Thursday, June 30, 2016

AJUZA KUJIPANDIKIZA MAYAI ILI AZAE

Mwanamke ashinda kesi kujidunga mayai ya uzazi.

Mwanamke ambaye anataka kutumia mayai ya uzazi ya bintinye ili kumzaa mjukuu wake ameshinda kesi mahakanani na kuruhusiwa kufanya hivyo.
Mwanamke huyo wa umri wa miaka 60 alikuwa amekatazwa kupeleka mayai ya bintiye kwenye kliniki moja nchini Marekani hali iliyosababisha akate rufaa.
Bintiye ambaye aliaga dunia mwaka 2011, anaripotiwa kumuambia mamake amzalie watoto wake. Lakini mamake alishindwa katika kesi mwaka uliopita.
Hata hiyo aliruhusiwa kupinga hukumu hiyo katika mahakama ya rufaa mjini London mbele ya jopo la majaji watatu.
Mwaka 2014 halmashauri inayohusika na mayai ya uzazi, ilisema kuwa mayai hayo hayangetolewa mjini London, kwa sababu bintiye hakuwa ametoa idhini kamili kabla ya kifo chake akiwa na umri wa miaka 28.
Lakini kwenye kesi ya sasa mawakili waliawaambia majaji kuwa, mwanamke huyo alikuwa anataka kutimiza matakwa ya bintiye ya kuzaa mtoto akitumia mayai yake na kisha amlee mtoto huyo.
BBC

AMKA NA MAGAZETI NA NEW AGE EDUCATION CENTRE TANGA, 0717 713866

Magazeti yanaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya Kituo cha Elimu Cha New Age Education Centre Tanga, New Age ni mabingwa wa kufaulisha wanafunzi kidato cha pili hadi cha sita na waojiendeleleza kielimu Maofisini, New Age wanatoa kozi mbalimbali za Kielimu kwa muda mrefu na Mfupi, New Age wapo Tanga mkabala na TANESCO simu 0717 713866




















TANZANIA



KENYA

UGANDA














Kila siku asubuhi na mapema tangakumekuchablog inakupa kurasa mwanzo mwisho ya magazeti nchini na Uingereza.

TUNDU LISSU APANDISHWA KIZIMBANI

MBUNGE TUNDU LISSU APANDISHWA KIZIMBANI MCHANA HUU.

  Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Tundu Lissu akifika  katika mahakama ya hakimu mkazi ya Kisutu jijini Dar es Salaam mchana huu. Ikiwa jana Mbunge huyo alihojiwa na Jeshi la Polisi katika kituo cha Polisi cha Kanda maalumu ya Dar es Salaam na kutupwa Rumande mara baada ya kukosa dhamana.


  Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Tundu Lissu apandishwa kizimbani mchana huu  katika mahakama ya hakimu mkazi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo.‪

  Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Tundu Lissu akionesha alama ya chama cha Democrasia na Maendeleo akiwa ndani ya Mahakama  ya hakimu mkazi ya Kisutu jijini Dar es Salaam muda huu.‪

SHEREHE TAMTA DAY ZAFANA TANGA



Wanafunzi wa Chuo Cha Tamta  cha Tanga wakiandamana kusherehekea Maulid ambayo husherehekea kila mwaka chuoni hapo maarufu kama Tamta Day.
Kila mwaka Chuo hicho hufanya Maulidi na kuwakutanisha wanafunzi na walimu kutoka Mikoa mbalimbali  ndani na nje ya nchi.









N i furaha tu kila kona ya jiji la Tanga shamrashamra zikipamba moto

GAZETI AUSTRALIA LABASHIRI MSHINDI WA UCHAGUZI

Mamba anayebashiri matokeo ya uchaguzi Australia

Gazeti moja nchini Australia limedai kwamba kuna mamba anayeweza kubashiri matokeo ya uchaguzi nchini Australia.
Gazeti hilo la Northern Territory News ni maarufu kwa habari zake katika ukurasa wake wa kwanza.
Huku raia wakisubiri uchaguzi wa siku ya Jumamosi ,gazeti hilo liliweka picha za wagombea wawili wakuu wa uchaguzi huo katika ndoana ya samaki na kumrushia mamba anayeitwa Burt mwenye urefu wa mita 5.1.
Burt alionekana kuifuata picha ya kiongozi wa upinzani Bill Shorten ,lakini baada ya mda akaamua kuitia mdomoni ndoana ya picha ya waziri mkuu Malcolm Turnbull,ikiwa ishara inayoonyesha kwamba ataibuka mshindi katika uchaguzi huo.
''Wanaobashiri tayari wamesema kuwa waziri huyo ataibuka mshindi'', alisema muhariri wa gazeti hilo Matt Williams.
Ubongo wa mamba huyo ni mdogo sana lakini ni miongoni mwa wanyama werevu sana.
Mamba huyo huishi katika mbuga ya wanyama pori ya Crocosaurus Cove na alishiriki katika katika filamu ya Australia Crocodile.
Ni mnyama wa hivi karibuni aliyebainika kuwa mwerevu huku yule maarufu akiwa Pweza Paul,ambaye alifanikiwa kubashiri matokeo ya mechi saba katika kombe la dunia la mwaka 2010 nchini Ujerumani.

PROFESA WA IVORY COAST APATA SIFA BAADA YA KUBEBA MTOTO MGONGONI

Profesa aliyebeba mtoto mgongoni apata sifa

h
Profesa mmoja wa chuo kikuu amesifiwa pakubwa nchini Ivory Coast kwa kumbeba mtoto wa mmoja wa wanafunzi wake mgongoni wakati wa masomo.
Picha za Honore Kahi wa chuo cha Bouake, zimesambaa pakubwa kwenye mitandao ya kijamii.
Alisema aliamua kumsaidia mwanamke katika darasa lake wakati mtoto alianza kulia.
Picha zilizochukuliwa na mwanafunzi mwingine zinamuonyesha, bwana Kahi akifunza huku mtoto akiwa mgongoni.
BBC

SIAFU WAUA HARUSI

Siafu waua bwana harusi

siafu



WAKAZI  wa Kijiji  cha  Nditu,  Kata  ya Suma, Wilaya ya Rungwe  mkoani Mbeya, wamegoma  kuzika mwili wa marehemu Shabani  Yusufu (27),  baada kushambuliwa na kundi la  siafu nyumbani kwake  na kusababisha apoteze uhai.

Yusufu, amefariki dunia ikiwa ni siku moja tu baada ya kufunga ndoa na kuzua gumzo kubwa kijijini hapo.

Alikutwa na mauti hayo akiwa amejipumzisha ndani usiku wa kuamkia jana, jambo ambalo linahusishwa na imani za kishirikina.

Akisimulia mkasa huo, baba mzazi wa marehemu, Ebron Mwaipaja, alisema mwanawe  alitoka kufunga ndoa  juzi na alikutwa na mauti hayo akiwa amejipumzisha chini ya mti nyumbani kwake, ambako ghafla alivamiwa na siafu.

Alisema kulikuwa na maneno ya hapa na pale wakati wa maandalizi ya harusi hiyo kutoka kwa baadhi ya watu, ambayo yamesababisha tukio hilo kuhusishwa na imani za kishirikina.

Baba huyo alisema baada ya tukio hilo, wananchi na uongozi wa Serikali ya kijiji walifika eneo hilo, huku wakimtaja mmoja wa wanakijiji kuwa ndiye “aliyetuma” siafu hao.

“Wananchi waligoma kuandaa taratibu za mazishi wakishinikiza aletwe mganga wa jadi apige ramli ili kumbaini mtu anayeendesha matukio ya ushirikina yanayoendelea kijijini hapa,” alisema.

Alisema baada ya wananchi kugoma kuzika, Serikali ya kijiji nayo iligoma kutoa kibali, ikisema siku zote Serikali haiamini uchawi, jambo ambalo lilisababisha wananchi waliokujwa na silaha za jadi, kufanya maandamano na kufunga barabara.

Baada ya hali ya usalama kuzidi kuwa mbaya, polisi walifika eneo la tukio na kutuliza ghasia, huku familia ikifanya maandlizi ya maziko bila wanakijiji kuhusika.

“Kijana wangu ndiyo kwanza alitoka kufunga ndoa akifurahia maisha ya kuwa na mke, amekutwa na umauti tena kwa kuvamiwa na siafu wakati kijiji hiki hakijawahi kuwa na wadudu hawa, yote namwachia Mungu,” alisema Mwaipaja.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wenzake, Joseph Kajura, alisema wanafahamu fika tukio hilo ni la kishirikina na ndiyo maana walimtafuta mganga wa kienyeji ili apige ramli kwa ajili ya kubaini mhusika.
MG

Wednesday, June 29, 2016

HADITHI, MWANAMKE SEHEMU YA 31

SIMULIZI ZA FAKI A FAKI 0713 340572

MWANAMKE 31

ILIPOISHIA

Niliposikia hivyo moyo wangu ulishituka. Kama namba za pikipiki yangu nazo zimeonekana nimekwisha!

Sikujua kama ile maiti ilikuwa ni ya shemeji yake mhasibu wetu. Nikaona nimejiingiza katika matatizo mengine ambayo sikuyatarajia.

“Hivi sasa nimeitwa polisi nikatoe maelezo, ile maiti imepelekwa hospitali kufanyiwa uchunguzi kujua kama ilibakwa. Kuna watu wanabaka maiti” Mhasibu aliendelea kutueleza.

“Inawezekana. Ni vizuri kama amepelekwa hospitali kufanyiwa uchunguzi. Binaadamu hivi sasa hawaaminiki kabisa” nikajidai kusema ili nisionekane nimefadhaika.

“Kumbe yule mlinzi alikwenda kuripoti polisi” Mwenzetu mwingine akauliza.

“Alikwenda polisi asubuhi. Ndio maana ninaitwa polisi” Mhasibu akamjibu kisha akatuaga na kuondoka.

Niliwaza kwamba kama mlinzi alikwenda kuripoti polisi, ile leseni yangu pia aliipeleka baada ya kuiokota pale ilipoanguka. Polisi watakuwa wameshaiona picha yangu. Bila shaka mhasibu wetu ameitwa ili kuoneshwa ile leseni ili athibitishe kama ndiye mimi.

Sasa sijui nikimbie kuepusha aibu, au niwangoje polisi waje wanikamate hapa hapa?

Kwa kweli nilikuwa nimechanganyikiwa.

SASA ENDELEA

Kwa dakika kadhaa sikuweza kujua nifanye nini. Wafanyakazi wenzangu walikuwa wakilizungumzia lile tukio la kufukuliwa kaburi, mimi nilikuwa kimya. Moyo wangu ulikuwa ukihangaika. Lakini hakukuwa na yeyote aliyeweza kunigundua.

Wasiwasi uliponizidi nilitoka nje ya duka letu. Kilichonitoa ni ule wasiwasi kwamba polisi wakitokea niweze kuwaona mapema. Nilikuwa nimeshapanga kuwakimbia.

Ilikuwa bora kupotea kuliko kupatwa na fedheha kama ile mbele ya wafanyakazi wenzangu.

Nilisimama nje ya duka letu kwa karibu nusu saa, nilipoona hakukuwa na polisi wowote waliokuwa wanakuja nikarudi ndani. Baadaye nikatoka tena. Nikaangalia pande zote za barabara kisha nikarudi.

Wakati nimekaa nikiendelea na mawazo yangu nilishituka nilipomuona mhasibu akiingia. Nilijua kuwa alikuwa amefuatana na polisi waliokuja kunikamata.

Lakini sikuona polisi. Alikuwa peke yake. Nikamkodolea macho ya tashiwishi. Nilikuwa na hisia kwamba alikuwa ameoneshwa leseni yangu na kunitambua.

Mfanyakazi mwenzetu mmoja akamuuliza kilichotokea huko polisi alikokwenda.

“Nimekwenda kutoa maelezo yangu” akasema na kuongeza.

“Ule mwili bado uko hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi”

“Huyo mtu aliyefukua hilo kaburi hakufahamika?’ nikauliza ili kuondoa dukuduku nililokuwa nalo.

“Si rahisi kufahamika. Mtu mwenyewe alikimbia na pikipiki” Mhasibu akanijibu.

Hapo wasiwasi ukanipungua kidogo.

Baada ya mhasibu kuzungumza na sisi kwa dakika chache akaingia ofisini kwake.

Haukupita muda mrefu, simu tuliyokuwa tunaitumia ikaita. Ilikuwa inapokelewa na mtu yeyote aliye karibu nayo. Akaipokea mfanyakazi mmoja akasikiliza kisha akaniita.

“Amour ni simu yako”

Moyo ukanipasuka.

Ni nani tena?

Nikaenda na kukipokea chombo cha kuzungumzia. Nikakiweka sikioni na kusema.

“Hello!”

“Naongea na bwana Amour?” Sauti nzito tena inayokwaruza ikauliza kutoka simu ya upande wa pili.

Moyoni mwangu nilikuwa nikijiuliza ni nani mwenye sauti hii? Akilini mwangu sikuweza kukumbuka mtu yeyote ninayemfahamu mwenye sauti inayolingana na ile.

Nikashuku kwamba anaweza kuwa afisa wa polisi ananipigia kuniita kituo cha olisi.

“Ndio. Wewe nani?”

“Hebu njoo hapa Tropicana, utanijua tu”

Tropicana ulikuwa mkahawa uliokuwa mtaa wa pili ambao wafanyakai wengi hupenda kunywa chai wakati wa saa nne na hata kula chakula cha mchana.

“Ni vizuri unifahamishe wewe nani?”

“Usiwe na wasiwasi. Ukifika hapa utaniona na utanijua”

Nikaurudisha mkono wa simu kisha nikatoka. Niliwaaga wenzangu kuwa ninakwenda kunywa chai.

Nilipotoka nje ya duka letu nilizunguka mtaa wa pili ambako kulikuwa na huo mkahawa wa Tropicana. Wakati natembea nilikuwa nikiwaza huyo mtu aliyeniita atakuwa nani kama si afisa wa polisi.

Nilikuwa na hakika kwamba sikuwa nikifahamiana na mtu aliyekuwa na sauti kavu kama ile.

Nilipofika kwenye mkahawa huo nikaingia. Nilisita kidogo kando ya mlango nikawatupia macho watu waliokuwamo ndani. Nikaona mtu mmoja aliyekuwa amekaa katika meza ya pembeni akinipungia mkono kuniita.

Sikuweza kumfahamu mpaka nilipofika karibu yake.

“Ah Mgosingwa!” nikasema mara tu sura yake iliponijia akilini mwangu.

Alikuwa mlinzi wetu ambaye alifukuzwa kazi kwa tabia yake ya ulevi wa kupita kiasi. Tulikuwa tunamuita Mgosingwa, neno la kabila la kizigua linalotokana na neno mgosi, yaani mwanamme.

Kwa vile yeye mwenyewe alikuwa mzigua, alikuwa akimuita kila mtu “mgosingwa” hasa pale anapotaka kumkopa mtu pesa ya kwenda kulewea. Na sisi tukampa jina hilo la mgosingwa. Nilizoea kumuita hivyo na jina lake halisi nilikuwa silijui.

“Vipi Mgosingwa?” akaniambia huku akinipa mkono kunisalimia.

“Salama tu Mgosingwa. Wewe ndio uliyenipigia simu kuniita?’

“Ndiye mimi Mgosingwa. Karibu ukae”

Nikakaa kwenye kiti.

“Ulikuwa unasemaje Mgosingwa?” nikamuuliza nikiwa na shauku ya kutaka kujua alichoniitia.

“Mgosingwa unatakiwa polisi!”

Kusema kweli nilishituka aliponiambia hivyo. Moyo wangu ukawa unadunda pu!pu!pu!

Nikajidai natabasamu.

“Nimefanya kosa gani Mgosingwa?”

Mgosingwa alitia mkono kwenye mfuko wa shati lake akatoa ganda kama la kitambulisho akaniwekea mezani.

“hii si leseni yako Mgosingwa?’ akaniuliza.

Nikalichukua lile ganda na kulifungua. Naam. Ilikuwa ni leseni yangu niliyokuwa nimeitupa kule makaburini. Pale pale uso wangu ulibadilika rangi kwa hofu iliyochanganyika na fadhaa. Nikamtazama mgosingwa huku nikijiuliza ameipata wapi leseni yangu.

“Huku nikiendelea na tabasamu langu la kulazimisha nilimuuliza.

“Mgosingwa umeipata wapi hii leseni yangu?’

“Si nimekwambia unatakiwa polisi?”

Jibu lake hilo lilizidi kunichanganya na kunifadhaisha. Midomo yangu niliyokuwa ninailazimisha kutabasamu huku nikiwa na fadhaa ilianza kutatizika na kutetemeka. Sasa haikuweza tena kutabasamu.

“Mgosingwa unanichanganya. Sasa nani kakupa hii leseni na kakupa kwa madhumuni gani?” nikamuuliza huku nikiizuia modomo yangu isitetemeke wakati nikimuuliza hivyo.

Mgosingwa aligundua kuwa nilikuwa nimetaharuki. Akacheka. Hata hivyo kwa vile uso wake ulikuwa umekunjana kutokana na kuendeleza kilevi, kicheko chake hakikuufanya uso wake upendeze, bali ulionekana kama anataka kulia.

“Mgosingwa hukumbuki uliiacha wapi leseni yako?” akaniuliza.

Nikatikisa kichwa.

“Sikumbuki” Nilimjibu hivyo ili nijue ataniambia nini.

“Mgosingwa jana usiku si ulikuja kule makaburi ukafukua lile kaburi nikakukurupusha”

JE NINI KITATOKEA? TUKUTANE KESHO PANAPO MAJALIWA

AMKA NA MAGAZETI YA TANZANIA NA UINGEREZA NA NEW AGE EDUCATION CENTRE 0717 713866

Magazeti yanaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha Elimu Cha New Age EDUCATION Centre Tanga, New Age ni mabingwa wakufaulisha wanafunzi kidato cha pili hadi cha sita na wanaojiendeleza kielimu, New Age wako na walimu mahiri na majengo ya kuvutia, New Age wapo Tanga mkabala na TANESCO simu 0717 713866











TANZANIA