Friday, September 30, 2016

WENGER AWAFAGILIA WACHEZAJI KUTOKA AFRIKA

Wenger: Wachezaji wa Afrika wamenifaa sana katika soka

Arsene Wenger ameongoza Arsenal kwa miaka 20
Nwankwo Kanu wa Nigeria alikuwa mmoja wa wachezaji waliokuwa wenye umuhimu mkubwa kwa ArseneMeneja wa Arsenal Arsene Wenger ameiambia BBC kuwa wachezaji kutoka nchi za Afrika wamekuwa wenye umuhimu mkubwa katika taaluma yake ya miaka 20.
Wenga alikuwa akizungumza wakati wa mkutano wake wa kawaida na waandishi wa habari kabla ya mechi ambapo pia alitunukiwa kwa kukiongoza klabu hicho kwa miongo mwili.
Akiwa mwenye uso uliotabasamu, Wenger amesena kuwa wachezaji kutoa Afrika wana moyo, wenye ubunifu na nguvu, masuala ambayo ni vigumu kuyapa kwenye mchezo.
Aliwataja wachezaji akiwemo Nwanko Kanu wa Nigeria, Kolo Toure wa Ivory Coast na gwiji raia wa Liberia George Weah, ambaye alikuwa meneja wake katika klabu ya Monaco nchini Ufaransa, kama wachezaji watatu waliokuwa na ushawishi mkubwa katika taaluma yake.

CHINA NA TEKONOLOJIA ZAKE, YAJENGA CHOO KWA VIOO

Vyoo vilivyojengwa kwa vioo vyazinduliwa nchini China

Mwanamume chooni Changsha, China, 29 Septemba 2016.Changsha, China, 29 Septemba 2016.Tianmen Mountain (1 Aug 2016)China imezidisha matumizi yake ya vioo kuunda vivutio vya kitalii kwa kujenga choo cha vioo ambacho mtu anaweza akaona nje na hata ndani.
Vyoo hivyo, vimejengwa karibu na Ziwa Shiyan, katika mkoa wa Hunan kusini mwa nchi hiyo.
Vioo hivyo vinawezesha wanaovitumia vyoo hivyo kutazama mandhari ya kuvutia ya msitu au wengine wanaotumia vyoo jirani.
Aidha, walio nje wanaweza kuona walio ndani ya vyoo
Kuta za vyoo hivyo, hata zile zinazotenganisha vyoo vya wanawake na wanaume, ni za vioo kabisa ingawa vioo hivyo vimetiwa ukungu kiasi.
Vyombo vya habari nchini humo vinasema ni watu wachache sana waliotumia vyoo hivyo siku ya kuzinduliwa kwake.

AIBA MASHUKA ALA KIBANO CHA MWAKA


Kijana anaedhaniwa kuwa kibaka alieshukiwa kuiba mashuka katika nyumba moja mtaa wa Chumbageni Tanga akipokea kibano kutoka kwa wakazi wa eneo hilo kisha kupelekwa kituo kikuu cha  Chumabageni


Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

AMKA NA MAGAZETI NA FREYS COACH TANGA, MOSHI, ARUSHA , BABATI HADI SINGIDA



Magazetini leo Jumamosi,Oktoba 1,2016..Yapo ya udaku,michezo,hard news ndani na nje ya Tanzania











TANZANIA


















Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

KITUNGUU SAUMU NA FAIDA YAKE

Tibu Ugonjwa wa Shinikizo la Damu Na Magonjwa Mengine Kwa Kitunguu Swaumu

Kitunguu swaumu (Garlic) mpaka sasa kimeripotiwa kuwa na matumizi 125 ya kitabibu kwa binadamu. Matumizi yafuatayo ya kitunguu swaumu ndio yamefanyiwa utafiti wa kitalaamu wa kitabibu:

Kupunguza tatizo la damu kuganda katika mishipa ya damu (reduce blood clotting) na ugonjwa wa shinikizo la damu (blood pressure): tafuna punje ya kitunguu swaumu kila mara au tumia unga wa kitunguu swaumu kwa kuweka kiasi kwenye maji ya moto au chai na kunywa.

Kuzuia Saratani ya Tumbo (Stomach cancer): Kula mara kwa mara kitunguu swaumu husaidia kuepusha kupatwa na saratani ya tumbo.

Kinga ya Mwili (Immune system): Ulaji wa kitunguu swaumu husisimua utendaji kazi wa macrophages utendaji kazi wa T cells.

Husaidia kukakamaa kwa mishipa ya damu ya Arteries (Atherosclerosis), kupunguza cholesterol (blood lipids) na tatizo la mzunguko wa damu mwilini (peripheral vascular disease): Tumia mafuta ya kitunguu swaumu au tafuna punje za kitunguu swaumu mara kwa mara.

Kutibu Minyoo aina ya Threadworms: Saga punje kadhaa na weka kwenye glasi ya maziwa ya vuguvugu/moto na kunywa asubuhi kabla hujala chakula chochote.

Miguu kufa ganzi (Leg numbness) na Sciatica pain relief: Saga punje kadhaa za kitunguu swaumu au chukua kisi kidogo cha mafuta ya kitunguu swaumu weka kwenye glasi ya maziwa moto. Kunywa mara 1 - 3 kwa siku hadi utakapopata nafuu.

MAADHIMISHO SIKU YA BAHARI DUNIANI



 Waziri wa Viwanda na Biashara wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Amina Salim Ali, akikagua banda la maonyesho la Idara ya Marini na kupata maelezo kutoka kwa Ayoub Mdikang’andu wa kitengo cha Marini wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Bahari Duniani yaliyofanyika Tangamano Tanga Leo.




 Waziri wa Viwanda na Biashara wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Amina Salim Ali, akikagua moja ya mabanda ya maonyesho kitengo cha Zimamoto na Usalama Mamlaka ya Bandari Tanga (TPA) na kupewa maelekezo na Othman Mkumbawakati wa kilele cha maadhimisho ya Bahari Duniani na kufanyika uwanja wa Tangamano Tanga  leo.


Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

WATOTO KUPIMWA MOYO TUMBONI

Watoto kupimwa moyo tumboni

KUTOKANA na idadi kubwa ya watoto wanaozaliwa na magonjwa ya moyo, wajawazito sasa watapimwa kuangalia mtoto aliye tumboni kama ameathirika na magonjwa hayo.

Uchunguzi wa magonjwa hayo ambao utaendeshwa na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), utahusisha ujawazito wa kuanzia wiki 18 na kuendelea.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa JKCI, Maulid Kikondo alisema uchunguzi huo utafanyika bure hospitalini hapo kwa siku tatu kuanzia Oktoba 12 hadi 14, mwaka huu.

“Tumegundua watoto wengi wanazaliwa na magonjwa ya moyo lakini upo utaalamu ambao wenzetu wamekuwa wakiutumia wa kupima ujauzito ukiwa na wiki 18 na kuendelea huweza kubaini mapema iwapo mtoto aliyeko tumboni ana matatizo au la.

“Mwenzetu Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kwa Watoto, Naiz Majani alikwenda nje ya nchi na akapata mafunzo, amerudi hivyo tutaanza kuwachunguza wajawazito,” alisema.

Alisema uchunguzi huo utafanywa kwa kutumia kifaa maalumu kiitwacho Fetal Echo-cardiology .

Kikondo alisema hawajaweka idadi maalumu ya wajawazito wanaotarajia kuwapima kwa kutumia kifaa hicho na amewataka wafike kwa muda uliopangwa.

“Kila atakayekuja atahudumiwa, mtoto anapogundulika kuwa na tatizo ni rahisi kutibiwa punde tu anapozaliwa na kuwa na afya njema akafurahia maisha kuliko akizaliwa na baadaye kugundulika kwa vile  matibabu yake yanachukua muda ikizingatiwa wengi huletwa wakiwa wamechelewa,” alisema.

Kikondo alisema pamoja na hilo, Oktoba 9 hadi 16, mwaka huu wataendesha kambi nyingine ya upasuaji kwa watoto 30 wenye magonjwa hayo.

“Madaktari wa JKCI watafanya upasuaji huo kwa kushirikiana na madaktari wenzao kutoka Addis Ababa wa hospitali ya Al muntada,” alisema.
MGBLOG

Thursday, September 29, 2016

CHAVITA WAMUOMBA RAIS MAGUFULI KUWEKA WATAALAMU WA LUGHA ZA ALAMA KWENYE LUNINGA



Tangakumekuchablog
Tanga, CHAMA Cha Viziwi Tanzania (Chavita) Kimeikumbusha Serikali kuwawekea wakalimani wa lugha za alama katika Televisheni ili kuweza kupata habari za Bunge na za kitaifa na Kimataifa na kuacha kusimuliwa.
Akizungumza katika Kongamano la Wajasiriamali Viziwi kuhusiana na kujiunga na Mifuko ya Bima, Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa , Nibros Mlawa, amesema walemavu wa kusikia wamekuwa wahanga wa kukosa habari kwa  muda mrefu.
Ameliomba Bunge kupitisha sheria ya kila Televisheni kuweka mkalimani wa lugha za alama jambo ambalo litasaidia kupata na kujua matukio yanayojiri na kuepukana na kupata habari za kusimuliwa ambazo nyengine hazina ukweli.
Akikumbushia walemavu kujiunga na mifuko ya jamii, Mlawa amesema walemavu wako tayari kujiunga na mifuko hiyo lakini kwanza kuboresha miundombinu ya kuyafikia matibabu ikiwemo kuweka ngazi maalumu kwa walemavu na barabara.




Mwenyekiti wa Chama Cha Viziwi Tanzania (Chavita), Nibros Mlawa, akizungumza na waandishi wa habari Tanga jana mara baada ya kufungua warsha ya wajasiriamali viziwi kupata elimu ya kujiunga na mifuko ya Bima ya Afya , kulia ni mkalimani kutoka kituo cha watoto wenye ulemavu (YDPC) Prisca Mwakasendile.


 Afisa Jinsia na Maendeleo Makao Makuu ya Chama Cha Viziwi Tanzania (Chavita), Lupi Mwaisaka, akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ufunguzi wa warsha ya Wajasiriamali Viziwi kupata elimu ya kujiunga na Bima ya Afya , kulia ni mkalimani wa kituo cha watoto walemavu (YDPC), Prisca Mwakasendile.
Kwa habari , matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog