Tuesday, June 30, 2015

NI PESA YAKO TU

Ni pesa yako tu! utanunua hata hili gari linalotembea barabarani na juu ya maji baharini.

GARI LA MAJININi dunia yenye vitu vingi na ubunifu mwingi kwenye kila kona ya kitu unachokijua, yaani kuna watu kila siku wanaumiza vichwa kutengeneza pesa kwa njia ya kiubunifu zaidi ambapo hii ya magari yanayoweza kutembea juu ya maji ni mojawapo.
Watercar ni kampuni ya Marekani ambayo ilianzishwa mwaka 1999 ambapo mwaka 2013 kampuni hii ilitengeneza gari la kwanza la kibiashara.
GARI LA MAJINI 2
GARI LA MAJINI 3
GARI LA MAJINI 4
GARI LA MAJINI 5
GARI LA MAJINI 6
Kwa habari ,amtukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

THE ROCK AACHANA NAMIELEKA

The Rock ameweka wazi sababu za yeye kuacha mchezo wa mieleka…

tr
Dwayne  Johnson maarufu kama The Rock ni mwigizaji, movie producer na mchezaji mieleka kutoka Marekani aliejitengenezea jina kubwa kwenye mieleka na kufanya apate shavu kubwa kwenye movie za action HollywoodMarekani.
The Rock alichukuwa time na kufanya interview na gazeti la Marekani Esquire na kuongelea mambo mengi ikiwemo sababu zilizomfanya aingie kwenye tasnia ya uwigizaji pamoja na mafanikio yake binafsi. The Rock alikuwa na haya ya kusema:
ex
Dwayne Johnson kwenye movie ya The Expendables 3 ambayo ndani Bruce Wills ameonekana pia.
Kuhama kwenye mieleka kwenda kwenye uwigizaji:“Baada ya kufanikiwa kwenye mieleka, nilihamasika kujabiru uwigizaji wa movie za action, na nimefika hapa nilipo kwa kutumia nidhamu niliojinfunza kwenye mieleka, kujenga ukaribu na watu kwenye industry, na kujiunga na madarasa ya kuigiza”.
gi
Dwayne Johnson kwenye movie nyingine kali ya G.I. JOE Retaliation.
Kama anapendelea uwigizaji zaidi kuliko mieleka:Mieleka ni mpenzi wangu wa kwanza, lakini kwenye uwigizaji kuna upendo tofauti ambao unaniruhusu mimi kugusa watu kupitia sanaa nyingine na pia kutengeneza hela ndefu zaidi, movie zinanifundisha mambo mengi sana ambayo nisingeweza kuyajua mwanzoni”.
saaaaan
Hapa ni kwenye movie aliyoigiza mwaka huu SAN ANDREAS, movie iliofanya vizuri Marekani.
Kama alichukuliwa serious alivyoanza kuigiza: “Haikuwa rahisi hapo mwanzoni, kama Anorld Schwarzenegger niliambiwa nina mwili mkubwa kuwa mwigizaji wa movie za action na nilinyimwa nafasi nyingi lakini sikukata tamaa, na leo niko hapa kwa sababu sikuchoka”.
Kwa habari, amtukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

PITTER CECH AJIUNGA RASMI ARSENAL

Arsenal yampa Cech mkataba miaka minne

Hatimaye yametimia kwa Arsenal kupata saini ya mlinda mlango Petr Cech kutoka Chelsea kwa kitita cha pauni milioni kumi.
Mlinda mlango huyo wa kimataifa kutoka Jamhuri ya Czech, ambaye amecheza zaidi ya mechi 400 katika misimu 11 akiwa na timu ya Chelsea, amejiunga na Arsenal the Gunners kwa mkataba wa miaka minne.
Cech, mwenye umri wa miaka 33, alicheza mechi saba tu msimu uliopita baada ya nafasi yake kunyakuliwa na mlinda mlango kutoka Ubelgiji Thibaut Courtois.
Cech amesema alifikiri angestaafia Stamford Bridge, alakini ameongeza kusema: "Maisha daima hayawi vile unavyofikiria yakawa."
Ameandika: "Msimu ulioopita wa kiangazi, mambo yalibadilika na nikaelewa kuwa sikuwa mlinda mlango chaguo la kwanza, lakini nilifikiria haukuwa wakati mzuri kwangu kuondoka.
"Wakati wa msimu huo, ilieleweka wazi kuwa hali yangu isingebadilika na kama ninavyofahamu siko katika kazi yangu ambapo nastahili kuwa- Niliamua kuondoka na kutafuta changamoto mpya."
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger anasema: "Petr Cech ni mchezaji ambaye nimemtamani kwa muda mrefu na nimefurahi sana ameamua kujiunga nasi."
Cech, alijiunga na Chelsea akitokea klabu ya Rennes ya Ufaransa Julai 2004 na kushinda makombe 13 akiwa na Chelsea - likiwemo kombe moja la klabu bingwa na mataji manne ya ubingwa wa ligi kuu ya England.
Kwa habari , matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

