nafsi yake kwa ajili yangu.
 
Maneno yake yalionesha alichokuwa akisema kilikuwa na udhati.
 
Hata hivyo niliwaza kuwa msimamo wa Yasmin haukuwa na msaada wowote kwangu zaidi ya kuonesha upendo. Ulikuwa msimamo wa kukata tamaa na haukuwana maana.
 
Atangulie yeye kufa halafu nifuatie mimi? Maana yake ni kuwa sote tutafikwa na mauti. Jambo hilo kwangu lilikuwa tishio ingawa yeye aliona lilikuwa la kijasiri.
 
Jambo la maana lilikuwa kupata wazo la kutunusuru sote na sio tufe sote.
 
Tulibaki kimya tukinywa uji. Uji huo niliunywa kwa kujilazimisha ili kumridhisha Yasmin. Kama ningekuwa peke yangu ningebaki na njaa hadi mauti yatakaponikuta.
 
Nilipomaliza kikombe changu cha uji Yasmin aliniuliza.
 
“Nikutilie tena?”
 
“Umetosha’ nikamjibu.
 
Yeye pia alikuwa amemaliza uji wake akaniambia.
 
“Basi nenda ukaoge, umeshatia nguvu kidogo”
 
Pamoja na kukabiliwa na tishio hilo la kifo kusema kweli nilihitajika sana kuusafisha mwili wangu. Nilikuwa nimechafuka sana na nilikuwa sijaoga kwa siku tatu.
 
Niliona aibu kumwambia Yasmin kuwa sitaoga. Nikainuka.
 
Yasmin akanipeleka bafuni kisha akaondoka. Nilioga haraka haraka. Nilipomaliza niliondoka bafuni na kumbishia Yasmin mlango.
 
Yasmin alinifungulia mlango na kuniambia.
 
“Karibu”
 
Niliingia mle chumbani alimokuwa. Hamkuwa na kiti. Akaniambia.
 
Kaa kitandani”
 
Nikakaa.
 
“Unajisikia vizuri kidogo?” akaniuliza.
 
Nilijaribu kutabasamu bila kufanikiwa. Niliishia kubenua midomo tu, uso haukukunjuka.
 
ITAENDELEA KESHO, USIKOSE
 
 
 

MIILI YA WAHANGA WA NGEDE ILIYOZAMA BAHARINI YAZIDI KUOPOLEWA

HUZUNI NA VILIO WAKATI MIILI YA ABIRIA WALIOKUFA  NDEGE YA AIR ASIA IKIWASILI KWA AJILI YA UTAMBUZI





KUFUATIA KUPIGWA RISASI MTUHUMIWA WA MADAWA YA KULEVYA, WENGI WANASEMA

Alichokisema msimamizi wa Mashtaka Kisutu na shuhuda wa tukio la mtuhumiwa aliyepigwa risasi

Alichokisema msimamizi wa Mashtaka Kisutu na shuhuda wa tukio la mtuhumiwa aliyepigwa risasiIMG-20141231-WA0008Mitandao ya kijamii na vyombo mbalimbali vya Habari leo viliripoti kuhusu mtu mmoja raia wa Sierra Leone, Abdul Koroma ambaye alikuwa anashikiliwa na Jeshi la Magereza nchini kufariki dunia leo Dar baada ya kupigwa risasi na askari Magereza wakati akijaribu kutoroka.

Mtu huyo alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa mara ya kwanza mwaka 2013 kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya na kushitakiwa.
Ameuawa katika uzio wa Mahakama hiyo baada ya kumtoroka askari magereza aliyekuwa amemsindikiza kujisaidia ambapo alijaribu kuruka ukuta wa mahakama hiyo.
Shuhuda mmoja wa tukio hilo amesema; “alikimbilia kwenye ule ukuta pale, akapandisha mpaka pale juu… anataka arukie upande wa pili magereza washatokea, wakaona hawawezi kukimbia yuko mbali ndio wakampiga zile risasi kama tatu hivi ndio akafariki…
Akizungumzia tukio hilo Msimamizi wa Mashtaka Mahakama ya Kisutu Tumaini Kweka amesema; “Wakati wapo kwenye sero ndipo yeye akajaribu kutoroka kwa kujaribu kuruka ule ukuta wetu wa Mahakama ndipo wanausalama wetu ambao wako hapa wakaweza kundhibiti…

OBAMA AWAOMBA RADHWI MAHARUSI HAWA

bama awaomba radhi maharusi hawa, waliondolewa uwanjani ili aendelee na mchezo wa gofu.

Obama awaomba radhi maharusi hawa, waliondolewa uwanjani ili aendelee na mchezo wa gofu.

obama-aurora-callNi mara chache tumesikia viongozi wakubwa kwenye  nafasi kama Rais akiomba radhi hadharani hata kama ni kweli amekosea.
Moja ya video zilizopata umaarufu mkubwa ndani ya saa chache ni hii inayoonyesha bibi na bwana wakiwa kwenye suti na shela, kwenye pilika pilika za sherehe ya ndoa kisha ikapigwa simu kutoka kwa Rais Obama akiwaomba maharusi hao radhi kwa kuwahamisha sehemu ambayo ilikuwa sherehe ya wawili hao ifanyike.
Maafisa usalama wa Marekani walilazimika kuwahamisha maharusi hao katika eneo ambalo ilikuwa ifanyike sherehe yao kwa kuwa Rais Obama alikuwa akienda kucheza gofu katika kipindi cha mapumziko.
Maharusi hao ambao wote ni wanajeshi, Kapteni Hiemel na Kapteni Mallue walipokea simu kutoka kwa Obama akiwaomba radhi kwamba alichelewa kupatiwa taarifa kuhusu shughuli ya maharusi hao kufanyika katika viwanja hivyo.

MOVE ZINAZONGOZA KWA KUIBWA MWAKA 2014

Movie zilizoongozwa kwa ‘kuibiwa’ kwenye mtandao 2014.

Movie zilizoongozwa kwa ‘kuibiwa’ kwenye mtandao 2014.

the_wolf1
Mwaka 2014 utakuwa mwaka wa kusahaulika kwa Muandaaji filamu Martin Scorsese ambaye filamu yake ya The Wolf Of Wallstreet iliyogizwa na star wa filamu Leornado Di Caprio iliongoza kwa kuibiwa kwenye mtandao kinyume cha sheria .
Vyanzo mbalimbali vya habari nchini Marekani wiki hii vilichapisha orodha ya filamu ambazo zimeongoza kuibiwa kinyume cha sheria yaani ‘Illegal Downloads’ orodha ambayo filamu hii ya Wolf Of Wallstreet iliongoza .
Watumia kompyuta wapata milioni 30 walidownload movie hii kwa kipindi cha kuanzia Januari 1 mpaka desemba 23 huku Movie ya vikaragosi au Animation Film ya Frozen ikishika nafasi ya pili baada ya kuibiwa na watu wapatao milioni 29.9.
Movie iliyoshika nafasi ya tatu klatika orodha ya filamu zilizoshushwa kwa wingi kinyume cha sheria kupitia mtandao wa internet ilikuwa filamu ya RoboCop ambayo ilishushwa mara milioni 29.6 huku Filamu ya Gravity nayo ikiwa kwenye nafasi ya nne baada ya kushushwa mara milioni 29.4
Movie nyingine zilionekana kwenye orodha hii ni “Thor: The Dark World,” “Captain America: The Winter Soldier” na filamu ya  “X-Men: Days of Future Past ambapo zote zilishushwa na watu ambao wanapita idadi ya watu milioni 20 .
12-years-a-slave
Filamu iliyofanya vizuri mwaka huu mpaka kutwaa tuzo ya Oscar huku ikimtambulisha rasmi star toka Afrika Mashariki Lupita Nyong’o ya 12 years a slave ilishushwa kwenye mtandao na watu milioni 23.7  huku American Hustle na Captain Philips nazo zikiingia kwenye roodha hii baada ya watu milioni 23.1 kushusha .

Orodha Kamili .
  1. “The Wolf of Wall Street”: 30.035 millioni
  2. “Frozen”: 29.919 millioni
  3. “RoboCop” (ikiwemo original 1987 movie): 29.879 millioni
  4. “Gravity”: 29.357 millioni
  5. “The Hobbit: The Desolation of Smaug”: 27.627 millioni
  6. “Thor: The Dark World”: 25.749 millioni
  7. “Captain America: The Winter Soldier”: 25.628 millioni
  8. “The Legend of Hercules”: 25.137 milioni
  9. “X-Men: Days of Future Past”: 24.380 milioni
  10. “12 Years a Slave”: 23.653 milioni
  11. “The Hunger Games: Catching Fire”: 23.543 millioni
  12. “American Hustle”: 23.143 milioni
  13. “300: Rise of an Empire”: 23.096 milioni
  14. “Transformers: Age of Extinction”: 21.65 milioni
  15. “Godzilla”: 20.956 milioni
  16. “Noah”: 20.334 milioni
  17. “Divergent”: 20.312 milioni
  18. “Edge of Tomorrow”: 20.299 milioni
  19. “Captain Phillips”: 19.817 milioni
  20. “Lone Survivor”: 19.130 milioni

RINHANA AMTOA KAKA YAKE KATIKA MAUZO YA CD

Rihanna kumtoa kaka yake kwenye ‘Game’.

Rihanna kumtoa kaka yake kwenye ‘Game’.

Rihanna
Siku zote ua huota kwenye bustani ambayo ina maua mengi , msemo huo umeonekana kuwa kweli kwenye familia ya mwanamuziki Robyn Fenty mwenye asili ya visiwa vya Barbados ambaye wengi humfahamu kama Rihanna baada ya mwanadada huyo kuamua kumsaidia ndugu yake wa kiume kuingia rasmi kwneye tasnia ya muziki ambako mwanadada huyo amekuwa akifanya vizuri .
Rihanna ameamua kumsaidia mdogo wake wa kiume ambaye anafahamika kwa jina la Rorrey ‘kutoka’ kwenye Sanaa ya muziki ambako kijana huyo anafanya muziki wa mtindo wa kufoka yaani Hip-Hop.
Rihanna mwenye umri wa miaka 26 aliamua kurudi nyumbani kwao huko visiwani Barbados ambako pamoja na kuwa mapumzikoni amekuwa ‘bize’ kikazi akimsaidia ndugu yake Rorrey Fenty kujaribu kujijengea jina katika muziki kama ilivyokuwa kwake .
Rihanna akiwa na mdogo wake Rorrey ambaye anafanya naye kazi akiwa na lengo la kumtoa kwneye game .
Rihanna akiwa na mdogo wake Rorrey ambaye anafanya naye kazi akiwa na lengo la kumtoa kwneye game .
Rihanna amekuwa akimshauri ndugu yake huyo kuzingatia muziki na si mambo mengine ambayo hayawezi kumsaidia yakiwemo kuishi mtindo wa maisha wa kuendekeza anasa na starehe .
Chanzo kimoja cha habari hii kimearifu kuwa Rihanna anatambua kuwa kaka yake ana kipaji kama msanii lakini pia anapenda sana maisha ya starehe jambo ambalo linaweza kumfanya ashindwe kuzingatia kazi na kushindwa kufanikiwa .
Rihanna anafahamu kuwa anao uwezo wa kumsaidia ndugu yake kwani akifanya naye wimbo bila ubishi wimbo huo utafanya vizuri na kuwa kama jukwaa la kuanzia kwa ndugu yake mwenye umri wa miaka 23 na ndio maana amemaua kupoteza muda wake kuhakikisha anamsaidia ili kumfanya ‘atoke’ kisanaa kama ilivyokuwa kwake (Rihanna)
rihanna+andd+rorrey
Rorrey Fenty anafahamika kwa jina la kisanii la GALLEST na hadi sasa ameshaachia ‘mixtape’ ambayo inafahamika kama ‘Intolerable Cruelty’ ambayo aliiachia mwanzoni mwa mwaka 2014 na Rihanna ana matumaini kuwa atakuwa msaada mkubwa kwa ndugu yake .
Kwa upande wake Rihanna mwenyewe ambaye kwa sasa amekuwa kwenye mapumziko akiwa amesimamisha kazi zake zote za  Sanaa atarudi rasmi kwenye Game mapema mwaka 2015 na anatarajiwa kuachia wimbo utakaojulikana kama R8’ ambao ameufanya akishirikiana na msanii Ryan Tedder wa kundi la muziki wa rock la One Republic.

ACHOMWA KISU KICHWANI NA KUTEMBEA NACHO HADI HOSPITAL

Huyu amechomwa kisu kichwani, ametembea nacho zaidi ya saa mbili akielekea hospitali

Huyu amechomwa kisu kichwani, ametembea nacho zaidi ya saa mbili akielekea hospitali

KnifeMwanaume mmoja Brazil amewashangaza wengi baada, ameweza kutembea masaa mawili kuelekea hospitali akiwa na kisu kichwani alichochomwa na majambazi waliomvamia akiwa anatoka Club.
Kisu hicho kilizama kichwani kwa urefu wa 30cm kilimpata mwanaume huyo Juacelo Nunes pembeni ya jicho la kushoto na kutokea kwenye shavu wakati akipambana na majambazi hao.
brazilKisu kilipita katika baadhi ya mishipa yake ya damu ambayo ingeweza kumuua kutokana na kuvuja kwa damu nyingi,” alisema daktari Gilberto Albuquerque aliyemhudumia mgonjwa huyo kutoka hospitali ya Teresina alipofikia kupata matibabu.
Kisu hicho kilitolewa na kukabidhiwa Polisi ambao wanaendelea na uchunguzi kuwatafuta wahusika wa tukio hilo.
Daktari amesema mgonjwa huyo kwa sasa yuko chini ya uangalizi wa madaktari na hali yake inaendelea vizuri.
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,kumekucha blog

DULLY SEX ATOA SHUKURANI


Kama ulipitwa na 255 leo December 31, nimeirekodi na kukuwekea hapa. Unaweza kuisikiliza

Kama ulipitwa na 255 leo December 31, nimeirekodi na kukuwekea hapa. Unaweza kuisikiliza

headphones-keyboard-computer-960x540
Msanii Dully Sykes amewashukuru wasanii wenzake waliojitokeza kumsupport kwenye show yake iliyofanyika jana Escape 1 Dar ambapo alikuwa akisherehekea miaka yake 15 kwenye muziki.
Dully amewataja baadhi ya wasanii kama Bushoke, Makomandoo, Queen Dareen, Ali Kiba na Diamond ambaye japo  hakufika kutokana na kuwepo nje ya nchi akifanya show, lakini wasanii hao kwa pamoja wamemsaidia kufanikisha show hiyo.
kasikitishwa pia na baadhi ya wale ambao alitarajia watakuwepo na hawakutokea huku yeye akiwa ni mtu ambaye katoa mchango wake sana katika mafanikio yao.
Baada ya kuachiwa video ya mwana ya Ali Kiba watu walikuwa na maoni tofauti kwamba kile ambacho walikitarajia kwenye video hiyo kuwa tofauti na ilivyotokea, Kiba amesema kuwa hivyo ambavyo alitaka video hiyo itokee na utofauti wake ndio uzuri wake, isingewezekana kila kitu kilichozungumziwa kiwepo katika video ya wimbo huo.
Staa Nick Minaj amesema kuwa aliwahi kutoa ujauzito akiwa na miaka 16, hajutii kitendo hicho kwa kuwa hakuwa na uwezo kumlean mtoto wake huyo, japo wakati akifanya kitendo hicho alihisi kama anafariki.

KANYE WEST ANUNUA JUMBA LA KIFAHARI

Kanye West na Kim Kadarshian wamenunua nyumba mpya… Hii huenda ikamfanya Kanye akatumia muda mwingi kuwa nyumbani.

Kanye West na Kim Kadarshian wamenunua nyumba mpya… Hii huenda ikamfanya Kanye akatumia muda mwingi kuwa nyumbani.

happyRatiba za mastaa wengi walio katika uhusiano wa kimapenzi huwa zinawafanya wanakuwa busy na kushindwa kupata time ya kuspend pamoja, Kim Kardashian na Kanye West ni moja ya mastaa ambao wao pia ratiba yao huwa ngumu kupata muda wa kukaa pamoja.
Kim yuko busy na TV show na deal zake za mitindo lakini ratiba yake haimfanyi awe busy kama ilivyo kwa Kanye ambaye amekuwa akizunguka kwa ajili ya show na pia kurekodi nje ya Marekani.
Story ya mwisho kusikika kuhusu mastaa hao ni ile ambayo imetoka siku moja iliyopita, wamenunua nyumba ya jirani yao yenye thamani ya dola mil.3 maeneo ya Los Angeles ambapo mkakati walio nao ni kuikarabati kwa kuweka vitu kadhaa ikiwemo Studio ya kisasa.
masiveKwenye nyumba hiyo pia kutakuwa na uwanja wa basketball, sehemu ya kuangalia filamu, sehemu ya michezo, chumba cha massage na eneo la kufikia wageni, studio itakayokuwepo hapo huenda ikasaidia kumfanya Kanye apate muda mwingi kidogo wa kukaa nyumbani tofauti na ilivyo sasa.sivee
Nakuhakikishia kwamba nitakufikishia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia, kumekucha blog

KINARA WA KUINGIZA MADAWA YA KULEVYA ATWANGWA RISASI NA KUFA


 Kuhusu huyu aliyeuwawa kwa risasi Mahakamani Dar es salaam leo.

Kuhusu huyu aliyeuwawa kwa risasi Mahakamani Dar es salaam leo.

Kisutu 4Saa kadhaa zilizopita Polisi walimfyatulia risasi mtuhumiwa aliejaribu kutoroka baada ya kufikishwa kwenye Mahakama ya Kisutu Dar es salaam leo December 31 2014.
Muda mfupi baadae Polisi ikatoa taarifa kwamba mtuhumiwa wa dawa za kulevya aliyeuwawa ni Abdul Koroma raia wa Sierra Leone na aliuwawa kwa risasi wakati akitoroka Mahakamani.
Kisutu 5
kisutu 3
Kisutu 1
kisutu 2

BIBI HARUSI AVURUMISHIWA MAWE AKIWA HOLINI


Hekaheka ya leo December 31 iko hapa, inatoka Vingunguti ambapo Bibi harusi walipigwa mawe katika sherehe

Hekaheka ya leo December 31 iko hapa, inatoka Vingunguti ambapo Bibi harusi walipigwa mawe katika sherehe

Stone II
Hekaheka ya leo December 31 ni ya mwisho kwa mwaka 2014, inatokea Vingunguti Dar es Salaam ambapo watu wasiofahamika wamekuwa na tabia ya kupiga mawe watu waliopo katika sherehe ya harusi ambazo hufanyika kwenye uwanja.
Dada mmoja ambaye jina lake ni Zay amesimulia kuhusu kisa kimoja ambacho kimejitokeza kwenye sherehe ya harusi ambapo Bibi Harusi alipigwa na jiwe jichoni wakati wakiwa katika tukio la kukata keki.
Warushaji wa mawe hawafahamiki na hawakuonekana kwa kuwa walijificha gizani.
Sherehe hiyo ilivunjika baada ya MC wa shughuli naye kupigwa jiwe na kupasuliwa miwani yake aliyokuwa amevaa.

NICK MINAJ AJUTA KUTOA MIMBA

Nick Minaj aweka wazi sababu za kutoa ujauzito akiwa na umri wa miaka 16

Nick Minaj aweka wazi sababu za kutoa ujauzito akiwa na umri wa miaka 16

minajHitmaker wa ‘Anaconda‘ Nick Minaj ameamua kuweka wazi sababu ya kuamua kutoa mimba wakati akiwa binti wa miaka 16 na kusema maamuzi hayo yaliuvunja moyo wake.
Nilijua ningekufa baada ya kufanya vile“…Wakati huo nilikua bado binti mdogo,nilikua na wakati mgumu sana ambao sijawahi kukutana nao tena,”anasema Nick Minaj alipokua akizungumza na jarida la Rolling stone.
Kwa mujinu wa jarida hilo liliandika kuwa mtu aliyempa mimba alikua ni mzee ambaye alikua na mahusiano naye wakati bado akisoma katika chuo cha mafunzo ya muziki na sanaa cha Manhattan’s Fiorello H. LaGuardia High School of Music & Art.
“Sikua tayari kubeba ujauzito kwa wakati huo na haikua chaguo langu kwani sikuwa na chochote cha kumpa mwanangu…najua wengi hawatapenda hiki ninachoongea,”alisema.
Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia, kumekucha blog

HILARY CLINTON NDIE ANAEPEDWA ZAIDI MAREKANI

Obama, Hillary Clinton kwenye rekodi hii mwaka 2014…

Obama, Hillary Clinton kwenye rekodi hii mwaka 2014…

BO
Tathmini kutoka Marekani imeonyesha idadi ya watu ambao wanapendwa zaidi Marekani kutoka sehemu mbalimbali Duniani.
Hii si mara ya kwanza kufanyika kwa tafiti hiyo, mara zote kumekuwa na majina tofauti yakijitokeza kila siku lakini kwa upande wa wanawake, Iron lady Hillary Clinton ameendelea kuwa kinara, akifuatiwa na Oprah Winfrey na nafasi ya tatu ikishikwa na Malala Yousafzai ambaye  ni mwanaharakati kutoka Pakistani.
Kwa upande wa wanaume Rais wa Marekani, Barack Obama ameongoza kwenye list hiyo, Papa Francis ameshika nafasi ya pili na Bill Clinton ameshika nafasi ya tatu.
Itazame list kamili hapa
LIST
Hii ni ya kutoka Marekani, nitafurahi ukiniandikia kwa hapa Bongo watu wako watatu waliokuvutia zaidi mwaka 2014.
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,kumekucha blog

colobo zilizofanya vizuri mwa 2014

Rekodi ya List ya Collabo za Muziki zilizofanya vizuri mwaka 2014 iko hapa mtu wangu…

Rekodi ya List ya Collabo za Muziki zilizofanya vizuri mwaka 2014 iko hapa mtu wangu…

The-Hit-List_Chan-Lo-700x457Ikiwa imebaki saa chache kumaliza mwaka, tathimini bado zinafanyika kwa mambo ambayo yametokea mwaka mzima.
Burudani mara zote imekuwa karibu na maisha yetu, ikiwemo muziki.
Kwenye rekodi mbalimbali zilizovunjwa kwa kufanya vizuri mwaka huu, ipo hii ya list ya Top Ten ya zile Collabo zitakazokumbukwa zaidi kwa kufanya vizuri Mwaka 2014 kwenye muziki.
  1. Hangover- Psy feat. Snoop Dogg.
  2. Flawless (Remix)- Beyonce feat. Nicki Minaj.
  3. Sing- Ed Sheeran feat. Pharrell Williams.
  4. Uptown Funk- Mark Ronson feat. Bruno Mars.
  5. Bang Bang- Jessie J feat. Ariana Grande & Nicki Minaj.
  6. Love Never Felt So Good- Michael Jackson feat. Justin Timberlake.
  7. Can’t Remember to Forget You- Shakira feat. Rihanna.
  8. Fancy- Iggy Azalea feat. Charli XCX.
  9. Dark Horse- Katy Perry feat. Juicy J.
  10. Ew!- Jimmy Fallon feat. Will.i.am.
Kilichonishtua kwenye list hii kuna majina machache sana ya mastaa.
Kwako mtu wangu, nikikuomba uangalie muziki wa Bongo 2014 halafu uniandalie list ya Top 3 ya Collabo ulizozipenda utaipangaje? Nitafurahi ukiniandikia.
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,kumekucha blog

SOMA MAKUU YALIYOJIRI MAGAZETINI, TZ

Stori zote muhimu zilizoandikwa kwenye Magazeti ya leo Tanzania Dec 31, 2014 Nimekuwekea hapa

STORI ZILIZOPEWA UZITO NA MAGAZETI YA LEO ZINALETWA KWENU NA MABINGWA WA TIBA ASILI, NI MKOMBOZI SANITARIUM CLINI , CHUDA TANGA

Stori zote muhimu zilizoandikwa kwenye Magazeti ya leo Tanzania Dec 31, 2014 Nimekuwekea hapa

lineee
JAMBOLEO
Mtu mmoja aliyekua ameandaliwa mazishi baada ya madai kuwa amefariki Wilayani Kiteto, Manyara ameonekana hai na kushangaza waombolezaji waliokua wanajiandaa na mazishi hayo.
Akizungumza kwa njia ya simu Diwani wa Kata Matui Othamn Kidawa alisema walipata taarifa za kuuawa kwa ndugu huyo na wenzake shambani na kuamua kuubeba mwili wa marehemu.
“Tulipofika shambani tulikuta uharibifu mkubwa uliofanywa na watu wanaodaiwa kuwa ni wafugaji na kuteketeza nyumba nne kwa moto na mali zote zilizokuwemo ndani”alisema.
Alisema wakiwa na askari waliokua na taarifa za kifo na wananchi waliofanikiwa kumpata majeruhi mmoja na baadaye Hassan Abdalah alidaiwa kufa.
Kwa mujibu wa Abdalah alisema alinusurika kuuawa baada ya kuvamiwa saa mbili usiku na wamasai waliowataka waondoke eneo hilo kwa madai kuwa ni eneo la malisho.
Alisema alipokua njiani alipokea taarifa kwa njia ya simu kuwa ndugu zake wameandaa mazishi kwa ajili yake na tayari walichimba kaburi na maandalizi mengine.
NIPASHE
Mtotomwenye ulemavu wa ngozi ‘Albino’ Pendo Emannuel mwenye miaka minne ameibiwa katika kijiji chaoWilaya ya Kwimba Mkoani Mwanza akiwa amelala na wazazi wake.
Kamanda wa Polisi Mwanza ValentinoMlowola alisema tukio hilo lilitokea Desemba 27 baada ya watu haokuvunja mlango kwa kutumia jiwe maarufu Fatuma nakuingia ndani.
Alisema watu hao baada ya kumchukua mtoto waliondoka kwa kasi wakitumia pikipiki na kutokomea pasipojulikana na askari kupata taarifa majira ya saa 7 usiku na kuanza kumsaka.
Mlowola alisema askari wake kwa kushirikiana na familia hiyo itamsaka mtoto huyo popote pale aidha akiwa amekufa ama mzimana kuhakikisha wahusika wanachukuliwa hatua kali.
NIPASHE
Kikao baina ya Waziri Mwakyembe na wadau wa Bandari ya Dar es salaam kimeibua ufisadi unaodaiwa kufanywa na kampuni ya kupakua na kupakia mizigo bandarini ya TICTS ambao umekua ukiwaumiza wateja wanaotumia bandari hiyo.
Ufisadihuo ambao uliibuliwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha wakala wa forodha na uondoshaji wa shehena Tanzania TAFFA,Edward Urio unadaiwa kufanywa na TICTS kwa kuwatoza wateja wa bandari hiyo viwango vya ubadilisha dola ya Marekani kwenda Shilingi ya Tanzania kinyume cha utaratibu wa nchi.
Waziri Mwekyembe amemwagiza Mtendaji mkuu wa TICTS na menejimenti yake kwenda ofisini kwake leo wakiwa na maelezo ya kutosha kwanini wanakiuka taratibu za nchi na wameanza lini kufanya hivyo.
Kabla ya kutoa maelezohayo Mwakyembe alitaka kujua kutoka Sumatra kamawanataarifa na kashfa hiyo na walithibitisha wanazo na kwamba wamekwisha kuindikia TICTS barua kuhusiana na suala hilo na Meneja wa TICTS alithibitisha kupokea barua hiyo.
MWANANCHI
Mkazi wa Geita aliyekua mjamzito wa miezi saba Meleciana Kubezya mwenye miaka 35 ameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na watu wasiofahamika chanzo kikitajwa kuwa ni imani za kishirikina na kugombania mashamba ya urithi.
Diwani wa Kata ya Bukombe alisema mauaji hayo yalitokea saa 2 usiku wakati mjamzito huyo akiwa nyumbani kwake na watoto wake wakati watu hao walipokua wakipita huku wakitafuta ng’ombe wao aliyepotea.
Alisema binti wa marehemu alisema hawajaona ng’ombe aliyepotea ndipo watu hao walipomba maji ya kunywa kwa madai wamechoka sana kutokana na kuwatafuta kwa muda mrefu na alipokwenda kufata maji ndipo walitumia muda huo kumuua mama yake.
“Walipogundua amepoteza maisha walikimbia kusikojulikana na wakati wanampiga aliwauliza kwa nini mnanipiga…?,kosa langu ni lipi kwanini mnaniua,lakini hauaji hao hawakutaka kumsikiliza…
MWANANCHI
Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mbeya imegundua viwanja na nyumba zaidi ya 10 za Serikali zikitumiwa na watu binafsi katika mazingira ya kutatanisha.
Nyumba zilizoubwa na utata huo zipo maeneo ya Uzunguni,Uhindini na Mwanjelwa moja ikiwa na vyumba vitano pamoja na maduka.
Pia imegundua mashamba yake yalilimwa mazao mbalimbali na watu binafsi katika maeneo ya Foresy ya zamani na mpya.
Katibu Tawala msaidizi Hamis Kaputa jana kuwa taarifa zaidi ya nyumba hizo zitatolewa na aliyekua Mwenyekiti wa tume ya uchunguzi ambaye kwa sasa yupo likizo.
Alisema taarifa ya tume ilishaandaliwa na kupelekwa kwa Waziri mkuu Pinda ambaye ndiye aliyetaka apatiwe matokeo ya kazi hiyo.
MWANANCHI
Mvua kubwa isiyotabirika inatarajiwa kunyesha sehemu mbalimbali nchini hasa ukanda wa Pwani ya Kaskazini maeneo ya jijini Dar es salam,Unguja na Pemba pia katika ukanda wa Kaskazini Mashariki kwa Mikoa ya Kilimanjaro,Arusha na Manyara.
Akitoa taarifa hiyo ya hali ya Hewa,Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa TMA Agnes Kijazi alisema mvua ya msimu katika maeneo hayo inatarajiwa kuisha leo.
Hata hivyo alisema mvua kubwa ya nje ya msimu inatarajia kuanza kipindi cha Januari 2015 na itaikumba pia Mikoa ya Mwanza,Kagera,Shinyanga na Geita.
Alisema mvua hiyo inasababishwa na ongezeko la joto linalolifanya anga kushindwa kutengeneza unyevunyevu ambao hugeuka kuwa mvua.
“Ninawashauri wananchi kuchukua hatua za kujikinga na athari za kiafya na mazingira zinazoweza kusababishwa na ongezeko la joto linaloendelea sambamba na mvua kubwa kunyesha”alisema.
MTANZANIA
Aliyekua Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka amesema hayuko tayari kujiuzulu ujumbe wa kamati kuu ‘CC’ ya Chama cha Mapinduzi.
Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya Rais Kikwete kutangaza kumfuta kazi katika mkutano wake na wazee wa Dar es saalam uliofanyika Decemba22 mwaka huu.
Karibu msaidizi Kazi maalum wa Tibaijuka,Nassor Hussein alisema suala la Tibaijuka kujiuzulu nafasi yake ya Ujumbe wa CCM lipo chini ya viongozi wa Kitaifa wa Chama hicho ambao hao ndio watakaoamua.
“Tibaijuka hayupo tayari kujiuzulu kwa sasa ujumbe wa kamati kuu,anachosubiri ni uamuzi wa Chama,jambo hilibado lipo kwa wakubwa na ni siri kwa kuwa lipo kiutendaji,hivyo litaamuliwa na kamati kuu ya chama husika”alisema
Nakuhakikishia kwamba nitakufikishia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia kumekucha blog

BABA WA BEYONCE AUZA CD MITAANI

Story za alichosema Baba wa Beyonce kuhusu kufilisika…Picha nyingine za Jay Z na Beyonce Thailand

Story za alichosema Baba wa Beyonce kuhusu kufilisika…Picha nyingine za Jay Z na Beyonce Thailand

vibe-vixen-beyonce-and-matthew-knowlesKulikuwa na story mitandaoni ambazo hazikuwa nzuri kwa familia ya mzee Mathew Knowles, ikasemekana eti amefilisika mpaka kafikia hatua ya kuuza vitu mbalimbali ikiwemo nguo za mtoto wake, yaani Beyonce pamoja na CD za nyimbo.
Hii haikuwa taarifa nzuri, Beyonce kaongoza kwa kuingiza pesa nyingi upande wa mastaa wa kike Marekani, ina maana amemtelekeza Baba yake kiasi hicho?
Mzee Knowles amekanusha story hizo; “Ningehitaji pesa nisingeuza T-shirt ya dola 5, ningeuza tuzo ya Grammy au BET…
beyonce-garage-sale-jpg
Mzee huyo kasema anauza vitu hivyo ili kupunguza mlundikano wa vitu ambavyo vilikuwa vinajaza nafasi tu ndani ya jengo la ofisi yake ambayo anapanga kuikarabati upya mwaka 2015.
Kwa hesabu ya haraka haraka ya vitu anavyoviuza Mzee Knowles ni kama atapata dola 2000/= tu.
Hayo yanaendelea Marekani, lakini Beyonce yuko na familia yake, Jay Z na mtoto wao Blue Ivy maeneo ya Thailand, picha za mwisho wameshare wakiwa kwenye ukumbi mkubwa wa Michezo wa  Muay Thai wakiangalia mchezo wa ngumi.
Jay Z iii Jay Z
Hapa kuna video inayoonyesha Mzee Knowles akiendelea na mauzo ya vitu hivyo.

Nakuhakikishia kwamba nitakufikishia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,kumekucha blog

Tuesday, December 30, 2014

KISIWA HARISHI (22)


HADITHI
 
KISIWA CHA HARISHI (22)
 
ilipoishia toleo lililopita
 
“Sidhani kama hapa ni karibu na kwenu Comoro. Mimi nadhani kama tutapata msaada wa kuokolewa tutapelekwa kwanza Zanzibar” nikasema.
 
“Si vibaya Zanzibar pia ni nyumbani lakini baba akipata habari atatuma ndege siku hiyo hiyo ituchukue pamoja na nyinyi”
 
“Itakuwa raha sana tukienda Comoro na kupokewa na rais” nikasema.
 
Shazume alikuwa kimya akitusikiliza. Bila shaka alikuwa anaona tunajidanganya kujifariji. Kwa mawazo yake sisi tulikuwa ni wa kufa tu.
 
“Si unajua mzazi aliyekwishamkatia tamaa mwanawe halafu anaambiwa amepatikana, atafurahije?” Yasmin akaniuiza.
 
“Atafurahi sana”
 
Iliwezekana tulikuwa tulikuwa tunajidanganya kweli kama alivyowaza Shazume lakini tulifarijika. Saa zikapita.
 
Tulipomaliza kula Yasmin alileta storitofauti tofauti kutuondoa katika mawazo mabaya. Tukawa tunazungumza.
 
Aliondoka jioni sana. Tukamsindikizakwa pamoja hadi nusu ya njia, tukarudi. Tukakaa kwenye kile kisehemu chetu kusubiri usiku. Hatukujua nini kitatokea kati yetu usiku huo.
 
SASA ENDELEA
 
Usiku ule tulikesha macho kwa sababu ya hofu. Tulikuwa tumejilaza chini kila mmoja upande wake lakini hakukuwa na aliyelala usingizi. Mara kwa mara nilimuona Shazume akijigeuza kila upande.
 
Ilikuwa kati kati ya usiku Shazume aliposhika mguu wangu. Sikujua kama alikuwa anataka kuniamsha au alitaka kujua nilikuwa macho lakini aliponishika nilishituka nikarusha mguu wangu.
 
“Nini?” nikamuuliza nikiizuia sauti yangu isisikike sana.
 
“Nimebanwa na haja ndogo” akaniambia.
 
“Sasa?” nikamuuliza.
 
“Tunaweza kutoka nikajisaidie”
 
“Haya tutoke” nikamwambia.
 
Shazume akainuka na mimi nikainuka. Akatangulia kutoka kwenye mlango. Kulikuwa giza sana. Hatukuweza kuona kwa mbali.
 
“Twende nje au uani?” Shazume akaniuliza.
 
“Naona tutoke uani” nikamjibu.
 
Shazume akaelekea upande wa uani. Mimi nilikuwa nikimfuata nyuma. Alifungua mlango akachungulia uani. Mwezi ulikuwa unaangaza, ua ulikuwa mweupe. Baada ya kuchungulia kwa tahadhari Shazume alivuka kizingiti cha mlango akatoka uani na mimi nikatoka.
 
Yeye alikwenda upande wake na miminilikwenda upande wangu tukachutama na kujisaidia. Mimi sikuwa na haja ndogo lakini baada ya mwenzangu kuniambiana mimi nikaisikia.
 
Tulipomaliza haja zetu tulirudi ndani tukajilaza tena. Safari hii tulipojilaza tu usingizi ulitupitia tukalala.
 
Wakati nipo usingizini niliota Harishi anatufukuza baada ya kutufuma tukiwa na Yasmin kwenye lile jumba lake. Tukaingia katika chumba kimoja kujificha chini ya mvungu wa kitanda. Muda si muda Harishi akafungua mlango na kuingia mle chumbani kututafuta.
 
Akaona mguu wa Shazume umetokeza chini ya mvungu. Akaushika na kuuvuta. Shazume akawa anapiga kelele kuniita.
 
Kelele hizo ndizo zilizoniamsha. Nikaamka na kuangaza macho. Nikasikia Shazume akiendelea kupiga kelele kuniita lakini sauti yake ilitokea kwa juu, sio pale chini tulipolala. Nikashituka sana kwa kujua kuwa haikuwa ndoto.
 
Nikatazama juu. Kwanza niliona kanzu nyeupe halafu nikaona upanga uking’aa. Nilipoona hivyo nilijisogeza zaidi ndani ya makorokoro na kuendelea kuchungulia.
 
Nilimuona Shazume ameinuliwa juu juu na Harishi. Nikajiambia kumbe ile ndoto ilikuwa ni kweli. Shazume alitolewa mle chumbani. Sikuweza kujua Harishi aliwasili muda gani na kumkamata Shazume.
 
Bila shaka kilichokuwa kimeninusuru mimi, ni kuwa nililala nyuma ya mlango. Harishi alipoingia alimuona Shazume na kumkamata yeye.
 
Ile ndoto niliyoota ilikuwa ya kweli. Harishi alikuwa ametuingilia!
 
Jitihada zetu za kujaribu kumkwepa zilikuwa za bure kwani Harishi alikuwa akitugundua kila tulipokwenda kujificha na sababu ni kuwa alikuwa akifuata harufu zetu kama vile m’bwa.
 
Harishi alipomtoa Shazume ukumbini, nilimsikia Shazume akipiga ukulele mmoja tu “Nakufa!”. Halafu sikusikia kitu tena.
 
Moyo ulikuwa ukinienda mbio na nilikuwa nikihema kwa nguvu kama niliyekuwa nafukuzwa. Tukio hilo lilikuwa la ghafla sana kiasi kwamba nililazimika kujiuliza, kama bado nilikuwa kwenye ile ndoto au kilichokuwa kinatokea kilikuwa kweli.
 
Hofu yangu sasa ilikuwa kwangu. Nilijiua Harishi akimaliza kumuua Shazume ataniingilia na mimi kwani alipoingia humo chumbani alituona tukiwa wawili.
 
Wazo hilo likanifanya nizidi kujisogeza kwenye makorokoro ili Harishi akiingia tena asinione. Lakini muda ulipita. Sikumuona tena Harishi.
 
Nikaendelea kukaa hapo hapo hadi nikaona kunakucha. Nikahisi kwa muda ule Harishi atakuwa ameshaondoka. Nikajiburuza kujitoa kwenye yale makorokoro nilikojiingiza.
 
Nilinyata hadi kwenye mlango nikaufungua na kuchungulia ukumbini. Nilichungulia upande wa mbele na upande wa uani. Niliiona maiti ya Shazume imelala chini kando ya mlango wa chumba tulichokuwemo. Harishi mwenyewe hakuwepo.
 
Nikatoka nje na kuangalia kila upande. Sikuona kitu. Kando ya ile nyumba palikuwa na mti. Nikapata wazo kuwa nipande juu ya ule mti kujificha. Nikaenda kwenye mti huo nikaupanda na kukaa kwenye tawi mahali ambapo nisingeweza kuonekana.
 
Wakati nipo juu ya ule mti nilimuona Yasmin kwa mbali akija. Nikajiambia tuliobaki katika kisiwa kile tulikuwa watu wawili tu, mimi na Yasmin.
 
Sikupenda kujisifu kuwa nilikuwa nina bahati kwa sababu nimenusurika. Nilijua kuwa wakati wangu ulikuwa haujafika. Pengine niliandikiwa niwe wa mwisho kufa.
 
Historia ya kisiwa hicho tangu tulipofika kila siku alikufa mtu. Leo nimeishuhudia maiti ya Shazume, huenda kesho Yasmin ataishuhudia maiti yangu.
 
Yasmin alipofika pale nilimuacha aingie mle ndani. Mara moja nikamuona ametoka akiwa amechanganyikiwa. Bila shaka alikuwa ameshitushwa na maiti ya Shazume.
 
ITAENDELEA KESHO, USIKOSE KESHO NINI KITAJIRI

HIFADHI YA TAIFA MKOMAZI YAKABIDHI JENGO LA MAMA NA MTOTO LENYE THAMANI YA MILIONI 81 SAME

Kumekucha blog

Same,MKUU wa Wilaya ya Same, Herman Kapufi, amewataka wakazi wanaokaa ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi kuacha kushirikiana na majangili na badala yake wawafichue vyenginevyo atakaebainika kufanya hivyo atafikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mheza kata ya Maore wakati wa kukabidhi mradi wa jengo la wodi ya mama na mtoto lililojengwa na Hifadhi ya Taifa Mkomazi(Tanapa), Kapufi amesema Serikali imejipanga kukabiliana na ujangili ndani ya hifadhi hiyo.

Amedai kuwa ziko taarifa za baadhi ya watu kuwahifadhi na kuficha taarifa za majangili ndani ya hifadhi hiyo na hivyo kuwataka kuacha kufanya  mara moja vyenginevyo wanaweza kujikuta wakikabilia na mkono wa sheria.

“Ndugu zangu  munaokaa ndani na nje ya hifadhi ya taifa ya Mkomazi tuache kuwalinda majangili wanaotumalizia rasilimali zetu----tukiwalinda watatumalizia vivutio vyetu na watalii hawatakuja na tutakaoathirika ni sisi” alisema Kapufi

“Hifadhi ni ya kwenu ninyi wenyewe na matunda yake ni kama haya ya leo---kama sio hifadhi ya taifa mkomazi jambo hilo lisingekuwepo na taarifa nilizonazo ni kuwa kuna mengi wamewafanyia” alisema

Akizungumzia baadhi ya watu kuchimba madini na kukata miti ndani ya hifadhi hiyo, Mkuu huyo wa Wilaya amekemea vikali na kusema Serikali imejipanga kukabiliana na jambo hilo na kuwataka kuacha mara moja.

Alisema  vitendo hivyo vinachangia kuwakimbiza wanyama na mvua kunyesha na kusema kuwa hakikubaliki na operesheni ya kulikomesha jambo hilo litaanza mara moja ikiwa ni kuzilinda rasilimali za nchi.

Awali akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Mkomazi, Donat Mnyagatwa, alisema mradi huo hadi kukamilika kwake umegharimu zaidi ya shilingi milioni 81 ikiwa wananchi wamechangia milioni 24.

Alisema mradi wa jengo la wodi ya mama na mtoto limekuja baada ya hifadhi hiyo kuona kero wanayoipata wakazi wa vijiji vya Mheza na Maore pamoja na vijiji jirani.

“Sisi Mkomazi baada ya kuona kero ya wananchi wanayoipata wenzetu mama wajawazito tukaona ni vyema tutawapunguzia usumbufu wa kufuata huduma masafa marefu kwa kujenga kituo hapa Maore” alisema Kapufi

Alisema mradi wa jengo hilo litakuwa msaada mkubwa kwa wakazi hao na vijiji vya jirani kwani kwa muda mrefu walikuwa katika adha na mateso na hivyo kuwataka kulitunza ili kuwa mkombozi kwa mama wajawazito na watoto.

                                  Mwisho

HIFADHI YA TAIFA YA MKOMAZI YAKABIDHI JENGO LA WODI YA WAZAZI KIJIJI CHA MHEZA SAME


 Wakazi wa kijiji cha Mheza na Maore Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro  wakifuatilia maelekezo ya huduma ya mama na mtoto wakati wa makabidhiano ya mradi wa wodi ya mama na mtoto iliyojengwa na Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi na kugharimu zaidi ya shilingi miloni 81 ambapo kati yake nguvu za wananchi ni milioni 24.





 Mkuu wa Wilaya ya Same, Herman Kapufi akikata utepe kuashiria kufunguliwa kwa kituo cha wodi ya mama na mtoto kijiji cha Maore Wilayani humo jana kilichojengwa na Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi kwa gharama zaidi ya shilingi milioni 81 ambapo nguvu za wananchi wamechangia milioni 24. Kulia kwake ni Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Mkomazi, Donat Mnyagatwa.

 Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, Donat Mnyagatwa akikabidhi taarifa ya mradi wa jengo la wodi ya mama na mtoto kwa Mkuu wa Wilaya ya Same, Herman Kapufi kijiji cha Maore Same Wilayani Kilimanjaro jana
 Mkuu wa Wilaya ya Same, Herman Kapufi na wakazi wa kijiji cha Mheza na Maore Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro wakifurahia baada ya kuzinduliwa kwa wodi ya mama na mtoto jana kilichojengwa na Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi kwa gharama zaidi ya shilingi milioni 81 ambapo nguvu za wananchi ni milioni 24

UTAFITI,FURAHA DUNIANI UMEONGEZEKA

Unafahamu kuwa furaha imeongezeka duniani mwaka 2015.

Unafahamu kuwa furaha imeongezeka duniani mwaka 2015.

8813468-happy-girl-wallpaper
Utafiti uliofanyika katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka umegundua kuwa hali ya kuwa na furaha miongoni mwa watu mbalimbali duniani kwa jumla imeongezeka katika kipindi cha mwaka mmoja .
Kwa mujibu wa utafiti uliofanyika kwenye nchi 65 ambao ulihusisha watu wapatao 64,000 furaha itokanayo na sababu mbalimbali imeongezeka tofauti na hali ilivyokuwa mwanzoni mwa mwaka.
Utafiti huu umeoneysha kuwa angalau asilimia 70% ya watu katika mataifa ambayo yamehusika kwenye utafiti huu wameridhika na hali ya maisha yao jambo ambalo linaongeza furaha .
Taifa la Fiji ambalo liko kwenye bara la Oceani kusini mashariki mwa dunia limeonekana kuwa taifa linaloongoza kwa furaha kutokana na asilimia 93% ya raia wanaoishi kwenye taifa hilo kuridhika na maisha yao .
Taifa la Fiji limetajwa kuwa taifa linaloongoza kwa furaha kwa mwaka 2014.
Taifa la Fiji limetajwa kuwa taifa linaloongoza kwa furaha kwa mwaka 2014.
Kinyume na Fiji taifa la Iraq limeonekana kuwa taifa linaloongoza kwa majonzi na furaha duni baada ya majibu ya utafiti kuonyesha kuwa taifa hilo lina asilimia 31% pekee ya watu wanaoridhishwa na maisha yao .
Katika hali isiyiokuwa ya kawaida bara la Afrika limetajwa kwenye utafiit huo kuwa bara linaloongoza kwa furaha ambapo asilimia 83 % ya wakazi wa bara hilo wamekiri kufurahishwa na maisha kwa jumla .
Eneo la ukanda wa magharibi mwa bara la ulaya limeonekana kuwa eneo ambalo watu wake hawana furaha kuliko maeneo yote kutokana na kuwa na asilimia 11% pekee ya watu ambao wamekiri kuwa na furaha maishani mwao
Iraq imeonekana kuwa nchi yenye furaha kwa kiwango cha chini kuliko yote duniani .
Iraq imeonekana kuwa nchi yenye furaha kwa kiwango cha chini kuliko yote duniani .
Katika utafiti huo asilimia 65% ya watu ulimwenguni kote walikuwa na maoni kuwa mwaka 2015 utakuwa mwaka mzuri kuliko mwaka 2014 baada ya robo tatu ya wakazi wa bara la Afrika na asilimia 26% ya wakazi wa magharibi mwa bara la ulaya wakiwa na uhakika juu ya kupata aina Fulani ya maendeleo katika mwaka ujao .
Utafiti huo pia umeitaja Nigeria kuwa nchi yenye hisia chanya kuliko mataifa yote huku Lebanon likiwa taifa linaloongoza kwa kuwa na hisia hasi kuliko yote .

KANYE WEST AWAFUNIKA MASTAA KIBAO KWA MAVAZI

Eti Kanye West anawafunika mastar wengine wa kiume kwa mavazi?

Eti Kanye West anawafunika mastar wengine wa kiume kwa mavazi?

Kanye WestzoooKumekuwa na mashindano ya ubunifu wa mitindo mbalimbali ya mavazi, wakati mwingine tumeona mastaa ambao hubuni mavazi yao wenyewe, hivi ukiambiwa umchague staa wa kiume ambaye ameongoza kwa kuvaa vizuri zaidi utamchagua nani?
Nilishawahi kusikia watu wakisema eti jamaa hajui kupangilia mavazi, ana mtindo wa kuvaa ambao hauvutii na ukimuangalia unaona kwamba ni kama hajali kuhusu mavazi yake.
Jarida la GQ wamefanya tafiti zao na watu wamepiga kura, majibu yemeonyesha kuwa rappa Kanye West, ndiye bingwa wa kutupia swaga kwa mwaka 2014.
Jamaa waliofanya tafiti wamesema mavazi ya Kanye West yametafsiri na kubadili mazingira ya fashion kwa wanaume wengi, mavazi yake ni kama yamekuwa yakielezea kesho zaidi kwenye Dunia ya mitindo.
Kwenye utafiti huu, Kanye kawashinda mastaa wengi ikiwemo staa wa movie ya ‘Long Walk to Freedom , Idris Elba.
Je unakubaliana na tathimini za Jarida la  GQ kuwa Kanye West ndio ameleta mapinduzi katika mtindo wa uvaaji kwa wanaume 2014?
showdowfinal-600x404Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia kumekucha blog