Monday, November 30, 2015

TUHUMA, MAHAKAMANI

Ripoti kutoka mahakamani Nigeria kuhusu kesi ya Mchungaji T B Joshua…

Mchungaji wa Kanisa la Church of All Nations Nigeria, TB Joshua na Wakandarasi wawili ambao wanakabiliwa na mashtaka ya uzembe uliopelekea jengo la Kanisa hilo kuanguka na kusababisha vifo vya watu 116, leo wameshindwa kufika Mahakamani kusikiliza kesi inayowakabili kuhusu vifo vya watu hao.
Kesi hiyo ilifunguliwa Mahakama Kuu ya Lagos Nigeria baada ya tukio la kuanguka kwa jengo la kufikia wageni lililopo kwenye Kanisa la TB Joshua September 12 2014 na kupelekea vifo hivyo ambapo kati ya waliofariki, 81 walikuwa raia wa Afrika Kusini.
Katika Mashtaka yaliyofunguliwa Mahakamani, Kanisa hilo limedaiwa kufanya ujenzi wa jengo hilo la ghorofa sita bila kuwa na kibali cha kufanya ujenzi huo.
Kwa upande wa TB Joshua wamekuwa wakijitetea kwamba sababu ya jengo hilo kuanguka inatokana na ndege moja ambayo ilizunguka juu ya jengo hilo, muda mfupi baadae jengo hilo likaanguka.. anaamini kuna hujuma zilizofanywa kwenye tukio hilo.
Kukosekana kwa T B Joshua na wakandarasi hao kumelalamikiwa pia kwamba ni kitendo cha makusudi na hakuna sababu yoyote ya msingi, japo mmoja wa wanachama wa Bodi ya kanisa hilo alikuwepo Mahakamani…
tb-joshua-church-collapse-e1410934119828
Jaji wa Kesi hiyo pia ameonekana kukerwa na kitendo hicho huku akisisitiza kwamba hatovumilia uzembe wa aina yoyote utakaofanya kuchelewa kusikilizwa kwa kesi hiyo.
Kesi hiyo imesogezwa mbele mpaka December 11 2015  ambapo TB Joshua na wakandarasi wake wawili wanatakiwa kuripoti Mahakamani hapo, Lagos Nigeria.

SAFISHA SAFISHA YA MAGUFULI YAUNGWA MKONO KILA KONA

Baada ya moto wa Magufuli kupita bandarini,

Ijumaa November 27 2015 Waziri Mkuu mpya wa Tanzania, Majaliwa Kassim Majaliwa alifanya ziara ya kushtukiza katika bandari ya Dar es Salaam na kuwasimamisha kazi maofisa watano wakihusishwa na ubadhirifu na kutowajibika.
mzungu
Muda mfupi baadae siku hiyohiyo, aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato TRA pia alisimamishwa kazi, lilikuwa ni agizo la Waziri Mkuu huyo kwamba yeyote aliyehusishwa na ubadhirifu akamatwe na uchunguzi uendelee juu yake.
IMAG1414
Nimeipokea Ripoti nyingine kutoka Jeshi la Polisi ambapo watu 12 wanashikiliwa mpaka sasa wakihusishwa na tuhuma za ubadhirifu bandarini Dar es Salaam.

KASI YA RAIS MAGUFULI , NI RAHA TU

Daraja juu ya Bahari Dar es salaam… Rais Magufuli alivyohakikishiwa ujenzi wake leo.

Vichwa vya habari za siasa Tanzania bado vinaendelea kubeba stori kila mara kuhusu Rais Magufuli… inawezekana ni kawaida kabisa kila siku kukutana na habari zaidi ya tatu au nne kuhusu Rais Magufuli tangu siku ya kwanza alipoapishwa na kuanza kazi ya Urais wa Tanzania.
MAGUFULI
Rais Magufuli akionesha ramani ya daraja la Salender, enzi hizo alikuwa Waziri wa Ujenzi.
Ninayo nyingine kutoka Ikulu sasahivi, hii inahusu Rais Magufuli kumuaga Balozi wa Korea Kusini, Chung IL ambapo Balozi huyo amemhakikishia Rais Magufuli kwamba daraja hilo litajengwa kwa ufadhili wa Serikali ya Korea Kusini.
IMG-20151130-WA0045
Daraja hilo litajengwa kuunganisha eneo la Coco Beach na Ocean Road ambapo litakuwa na urefu wa kilometa 6.3.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

KASI YA DR MAGUFULI GUMZO HADI CHINA

Tafsiri ya gazeti la China lililomuandika Rais John Pombe Magufuli.

Kuanzia wiki iliyopita zilianza kusambaa picha za gazeti lenye maandishi ya Kichina ambalo lilikua na picha ya Rais mpya wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli, nikaamua kuchukua time kumtafuta Mchina ili atupe tafsiri wameandika nini kuhusu Dr. Magufuli,

MAHAKAMA YAMUACHIA HURU SHEIKH ISSA PONDA

MAHAKAMA ya hakimu mkazi Morogoro imemuachia huru leo Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda aliyekuwa akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi baada ya mahakama kutoridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka na hivyo kuonekana hana hatia.

********
Historia ya kesi ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda.
Hati ya Mashitaka ya Kesi hiyo ilikuwa na jumla ya Mashitaka matatu  lakini Julai 22 mwaka 2015, Hakimu Mkazi Mary Moyo  alitoa  uamuzi wa kumfutia shitaka la kwanza kwasababu lilishatolewa uamuzi na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, na hivyo mahakama hiyo ya Morogoro siku hiyo ilitoa uamuzi wa kumuona ana kesi ya kujibu  katika mashitaka mawili yaliyosalia ambalo ni kosa la pili na la tatu .
Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro  ilimfungia dhamana Sheikh Ponda baada ya kukubaliana na hati ya aliyekuwa  Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), wakati huo Dk.Eliezer Feleshi ambaye kwasasa ni Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam liloomba Mahakama hiyo imfungie dhamana mshitakiwa huyo chini ya Kifungu cha 148(4) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya jinai ya Mwaka 2002.

Hatua hiyo ya kufunguliwa kesi katika Mkoa wa Morogoro ilikuja ikiwa ni muda mfupi baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, Agosti 19 Mwaka 2013 saa Tatu asubuhi,  kumfutia kesi ya jinai  Na.144/2013 katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano baada ya DPP kudai kuwa hana nia ya kuendelea kumshitaki katika kesi hiyo No.144/2013  kwa mujibu wa kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002.

Hata hivyo baada ya hakimu Liwa kumwachilia huru,Ponda ambaye aliletwa mahakamani hapo saa 12 asubuhi na wanausalama wa polisi na magereza chini ya ulinzi mkali, alikamatwa tena na kupakizwa kwenye magari ya wanausalama hao ambapo baadhi ya wanausalama hao waliliambia gazeti hili kuwa wanampeleka Ponda mkoani Morogoro kwaajili ya kufunguliwa makosa matatu ya uchochezi, kufanya mkusanyiko haramu na kisha akarejeshwa gereza la Segerea Dar es Salaam , lakini baadae Uongozi wa Jeshi la Magereza uliamua kumuamisha Ponda kutoka Gereza la Segerea na kumuamishia Katika Gereza Moja Mkoani Morogoro.
Sheikh Ponda alifikishwa mahakamani hapo akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi, baada ya kuwasili kwa helikopta ya Jeshi la Polisi katika uwanja wa gofu mjini Morogoro.
Akisoma mashitaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro, Richard Kabate, Mwanasheria Kiongozi  wa Serikali, Bernard Kongola, alidai  kuwa Agosti 10, mwaka 2013, katika eneo la Uwanja wa Ndege, Manispaa ya Morogoro, Ponda aliwaambia Waislamu wasikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za misikiti, kwa madai kuwa zimeundwa na BAKWATA, ambao ni vibaraka wa CCM na serikali.
Alidai kuwa Sheikh Ponda ambaye anatetewa  na wakili wa kujitegemea Juma Nassor aliwaagiza waumini hao kuwa endapo watu hao watajitokeza kwao na kujitabulisha kwamba ni kamati za ulinzi na usalama za misikiti, wafunge milango na madirisha wawapige.
Ilielezwa kuwa kauli hiyo ni kinyume cha agizo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliyotolewa na Hakimu Victoria Nongwa Mei 9, mwaka 2010, ambayo ilimtaka Ponda ndani ya mwaka mzima kuhubiri amani na Kuwa Raia Mwema.
Katika shitaka la pili, Kongola alidai kuwa Agosti 10, mwaka huu, katika eneo la Uwanja wa Ndege, Morogoro, Ponda aliwaambia Waislamu kuwa serikali ilipeleka jeshi Mtwara kushughulikia suala la vurugu iliyotokana na gesi ili kuwaua, kuwabaka na kuwatesa wananchi, kwa sababu asilimia 90 ya wakazi hao ni Waislamu.
Kwamba, Ponda aliwaambia wafuasi wake kuwa serikali haikufanya hivyo kwa wananchi wa Loliondo walipokataa Mwarabu asipatiwe kipande cha ardhi ya uwindaji baada ya kudai ni mali yao, kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wa huko ni Wakristu.
Shitaka la tatu ambalo linafafana na lile la pili, ambalo nalo linadaiwa kutendwa Agosti 10, mwaka huu, ambapo kauli ya Ponda inadaiwa kuumiza imani za watu wengine kinyume cha kifungu cha sheria namba 390 na kanuni ya adhabu namba 35 cha mwaka 2002.
Oktoba 18 mwaka 2012, Ponda na wenzie 49 walifikishwa Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa Mara ya kwanza   wakikabiliwa na makosa matano, kosa la kwanza ni la kula njama, kujimilikisha mali, kuingia kwa jinai katika kiwanja cha Chang'ombe  Markas,wizi wa malighafi zenye thamani ya Sh. Milioni 59 na kosa la uchochezi ambapo katika kesi hiyo Jamhuri ilikuwa ikiwakilishwa na wakili Mwandamizi wa Serikali , Tumaini Kweka .Mahakama pia iliwafunga dhamana ya Ponda na mshitakiwa wa pili tangu 0ktoba 18 Mwaka 2012 hadi siku Kesi hiyo iliyotolewa hukumu Mei 9 Mwaka 2013.
Mei 9 mwaka 2013 Hakimu Mkazi Victoria  Nongwa akitoa hukumu yake katika kesi hiyo ya Ponda na wenzake alisema anawaachiria huru washitakiwa 49  kwasababu upande wa jamhuri  umeshindwa kuthibitisha kesi dhidi yao na kwamba anamtia hatiani Ponda kwa kosa moja tu  la kuingia kwa jinai na kwamba na anamuachiria huru katika makosa manne yaliyosalia kwasababu pia jamhuri ilishindwa kuthibitisha mashitaka hayo dhidi ya Ponda.
Sheikh Ponda alikataa rufaa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kupinga hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Mei 9 mwaka 2013 ambapo alishinda rufaa yake.
Hata hivyo siku Chache baada ya Kufungwa Kifungo hicho cha nje Mei 9 mwaka 2013, Ponda alikwenda Mkoani Morogoro na kufanya mkutano ambao alidai wa Kutenda makosa ya jinai ambao alikamtwa  Agosti Mwaka 2013 na kuwekwa chini ya ulinzi na kufunguliwa Kesi Mahakama ya Kisutu Na.144/2013 ikafutwa na DPP na ndipo akafunguliwa kesi hiyo Mkoani Morogoro ambayo imetolewa hukumu Leo na kuachiwa huru.

CHANZO : OTHMANI MICHUZI

Sunday, November 29, 2015

SOMA MAGAZETI NA CANDLE EDUCATION CENTRE TANGA, 0715 772746

 

KIPINDUPINDU KITAONDOKA HALI KAMA HII TANGA?

 Takataka zikiwa zimerundikana na kuzagaa hadi kuziba njia barabara ya 16 Soko la Mlango wa Chuma Masiwani Tanga na kusababisha kero kwa wakazi wa eneo hilo na kutoa harufu kali kipindi hiki cha kuzuka ugonjwa wa kipindupindu .
Inadaiwa kuwa mawakala wa zabuni wanaoshughulikia usafi hususani katika masoko wamekuwa wakilaumiwa kwa kuacha takataka hadi kurundikana na kufikia kiwango cha kuziba barabara .
Hii imekuwa ikijitokeza mara kwa mara katika masoko na kufanya madampo hali ambayo inatishia kuzuka kwa magonjwa ya Kipindupindu na mengineyo. 
Wanaharakati Tanga wameiambia Tangakumekuchablog kuwa kuna uzembe na kutofuatilia na hivyo kushauri hatua madhubuti kutekelezwa.





NAYO REAL MADRID YAONA MWEZI

Real Madrid wafuta machungu ya El Clasico kwa kuifunga Eibar, haya ndio matokeo kamili

Baada ya Jumamosi ya November 28 klabu ya FC Barcelona kushuka dimbani kucheza mchezo wake 13 dhidi ya Real Sociedad na kuibuka na ushindi wa goli 4-0, November 29 ilikuwa zamu ya wapinzani wao wa jadi klabu ya Real Madrid ya Hispania ambao wao walilazimika kusafiri hadi dimba la Municipal de Ipurúa kucheza na klabu ya Eibar.
takashi-inui-eibar-toni-kroos-real-madrid
Real Madrid ambayo ilikuwa ugenini na wachezaji wake nyota kama Cristiano Ronaldo na Gareth Bale ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya wenyeji wao klabu ya Eibar, licha ya kuwa Real Madrid hawana kumbukukumbu nzuri katika mchezo wao wa El Clasico uliyochezwa weekend iliyopita ilifanikiwa kuiondoka na point 3 na kufanya tofauti yake na FC Barcelona kuwa ya point 6.
2EE80D3700000578-0-image-a-68_1448815339773
Hata hivyo ushindi walioupata Real Madrid haukuwa mwepesi kwani klabu ya Eibar ilikuwa imefanikiwa kuwadhibiti Real Madrid hadi dakika ya 43 ndio Gareth Bale akafanikiwa kufunga goli la kwanza, goli la pili la Real Madrid lilifungwa kwa mkwaju wa penati na nyota wa kimataifa wa Ureno anayekipiga katika klabu hiyo Cristiano Ronaldo dakika ya 82.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapoa tangakumekuchablog

CHALSEA BADO HAKUJATULIA, YALAZIMISHWA DROO NA TOTTENHAM



TOTTENHAM XI (4-2-3-1): 
Lloris 6.5; Walker 6, Alderweireld 6.5, Vertonghen 6, Rose 7; Mason 6 (Lamela 55, 6.5), Dier 6.5, Dembele 6.5, Son 6.5 (Njie 73, 6); Eriksen 6.5; Kane 6.
Booked: Rose, Kane, Walker, Vertonghen.
Manager: Mauricio Pochettino 6
Subs not used: Vorm, Trippier, Onomah, Wimmer, Carroll.

CHELSEA XI 
(4-2-3-1): Begovic 6.5; Ivanovic 6, Zouma 7.5, Cahill 7, Azpilicueta 6; Fabregas 6.5, Matic 7; Willian 6 (Kennedy 88), Oscar 6.5, Pedro 6 (Loftus-Cheek - 91); Hazard 6.5.
Booked: Matic, Azpilicueta
Manager: Jose Mourinho 6.5
Subs not used: Amelia, Rahman, Mikel, Djilobodji, Kenedy, Costa
Stadium: White Hart Lane
Attendance: 35639
MOM: Zouma 
Referee: Michael Oliver 7.









NGUMI ULINGONI