MUGABE AMKEBEHI, OBAMA

Maneno ya utani ya Rais Mugabe kwa Obama baada ya kuruhusu ndoa ya jinsia moja…

mugabe
Ndani ya wiki moja baada ya Serikali ya Marekani kupitisha Sheria ya kuruhusu Ndoa za jinsia moja kwa raia wake kumekuwepo na maoni mbalimbali kutoka kwa watu kuhusiana na maamuzi hayo.
Mmoja wa watu walioguswa na maamuzi hayo ni Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe ambaye ameeleza hisia zake baada ya maamuzi hayo kupitishwa.
obama
Rais wa Marekani Barack Obama
Katika mahojiano na radio ya Taifa ya Zimbwabwe, Mugabe alisema hawezi kupingana na maamuzi ya nchi hiyo kwani ni sheria ambayo imepitishwa na Serikali na kama ni hivyo ataamua kufunga safari kwenda mpaka Washington kuomba kufunga ndoa na Rais Barack Obama.
Ameongeza kuwa, Serikali ya Marekani imekuwa ikiongozwa na wajinga ambao ni  wafuasi wa shetani wanaoitukana taifa la Marekani akisisitiza Marekani imechafuka na wanaiendesha nchi kwa dhana zao binafsi ambazo ni potofu.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

MAMA MLA WATOTO AKIKWIDWA NA KUWEKWA KOROKORONI

Mengine ya India yaliyosikika leo ni hii ya mama kumla mtoto wake mwenyewe…

indiaaaa
Kumekuwepo na matukio ya baadhi ya wazazi kuwanyanyasa na hata wengine kuripotiwa kuwaua watoto wao wa kuwazaa wenyewe kutokana na sababu mbalimbali.
Headlines nyingine leo zinatokea kule India ambapo mama mmoja amefunguliwa mashtaka baada ya kuripotiwa kumla mtoto wake wa miaka minne huku akiwa  hai.
Pramila Mondal ambaye anadaiwa  kuwa na matatizo ya akili alifanya kitendo hicho akiwa nyumbani kwake na kukutwa na shemeji yake akiendelea kumla mtoto huyo sehemu mbalimbali za mwili wa mtoto wake huyo ambaye alikuwa wa kike.
Baada ya Polisi kufika na kumshilika mama huyo, mtoto huyo alikimbizwa katika hospitali ya Malda Medical center huku akiwekwa katika chumba cha uangalizi maalum kutokana na kuwa na majeraha makubwa.
Polisi walisema pamoja na mama huyo kudaiwa kuwa na matatizo ya akili pia pombe pamoja na madawa vimechangia yeye kufanya tukio hilo.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

RAMOS KING'ANG'ANIZI

Baada ya Madrid kuikataa Ofa ya Man Utd, Ramos amefanya uamuzi huu

Wiki moja baada ya ofa ya kwanza ya Manchester United kumsajili Sergio Ramos kukataliwa na Real Madrid, hatimaye mchezaji huyo ambaye yupo mapumzikoni ametoa kauli yake.
United walituma ofa ya kwanza ya paundi milioni 28.3 kwa Madrid ili kupata saini ya beki huyo wa kimataifa wa Spain, lakini Madrid waliikataa ofa hiyo.
Hata hivyo baada ya Ramos kugundua Madrid wameikataa ofa hiyo, alichukua uamuzi wa kuwaweka wazi viongozi wa Madrid kupitia wakala wake kwamba anataka kuondoka na kujiunga na United na kuiomba Madrid ikubaliane bei na Manchester United.
Uamuzi huo wa Ramos umeishtua Madrid, ambao walitegemea wangefanya makubaliano ya mkataba mpya na beki huyo.
Madrid wanategemewa kujaribu kumtuliza Ramos na mkataba mnono mpya lakini kaka na meneja wa mchezaji huyo, Rene Ramos ameshaifahamisha Madrid lengo la mteja wake kutaka kuanza maisha mpya sehemu nyingine.
Rene ameripotiwa kusema kwamba Ramos anataka kuhamia Old Trafford wakati huu wa dirisha la usajili na klabu pekee ambayo anataka Madrid ifanye nayo makubaliano ni United.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

UTATA WAIBUKA BAADA YA KIFO CHA MTU BAGAMOYO

Utata wa marehemu kufufuka Bagamoyo upo kwenye Hekaheka ya leo…

ripJana mji wa Bagamoyo uliingia katika taharuki kubwa baada ya habari kuenea kuwa kuna marehemu kafufuka baada ya kuthibitishwa na madaktari kuwa amefariki.
 Umati wa watu katika nyumba ambayo marehemu alikua akiishi ikiwa ni muda mchache baada ya mwili wake kurejea kutoka hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo ambapo ndipo alipofariki.
Majirani walidai baada ya mwili wa marehemu huyo kurudishwa nyumbani ili kuanza taratibu za mazishi walishangaa kuona bado mwili wa moto na alikua akijitingisha wakati waoshaji wakimuandaa kwa ajili ya kumzika.
Shangazi wa marehemu alisema ni kweli baada ya kumleta walishangaa mwili ukiwa wa moto na mapigo ya moyo yakifanya kazi kama kawaida licha ya madaktari kuthibitisha kuwa amefariki, na wakaamu kusimamisha shughuli za mazishi hadi kesho yake walipoona  amekuwa wa baridi na tayari alishafariki.
Daktari aliyethibitisha kama marehemu amefariki alisema baada ya kumpima marehemu alikua amefariki na kuruhusu taratibu ziendelee, na alisema kuwa mwili wa marehemu kuwa wa moto inategemee na mazingira ya sehemu alipohifadhiwa.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

MABILIONEA MASTAA

Forbes imesema hii ndio orodha ya mastaa wenye pesa kwa mwaka wa 2015, Floyd Mayweather na Manny Pacquiao watajwa pia!!


LOS ANGELES, CA - JUNE 28:  Professional boxer Floyd Mayweather, Jr. (L) attends the 2015 BET Awards at the Microsoft Theater on June 28, 2015 in Los Angeles, California.  (Photo by Christopher Polk/BET/Getty Images for BET)
Kama wewe ni shabiki wa mastaa wowote wa mbele, basi utapenda kujua wana thamani ya kiasi gani cha pesa mwaka huu. Forbes imeachia orodha ya wasanii 100 wenye pesa zaidi kwa mwaka huu wa 2015, na kwenye orodha hiyo utakutana na watu kama Katy Perry, Beyonce, Kim Kadarshian, Floyd Mayweather, Manny Pacquiao, Taylor Swift na wengine kibao so unaweza ukavuta picha nani kampiku nani kwenye uwezo wa kifedha mwaka huu.
Staa anayeshika kijiti kwenye orodha ya mwaka huu ni Floyd “Money” Mayweather akiwa na thamani ya millioni $300 , Manny Pacquiao kwenye nafasi ya pili akiwa na thamani ya $160 million, Katy Perry akishika nafasi ya 3 akiwa na thamani ya millioni $130.
Kuonyesha uwezo wake wa kifedha, Floyd “Money” Mayweather kama wengi wanavyomuita ameamua kuweka headline juu ya headline, kaamua kununua gari jipya, gari lenye thamani ya millioni $4.8, aina ya Koenigsegg CCXR Trevita gari ambalo kwenye rekodi ya dunia yapo matatu tu, na sasa akiwa mmoja kati ya watatu wanaolimiliki gari hilo! Gari hilo litakuwa gari lake la 9,mengine nane yakiwa aina ya, Ferrarsi, Porsches, Lamborghinis, Bugattis na ndege yake binafi aina ya Gulfstream V private jet vyote hivi vikiwa na thamani ya millioni $55.
Hapa chini nimekusogezea orodha ya mastaa kumi tuu kutoka kwenye list ya Forbes 100 Richest Celebrities 2015, pamoja na picha ya gari jipya la Floyd Mayweather pamoja na picha inayo onyesha jumla ya magari alionayo na ndege yake.
1. Floyd Mayweather ($300 million)
2. Manny Pacquiao ($160 million)
3. Katy Perry ($130 million)
4. One Direction ($130 million)
5. Howard Stern ($95 million)
6. Garth Brooks ($90 million)
7. James Patterson ($89 million)
8. Robert Downey Jr. ($80 million)
9. Taylor Swift ($80 million)
10. Cristiano Ronaldo ($79.5 million)
FLYOD
Gari jipya la Floyd Mayweather “Koenigsegg CCXR Trevita” yako matatu tu duniani, na hili ni moja wapo.
FLOYD 2
Hii ni picha inaonyesha jumla ya magari na ndege alionayo Floyd Mayweather. Kila gari limewekwa thamani yake.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

KWA MARA YA PILI NDEGE YAANGUKIA NYUMBA ENEO HILO HILO

Ajali ya ndege ya Kijeshi iliyotokea muda mfupi uliopita kwenye makazi ya watu Indonesia… (Pichaz)


Indonesia
Kama uko karibu sana na TV za Kimataifa kama BBC, Sky News na CNN utagundua kwamba kwenye stori kubwa zilizopewa headlines sana iko ya Shambulio la Kugaidi lililotokea Tunisia na kusababisha mauaji ya Watalii.. Breaking News imeingia nayo kwenye stori kubwa zilizo kwenye headlines sasahivi, inahusu Ndege ya Kijeshi kuanguka kwenye makazi ya watu Indonesia na watu 30 wamefariki.
BBC Ajali II

Ndege hiyo ilipata ajali muda mfupi baada ya kuruka kutoka kwenye Uwanja wa Medan Polonia Airport.. ndani ilikuwa imebeba jumla ya watu 12, ndege imeanguka kwenye mtaa ambao una makazi ya watu pamoja na Hoteli, gari moja pia limewaka moto baada ya kutokea ajali hiyo.. eneo lote la ajali limeshika moto.
BBC Ajali

Wenyeji wa eneo hilo wamesema hii ni mara ya pili kwa nyumba za eneo hilo kuangikuwa na ndege, iliwahi kuanguka Boeing 737 mwaka 2005 ikaua watu 143 na kati yao watu 30 walikuwa ni watu ambao wanaishi eneo hilo, hawakuwemo ndani ya ndege.
Map
Vikosi vya Zimamoto na Uokoaji vinaendelea na kazi ya kuzima moto pamoja na kutoa miili ya watu waliofariki kwenye ajali hiyo, huenda idadi ya waliofariki na majeruhi ikaongezeka wakati wowote kuanzia sasa.

SOMA HABARI KUBWA ZILIZOPEWA UZITO MAGAZETI YA LEO, JUNE 30 TZ

Uchambuzi huu wa magazeti unaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha Elimu Cha Candle Education Centre Tanga. Kituo kinaongoza kufaulisha wanafunzi kidato cha pili hadi sita na wanaojiendeleza kielimu. Wapo Tanga mkabala na Bank ya CRDB simu 0715 7727246

bus
MTANZANIA
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, Katavi imemuhukumu mwalimu mstaafu wa shule ya msingi  Mpanda Ndogo , Rashid  Ndogo mwenye miaka 65 kifungo cha maisha jela baada ya kumbala mjuu wake wa miaka mitano na kumuharibu vibaya sehemu zake za siri.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, Chiganga Ntengwa baada ya mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa na pande zote mbili za mashtaka na utetezi.
Awali katika kesi hiyo mwendesha mashtaka alidai mahakamani kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Oktoba mwaka jana majira ya saa 2 na nusu usiku nyumbani kwake katika kijiji cha Majalila.
Siku hiyo mshatakiwa alidaiwa kumbaka mjuu wake wakati amelala chumbani akiwa na mtoto wa mshtakiwa ambaye alishugudia baba yake akitenda kosa hilo la kinyama.
Siku ya tukio mke wa mshatakiwa alimwaga mume wake kuwa amekwenda kufunga zizi la mbuzi lililokuwa jirani na nyumbani kwao na mumewe kutumia mwanya huo kuingia chumbani kwa mjuu wake na kuanza kumbaka huku mwanaye akishuhudia.
Mshakiwa alikamatwa na majirani siku hiyo na kupelekwa kituo cha Polisi ambapo alifunguliwa mashtaka huku mjukuu wake akikimbizwa hospitali kupatiwa matibabu.
MTANZANIA
Jeshi la Polisi Dar  limebaini mabaki ya mwili wa mmiliki wa shule ya Mtakatifu Zion, Anna Mizinga aliyeuawa Desemba mwaka jana na kutupwa kwenye shimo la choo cha shule yake.
Kamanda wa Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam Suleiman Kova alisema  mabaki ya mwili huo yalibainika Juni mwaka huu na tayari watu watatu wanashikiliwa na Polisi wakidaiwa kufanya unyama huo.
Akifafanua juu ya tukio hilo Kova alisema  Februari mwaka huu mtu mmoja alitoa taarifa polisi juu ya kupotea kwa mmiliki huyo tangu Desemba mwaka jana saa 11 jioni na hakuonekana tena.
Alisema mmiliki huyo alindoka nyumbani kwake na gari dogo aina ya Verosa akiwa na mtu mmoja ambaye naye ni miongoni mwa watuhumiwa wanaoshikiwa na jeshi hilo na abada ya taarifa hiyo walifungua jalada la uchunguzi na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao.
Alisema mtuhumiwa wa kwanza alikamatwa Uchira, Moshi na kuwataja wenzake.
“Katika mahijiano mmoja alisema yeye na marehemu waliondoka hadi shuleni kwake na walipofika walivamiwa na watu wapatao wanne na kuanza kupigwa, lakini yeye alifanikiwa kutoroka na kujificha katika uzio wa shule, na aliwaona watu hao wakiendelea kumpiga mama huyo na kisha kumtupa katika shimo la choo kisha kutokomea na gari lake kusikojulika” Kova.
Watuhumiwa hao wanaendele kuhojiwa ili kupata undani wa tukio hilo, ikiwa ni pamoja na kuwatafuta na kuwakamata watuhumiwa wengine wanaohusika na tukio hilo.
MTANZANIA
Waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa amemaliza safari yake ya kusaka wadhamini katika Mikoa yote ya Tanzania na kujikusanyia zaidi ya wadhamini laki 8.
Lowassa alianza safari ya kusaka wadhamini Juni 4 baada ya kuchukua fomu ya kugombea Urais kupitia CCM na jana amehitimisha safari yake hiyo katika Mkoa wa Morogoro.
Hata hivyo kwa mujibu wa kanuni za CCM, kada anayewania kugombea Urais, anatakiwa kuwa na wanachama waliomdhamini 450 kutoka Mikoa 15 ikiwemo mitatu kutoka Zanzibar.
Katika baadhi ya Mikoa ambayo Lowassa alipata wadhamini wengi ni pamoja na Dar es salaam, Arusha, Morogoro, Pwani, Iringa, Mbeya, Ruvuma , Kilimanjaro, Tanga na Singida.
MWANANCHI
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeahirisha kwa muda uandikishaji wa wapigakura katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani hadi hapo itakapotangazwa.
Uandikishaji huo unaofanywa kwa teknolojia inayochukua alama na taswira za mpigakura ‘Biometric Voters Registration’ (BVR)) ulipangwa kuanza Julai 4 hadi 16 kwa Dar es Salaam na Juni 25 kwa Mkoa wa Pwani.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Julius Mallaba alisema jana kuwa kazi hiyo imeahirishwa kutokana na kuchelewa kwa vifaa vinavyotumika kuandikisha wapigakura.
Alisema vifaa vilivyokuwa vinakusudiwa kutumika Dar es Salaam bado vinatumiwa katika mikoa ambayo wananchi wamejitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura.
“Mwitikio umekuwa mkubwa ndiyo maana tumeamua kusogeza mbele tarehe ili wamalizie huku tukiendelea kusubiri vifaa. Tunataka vikija tuishambulie Dar es Salaam kwa kipindi kifupi,”  Mallaba.
Mallaba alisema tarehe ya kuanza tena kwa kazi hiyo kwa mikoa ya Dar es Salaam na Pwani itatangazwa na NEC baada ya kupata vifaa kutoka mikoa itakayokuwa imekamilisha uandikishaji.
“Ninaomba wananchi wafahamu kuwa mwezi uliokuwa umepangwa na NEC kukamilisha zoezi hilo utabaki kuwa Julai. Tarehe tu ndiyo itabadilika,” alisema na kusisitiza kuwa wanataka uandikishwaji kwa jiji hilo uwe wa kipekee ukiwa na vifaa vya kutosha kutokana na idadi kubwa ya watu. Aliwataka wananchi wote wa mikoa hiyo miwili kuwa watulivu wakati huu.
Mbunge wa Ubungo (CHADEMA), John Mnyika alisema NEC imedhihirisha hoja aliyowahi kuitoa bungeni kwamba Bunge liahirishwe ili wajadili suala hilo kwa dharura.
“Kuna udhaifu mkubwa kwa upande wa NEC na Serikali kuhusu BVR… hata baada ya madai kwamba umerekebishwa lakini ukweli ni kwamba hali ni tete hata katika maeneo mengine ambayo uandikishaji unaendelea,” Mnyika.
Alieleza kuwa Dar es Salaam ndiyo itakayoamua mshindi wa urais katika Uchaguzi Mkuu ujao kutoka na idadi kubwa ya wapigakura.
Alidai kwamba kubadilishwa huko kwa ratiba kutatoa mwanya kwa CCM ambayo ilishasema kupitia kwa Nape Nnauye kuwa inajiandaa kufunga goli la mkono kufanya hujuma.
MWANANCHI
Mahakama ya Mkazi Kisutu jana ilishindwa kutoa hukumu ya kesi ya wizi wa milioni 207 kutoka kwenye akaunti ya  madeni ya nje EPA kutokana na mshtakiwa wa tatu kulazwa katika hospitali ya Muhimbili, kitengo cha wagonjwa wa akili.
Hukumu ya kesi hiyo inayowakabiliwa makada watatu wa CCM, Rajabu Maranda na wenzake wanne, sasa itasomwa kesho kutokana na kulazwa kwa mtuhumiwa huyo, Iman Mwakosya ambaye alikuwa mkuu wa kitengo cha madeni ya nje cha benki kuu ya Tanzania.
Wengine kwenye jopo hilo ni Ignas Kitusi na Eva Nkya.
Mahakama itaandika barua kwa hospitali ya Muhimbili kabla ya Julai Mosi kwa ajili ya kupata taarifa kama mshtakiwa huyo anaweza kuelewa mwenendo wa kesi ili waweze kusoma hukumu.
NIPASHE
Magonjwa yasiyoambukiza yakiwamo ya kisukari, moyo na saratani, yanazidi kuongezeka kwa kasi na kuendelea kuwa chanzo kikuu cha vifo duniani kote.
Aidha, inakadiriwa kuwa kisukari pekee kimeathiri maisha ya watu takribani milioni 371 duniani kote huku asilimia 80 ya idadi hiyo ikiishi katika nchi zenye uchumi wa kati na maskini.
Nchini Tanzania, takribani watu tisa kati 100 wana ugonjwa wa kisukari na kwamba mtu mzima mmoja kati ya watatu, ana tatizo la shinikizo la juu la damu.
Kaimu Mkurugenzi kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Hauson Rweumbiza, alisema wakati wa semina ya siku moja iliyowashirikisha waandishi wa habari wa kutoka vyombo mbalimbali.
Lengo la semina hiyo lilikuwa ni kuzungumzia magonjwa mbalimbali yasiyoambukiza.
Alisema gharama ya kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza duniani kote ni mabilioni ya dola na hivyo kusababisha upotevu mkubwa wa rasilimali finyu zilizopo.
“Kwa mwaka 2010, Shirika la Afya Duniani lilikadiria kuwa jumla ya gharama zinazohusiana na kisukari zilifikia Dola bilioni 378 duniani kote na kiasi hicho cha fedha kinaweza kufikia Dola bilioni 490 ifikapo mwaka 2030, alisema.
Naye Mratibu kutoka Taasisi ya Kisukari hapa nchini, John Gadina, alisema utafiti uliofanyika mwaka 2012, ulionyesha kuwa asilimia tisa ya Watanzania waligundulika kuwa na kisukari huku Wilaya ya Temeke ikiongoza.
Alisema ugonjwa huo umewakumba vijana na watu wenye umri mkubwa na kwamba serikali mpaka sasa imefikia kutoa huduma hiyo kwa asilimia 75 ambapo kila palipo na hospitali panakuwa na kitengo cha kutoa huduma za ugonjwa huo.
Alisema sababu ya Wilaya ya Temeke kuwa na wagonjwa wengi imetokana na ulaji kwa wingi wa vyakula vya nazi, chapati, wali pasipo kufanya mazoezi.
JAMBOLEO
Serikali imekanusha taarifa zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii, kuwa kuanzia kesho na keshokutwa kutakuwa na uhaba wa mafuta kwenye vituo vya kuuza mafuta.
Kauli hiyo ya kukanusha imetolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Mwijage wakatia kijibu swali lililoulizwa na Job Ndugai jana Bungeni, Dodoma.
Ndugai alimtaka Waziri kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa ambazo zinasambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwamba kaunzia kesho kutakua na tatizo la upatikanaji wa mafuta na kusababisha shughuli nyingi kusimama.
Mwijage alisema taarifa ambazo wanazo kama Wizara ni kuwa hifadhi ya mafuta ipo ya kutosha na kuwa uhaba wa mafuta hauwezi kutokea kwa kuwa wana uhakika kuwa mafuta yapo ya kutosha.
Alisema hata yeye ameonakwenye mitandao ya kijamii na sasa wanafuatilia ili kujuab chanzo cha taarifa hizo ni nini.
lisema iwapo kuna msambazaji au mfanyabiashara atajaribu kufanya hivyo kanuni kanuni na sheria zilizopo zitatumika kuhakikisha wahusika wanawajibishwa.
HABARILEO
Walimu wawili wapya wa Shule ya Msingi Sang’ang’a kata ya Pemba tarafa ya Inchugu wilayani Tarime, mkoani Mara wanashikiliwa nchini Kenya kwa kosa la kuingia nchini humo bila kuwa na kibali.
Walimu hao wawili ambao ni Ahedius Orio kutoka mkoa wa Kilimanjaro na mwenzake Elias Nandi kutoka Lindi wanashikiliwa na polisi nchini Kenya walipokwenda nchini humo kwa matembezi.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Tarime/Rorya, Sweetbard Njewike alithibitisha kukamatwa kwa walimu hao wawili wapya wa shule ya msingi Sang’ang’a iliyopo umbali wa kilometa moja kutoka mpakani mwa Tanzania na Kenya.
Kamanda huyo alisema walimu hao katika kipindi hiki cha likizo, mwishoni mwa wiki waliamua kwenda kutembelea kijiji jirani cha Nyametaburo Kipimo ambacho kiko upande wa Kenya.
Alisema wakati wakiwa kijijini hapo walikutwa na Polisi wa nchi hiyo na kuwapeleka, kituo cha Polisi na Uhamiaji cha Isebania kuwahoji ambapo ilidaiwa waliingia nchini humo bila ya kufuata taratibu za kuwa na vibali vya kuingia nchini humo.
Tumewasiliana na wenzetu wa nchini Kenya ambapo wamedai kuwapeleka mahakamani kujibu shitaka la kuingia nchini humo bila vibali na wanatakiwa ndugu zao ama marafiki wakawadhamini huku juhudi za kuwasaidia walimu hao zinafanyika ili waweze kuachiliwa,Njewike.
Awali habari zilizotangazwa na vyombo vya habari vya Kenya, ikiwemo televisheni na redio za Citizen zilitangaza kuwa walimu hao walidaiwa kuwakusanya na kuwashawishi vijana wakiwemo kutoka Tanzania na Wakenya kujiunga na vikundi vya kigaidi vya al Shabaab.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

AMKA NA MAGAZETI NA TANGAKUMEKUCHABLOG

Magazeti yanaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha Elimu Cha Candle Education Centre Tanga. Kituo kinaongoza kufaulisha wanafunzi kidato cha pili hadi cha sita na wanaojiendeleza kielimu. Pia kituo kinatoa kozi ya Kiingereza na Computer na kutoa Cheti. Wapo Tanga mkabala na Bank ya CRDB simu 0715 772746
























Monday, June 29, 2015

POMBE KWA MAMA WAJAWAZITO , HATARI

Mama mjamzito akatumia pombe aliyoyapata  pamoja na mtoto atakayezaliwa…

Liquor
Wapo wanawake ambao ni wajawazito na wanatumia vilevi, Mbunge Kidawa Hamid Salehe akauliza swali kuhusu athari za vilevi kwa mtoto aliye tumboni.
Naibu Waziri Steven Kebwe akatoa haya majibu >>> “Dawa za kulevya na vileo vikali zina madhara kwenye mfumo wa mwili wa binadamu ikiwemo mtoto ambaye hajazaliwa… Madhara yanayoweza kujitokeza kwa motto ni pamoja na kupunguza ukuaji wa Ubongo, kuathirika kwa mfumo wa uzazi pamoja na kuzaa watoto wenye mtindio wa Ubongo, kuharibika kwa mimba sambamba na kuzaa watoto njiti…
Mtoto akizaliwa uwezo wa kujifunza unakuwa mdogo, anakuwa na tabia ya kutotulia mahali pamoja, kuwa na wasiwasi na msongo mkubwa wa mawazo nap engine motto akafia tumboni.
Kuna uwezekano pia mama akaambukizwa magonjwa ya zinaa, au kusababisha mtoto kuzaliwa na ngozi kama ya mzee”>>> Naibu Waziri wa Afya na ustawi wa jamii, Dk. Steven Kebwe.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

PETER CECH ATUA RASMI ARSENAL

Ujumbe wa kwanza aliopost Peter Cech baada ya kusajiliwa rasmi Arsenal

  Hatimaye golikipa Petr Cech ametambulishwa rasmi kuwa mchezaji wa Arsenal baada ya kocha Arsene Wenger kufanikiwa kukamilisha usajili wa malipo ya £10million Chelsea.
 Golikipa wa Czech Republic alifaulu vipimo vya afya siku ya Ijumaa asubuhi na Leo rasmi ametambulishwa kuwa mchezaji mpya wa Arsenal. 
Cech amesaini mkataba wa miaka minne na Arsenal, na atakuwa analipwa kiasi cha £100,000 kwa wiki, na anaweza kuanza kuichezea Arsenal vs Chelsea katika mchezo wa ngao ya hisani.
Muda mfupi baada ya kutambulishwa na Arsenal, Cech alitumia mtandao wa Twitter kuwaandikia ujumbe maalum kwa washabiki wa Chelsea na kuwaaga.

NKURUNZINZA AENDA KUPIGA KURU AKITUMIA BASKELI

Rais Nkurunziza alivyofika Kupiga kura kwenye Uchaguzi leo June 29 2015 Burundi.. (Pichaz)


Burundi
June 29 2015 Burundi wanafanya Uchaguzi Mkuu leo, lakini ishu ni kwamba Uchaguzi huo wa Wabunge unafanyika huku vyama vya Upinzani wakiwa wamesusia Uchaguzi huo.. kingine ni kwamba japo kumekuwa na machafuko ya muda mrefu kupinga Rais Piere Nkurunziza kugombea kwa mara ya tatu kwenye Uchaguzi huo lakini Ratiba inavyoonesha ni kwamba Uchaguzi wa Rais utafanyika mwezi July 2015.
Leo umefanyika Uchaguzi wa Wabunge, picha zilizoenea Mitandaoni zinamwonesha Rais Nkurunziza akiwa anaelekea kupiga kura akitumia usafiri wa baiskeli.
Piere II
Piere III
Piere

Burundi II
Pembeni ya vituo vya Kupigia kura walikuwepo Askari wakiwa na silaha kuhakikisha Usalama unakuwepo.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog