Wednesday, September 30, 2015

ULIMI WA KIATU WAKWAMISHA NDOTO YAKE MASHINDANO YA MARATHON , BERLIN

Pale ambapo viatu vimesababisha Mwanariadha wa Kenya ashindwe kuvunja Rekodi ya Dunia..

Eliud Kipchoge ni Mwanariadha aliyewakilisha Kenya kwenye Mashindano ya Riadha ya Berlin Marathon ambayo yamefanyika Berlin Ujerumani… Round ya kwanza haikuwa na neema kwake, ulimi wa ndani ya viatu ulitoka na kusababisha jamaa ashindwe kuivunja Rekodi ya Dunia kwenye Mashindano hayo.,
Unaweza kuchukulia ni kitu cha kawaida, lakini Eliud anasema mpaka anamaliza mbio alikuwa na malengelenge miguuni pamoja na kidole gumba kupata jeraha na kutokwa damu nyingi, hiyo ilifanya amalize round zote za Riadha akiwa na wakati mgumu sana !!
A_Nike_runner_missed_a-0393ac16366df7c6748c4ae43dd0b500
Haikuwa siku nzuri mimi kutumia hivi viatu, nilivijaribu nikiwa Kenya na vilikuwa sawa tu!! Lengo langu ilikuwa nivunje Rekodi ya Dunia leo lakini naona haikuwa siku yangu– Eliud Kipchoge.
Mbali ya changamoto zote, Eliud aliibuka na ushindi kwenye mbio za Maili kumi huku akiweka Rekodi ya kumaliza mbio kwa saa mbili na dakika nne.
Unaweza kucheki kwenye hii video ya sekunde 76 mbio zenyewe ilivyokuwa mpaka mwisho…

Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

MTOTO WA WIKI 5 ASINDWA MASHINDANO YA UREMBO, UINGEREZA

Kutana na mtoto wa wiki 5 tu lakini kavunja rekodi kwenye mashindano ya Urembo..Pichaz


Imezoeleka wanaoshiriki mambo ya urembo ni mabinti  ambao tayari wanajitambua na wenye uwezo wa kujibu maswali pale wanapokuwa wakihojiwa.
Hii imekuwa tofauti kwa Matilda Mackie mtoto aliyeshiriki mashindano hayo akiwa na wiki 5 tu tangu azaliwe huko Uingereza.
Mama wa mtoto huyo Jennifer alipeleka jina la mtoto wake kwa majaji wa shindano hilo la Kitaifa la urembo lililofanyika Glasgow mwezi uliopita na mwanaye kufanikiwa kuhika nafasi ya pili.
Mama huyo amesema nia ya kumshirikisha mwanaye huyo kwenye mashindano makubwa kama hayo ni kuweza kumshinda rafiki yake pamoja na kutimiza ndoto baada ya watoto wake wawili kufanya vizuri.
Amesema anajiona ni mama mwenye bahati kubwa baada ya watoto wake wengine Alexis na Maclan Mackie nao kufanikiwa kushiriki mashindano hayo na kufanya vizuri.

pegant

pgnt2
Matilda Mackie akiwa na mama yake Jennifer

ale
Alexis Mackie

lach
Lachlan Mackie baada ya kushinda

pgnt3
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

VIMBWANGA VYA WALIMWENGU

Bibie hakutaka utani, kaamua kutumia Bango kubwa barabarani kutangaza Ndoa Yake imevunjika..

Kuna msemo wa Kiswahili unasema,Simulia ila usiombee yakukute !! Pata picha tukio la mpenzi wako analipia kabisa liwekwe Bango kubwa barabarani lenye ujumbe kwamba wewe na yeye biashara yenu imefikia mwisho, yani hakuna mapenzi tena !!
Watu wa maeneo ya Sheffield, Kaskazini mwa Uingereza wameishuhudia hii yani pembeni ya barabara kubwa kabisa, mwanamke mmoja ambaye jina lake ni Lisa aliona afanye maamuzi magumu baada ya kutopendezwa na kitendo cha mumewe kuwa sio mwaminifu kwenye uhusiano wao, mama akaona isiwe shida.. kaenda kwenye Kampuni ambayo inahusika na kuweka mabango makubwa mjini, akalipia na yeye litundikwe Bango lenye ujumbe maalum kabisa kwa mumewe.
MAIN-Sign-on-motorway-woman-dumping-husband
Jamaa nao kwa sababu hiyo ni biashara yao hawakuwa na neno, siku ilipofika wakaenda kutundika Bango hilo ambapo baadhi ya Mashuhuda wamesema walishuhudia Bango hilo linaning’inia kati ya saa 12 mpaka saa tatu asubuhi, muda ambao kunakuwa na msongamano mkubwa wa magari kwa wanaowahi kwenye shughuli zao.
Kwenye Bango kulikuwa na maneno ambayo Lisa aliyaandika kwa mumewe Paul kwamba aendelee tu na maisha yake akirudi hatomkuta nyumbani, na anamtakia kazi njema.
Bango
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

AFRICAN SPOTRS BADO UGENI UNAWASUMBUA

 Mchezaji wa timu ya African Sports, Victor Agai, akiwatoka mabeki wa timu ya Mgambo JKT katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara LEO Uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga.

 , Washabiki wa timu ya African Sports wakiishangilia timu yao  wakati wa mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara uwanja wa CCM Mkwakwani leo.
Tangakumkekuchablog
Timu za Tanga bado hazijatulia na hivyo kuendeleza kupokea dozi ya mabao kutoka kila timu inayopambana nao na leo, African Sports imekubali kupokea kipigo cha bao 1 bila huruma  ambapo nayo Coastal Union imetandikwa mabao 2 bila huruma hivyo  na hivyo kuendeleza uteja wao
Wakati wa mchezo kuanza Sports waliuanza mpira kwa kasi na kutawala kila idara na kupelekea kukosa magoli matatu kipindi cha kwanza.
Waswahili wanasema siku ya kifo cha Nyani miti yote huteleza na ndipo wapinzani wao, Mgambo JKT ilipopata bao sekunde ya 40 tu ya mchezo kuanza.
Baadhi ya washabiki uwanjani hapo wameiambia tangakumekuchablog kuwa Sports inapaswa kujilaumu kufuatia mabao ya wazi iliyokosa.
Walisema mchezo huo ulikuwa wao baada ya kutawala kuanzia kipindi cha kwanza hadi mpira kuisha.

COASTL UNION YATANDIKWA BILA HURUMA NA WASAGAJI UNGA


AZAM FC imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Coastal Union ya Tanga, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. 
Mchezo huo uliocheeshwa na refa Alex Mahagi wa Mwanza, mabao ya Azam yalifungwa na beki Shomary Salum Kapombe na mshambuliaji Kipre Herman Tchetche raia wa Ivory Coast, yote kipindi cha pili.
Kipre Tchetche ameendela kuifungia Azam FC Ligi Kuu 

Kapombe alifunga bao safi dakika ya 47 akimalizia mpira wa kona uliopigwa na winga Farid Mussa, wakati Kipre Tchetche alifunga dakika ya 74 akimalizia krosi ya kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy.’
Refa Mahagi alimtoa nje Kocha wa Azam FC, Muingera Stewart Hall baada ya kupishana kauli na mwamuzi wa kiba dakika ya 79.
Azam FC inatimiza pointi 15 baada ya kushinda mechi zake zote tano za mwanzo za Ligi Kuu.
Kikois cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Shomary Kapombe, Racine Diouf, Pascal Wawa, Said Mourad, Farid Mussa, Frank Domayo, Jean Baptiste Mugiraneza, Ramadhani Singano ‘Messi’/Salum Abubakar ‘Sure Boy’ dk65, Allan Wanga/Didier Kavumbangu dk72 na Kipre Tchetche/Ame Ali ‘Zungu’ dk77.
Coastal Union; Sebwato Nicholas, Hamad Juma, Tumba Lui, Yassin Mustafa, Abdallah Mfuko, Youssoufa Sabo, Twaha Ibrahim ‘Messi’, Nassor Kapama/Mohammed Hamisi dk56, Ali Ahmed ‘Shiboli’/Chidiebele Abasalim dk61, Ayoub Yahaya na Ismail Mohammed.

RAIS WA NIGERIA AJIPACHIKA NAFASI YA UWAZIRI WA MAFUTA

Rais wa Nigeria kajipa majukumu haya mengine ndani ya serikali yake…

May 29, 2015 Muhammadu Buhari aliapishwa kuwa Rais mpya wa Serikali ya Nigeria.
Baada ya kuingia madarakani moja ya vipaumbele vya Buhari aliahidi kupambana na rushwa na ubadhirifu wa mali za umma pamoja na kupambana na kundi la kigaidi la Boko Haram.
Headlines za leo kuhusu Rais huyo kupitia kwa msemaji wake, Femi Adesina zimethibitisha kuwa mbali ya nafasi yake hiyo ya kuwaongoza Wanigeria atashika nafasi ya kuwa Waziri wa mafuta akisaidiwa na Naibu wake ili kupambana na wanaotumia vibaya nafasi kama hizo.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

TASWIRA YA TANGAKUMEKUCHA LEO

  Vibarua na Nguvu kazi  katika  maduka  mtaa wa Relini Taifa road  karibu na uwanja wa Tangamano Tanga, wakiangalia mfereji ulioziba na kushindwa kupitisha maji na kusababisha takataka kujaa na kuwa  kero kwa wapita njia na wenye maduka karibu na mfereji huo.
Wanaharakati na wadau wa mazingira Tanga wamedai kuwa kukithiri uchafu na takataka katikati ya jiji la Tanga ni kutokana na watu waliopewa dhamana kutojali afya za watu.
Jiji la Tanga inadaiwa toka kupewa hadhi ya jiji yapata zaidi ya miaka 20 lakini bado sifa hiyo haiendani na mazingira halisi ya jiji hilo.
Ili kuweza kuhakikisha mazingira yanakuwa safi na salama kwa matabaka mbalimbali ni vyema halmashauri ya jiji kuchukua hatua kali kwa wachafuzi na wale waliopewa jukumu la kuliweka jiji hilo safi kuanzia mitaro, madampo pamoja na sokoni.
Tangakumekuchablo imekuwa ikiripoti matukio ya uchafuzi na uchafu kila pembe ya jiji hilo ikiwemo mitaani, karo na chemba zinazotiririsha maji machafu pamoja na masoko na madampo yaliyojazana takataka na uchafu ikiwa na lengo la kuhakikisha jiji hilo linakuwa katika usafi na kuwa mfano wa kuigwa.
Kama mtaani kwako au uonapo kero yoyote pale usiifumbie macho, wasiliana nami kwa simu 0655 902929




SAFARI NDEFU ZAIDI DUNIANI UKIWA ANGANI

Hizi ni safari ndefu zaidi za Ndege Duniani, unakaa mpaka saa 17 angani mtu wangu..

Unaweza ukaona safari ya kutoka Mwanza mpaka Dar es Salaam ni ndefu kwa sababu unatumia kati ya saa 12 mpaka 16 ndani ya basi, lakini kwa Usafiri wa Ndege ni kama saa moja tu hivi unakuwa umemaliza safari !!
Sasa hizo saa za kukaa kwenye basi safari ya Mwanza-Dar kuna watu wanazitumia wakiwa angani kwenye Ndege… Nimezipata Rekodi Mitandaoni, zinaonesha safari kumi za Ndege ambazo wasafiri wanatumia muda mwingi zaidi hewani kwenye safari moja.
1.Dubai Mpaka Panama– Hii ni Safari ambayo inachukua saa 17 na dakika 35 angani… yani Ndege ikiruka Dubai hakuna sehemu inatua mpaka ifike Panama. Hii ndio safari ndefu zaidi kwa sasa ambayo inafanywa na Ndege za Emirates… umbali toka Dubai mpaka Panama ni Kilometa 13, 820.
emirates (1)2. Dallas mpaka Sydney- Unaambiwa umbali toka Dallas Marekani mpaka Sydney Australia ni Kilometa 13,804. Hiyo ni safari ambayo inachukua saa 17 kwa Ndege za Qantas.
3. Atlanta mpaka Johannesburg– Hapo kuna umbali wa Kilometa 13,580.. safari hii inakamilika kwa Ndege za Shirika la Delta kukaa angani kwa saa 16 na Dakika 55 ambazo ni kama saa 17 hivi mwanzo mpaka mwisho wa safari.
60966325
4. Los Angeles mpaka Dubai– Kama kuna wakati unawaza kufanya safari kati ya hayo Majiji mawili, basi utambue kabisa kwamba umbali wake ni Kilometa 13,420.. na Ndege inatumia saa 16 na Dakika 30. Hii sio safari fupi hata kidogo mtu wangu !!
5. Los Angeles mpaka Jeddah– Shirika la Ndege la Saudi Arabia ndio ambao wamekamata hii njia, unaambiwa umbali toka Los Angeles Marekani mpaka Jeddah Saudi Arabia inakuchukua saa 17 pia kuimaliza hiyo safari yenye umbali wa Kilometa 13,409.
Picha ya muonekano wa juu wa Jeddah Airport mpya, Saudi Arabia.
Picha ya muonekano wa juu wa Jeddah Airport mpya, Saudi Arabia.
6. Los Angeles mpaka Abu Dhabi– Umbali kati ya hiyo Miji miwili ni Kilometa 13,500.. sio safari ndogo aisee, Ndege za Etihad zinakamilisha hiyo safari kwa saa 16 na Dakika 50 mwanzo mwisho.
7. Houston mpaka Dubai– Kilometa 13,145 zimetajwa kwamba ndio umbali kati ya Miji hiyo miwili, safari yake mwanzo mpaka mwisho kwa Ndege inachukua muda wa saa 16 na Dakika 10… Ndege za Emirates zinahusika pia kusafirisha watu kati ya Miji hii miwili.
8. San Francisco mpaka Abu Dhabi– Umbali kati ya hiyo Miji ni Kilometa 13,130.. na safari yake inachukua saa 16 kukamilika.
9. Dallas mpaka Hong Kong– Hapo unazungumzia Marekani na China, umbali wake ni Kilometa 13,700 na umbali huo kwa safari ya Ndege inachukua saa 16 na Dakika 15… Ndege za American Airlines zimeunganisha hii Miji miwili kwa Ndege za moja kwa moja.
American_Airlines_Boeing_777-200ER_N775AN_PVG_2013-5-21
10. San Francisco mpaka Dubai– Hii nayo imo kwenye list ya safari ndefu za Ndege, umbali wake ni Kilometa 13,040… Ndege za Emirates zimeunganisha hii Miji pia kwa safari ya Ndege ya moja kwa moja. Safari yote inakamilika ndani ya saa 16 na Dakika 40.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

USHAMBA WA SELFIE WAZIDI KUTOA ROHO ZA WATU

Selfie nyingine iliyosababisha kifo cha mwanafunzi huyu..

Bado matukio ya watu kupoteza maisha kutokana na upigaji wa picha za Selfie yameendelea kuripotiwa kila siku.
Hii nyingine ni mwendelezo wa matukio hayo ambapo huko Russia kuna mwanafunzi mmoja kawachukua marafiki zake na kutaka wamsindikize kwenda kupiga selfie ya kipekee kwenye moja ya majengo marefu nchini humo.
Walipofika mwanafunzi huyo akapanda juu ya jengo hilo lenye gorofa tisa na akaanza kupiga picha ili atimize lengo lake la kupiga selfie ya kipekee.
selfie
Sekunde chache baadaye aliteleza na kudondoka chini ambapo alikimbizwa hospitali akiwa na majeraha makubwa na baada ya masaa mawili kupita alifariki dunia.
selfie3

Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapatangakumekuchablog

Tuesday, September 29, 2015

CHRIS BROWN AJUTIA KITENDO CHAKE CHA KUMPIGA RIHANNA

Chris Brown anajutia makosa yake baada ya kuzuiwa kuingia Australia? Kayaandika haya..

Kesi ya Chris Brown kumpiga mpenzi wake wa zamani itabakia kuwa moja ya makosa ambayo Chris Brown anajutia sana kuyafanya… story ambayo iligusa Vichwa vya Habari kwenye Entertainment ikiwa na jina la staa Chris Brown siku chache zilizopita ilikuwa ishu ya Chris kuzuiwa kuingia Australia December 2015 kwa ajili ya kupiga show.
Maombi ya Viza yalikataliwa huku wanaharakati wakionekana kuchochea zaidi Chris azuiwe, hiyo yote ilitokana na hatia aliyokutwa nayo Chris baada ya kumpiga Rihanna miaka zaidi ya mitano iliyopita ..!!
231020130803484502293
Chris kaandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kwamba yeye sio yule mtu mkorofi tena, kingine amesema anakubali makosa yake na anaamini makosa yake ingekuwa ni kitu ambacho wengine wangejifunza kupitia kwake…
Chris II Chris
Chris III
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

VICTOR VALDES, KUFUNGASHIWA VIRAGO VYAKE OLD TRAFORD

Klabu ya Manchester United ipo tayari kuvunja mkataba na golikipa wa kihispania Victor Valdes, baada ya pande zote mbili kukaa chini na kukubaliana kuhusiana na suala hilo, Klabu ya Manchester United ipo tayari kumuachia golikipa huyo ila kama atakubali kuhamia timu ya nje ya Uingereza.
victor-valdes-manchester-united-u21s_3256808
Huu umekuwa ni utamaduni wa vilabu vingi duniani hususani vilabu vya Uingereza havipendi kuuza mchezaji katika klabu pinzani, kwani wengi wamekuwa wakiamini kumuuza mchezaji ndani ya klabu inayoshiriki Ligi Kuu Uingereza ni sawa na kumuuzia adui yako silaha.
Victor-Valdes-Man-Utd-Debut
Mkataba wa Victor Valdes na Manchester United unamalizika mwishoni mwa msimu huu, ila kurejea kwa David de Gea katika kikosi cha kwanza kunatoa nafasi ya Valdes kuondoka, sababu za Valdes kupewa nafasi ya kuhama klabu hiyo zinatokana na kugombana na kocha wa Man United Louis van Gaal, klabu ya Man United haipendi kuona akijiunga na timu inayoshiriki Ligi Kuu Uingereza hususani timu zilizo nafasi nne za juu.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

UZEMBE WA KIPA WA ARSENAL (OSPIMA) WAIGHARIMU ARSENAL NA KUDUNDWA BAO 3, 2



MATOKEO YA LIGI YA MABINGWA ULAYA
Septemba 29, 2015  
Maccabi Tel Aviv 0-2 Dynamo Kyiv 
FC Porto 2-1 Chelsea 
Barcelona 2-1 Bayer 04 Leverkusen 
BATE Borisov 3-2 Roma
Arsenal 2-3 Olympiakos
Bayern Munich 5-0 Dinamo Zagreb
Zenit St Petersburg 2-1 KAA Gent
Lyon 0-1 Valencia CF
Mechi za Leo Jumatano Septemba 30, 2015
FC Astana v Galatasaray
CSKA Moscow Vs PSV 
Juventus Vs Sevilla
Borussia Monchengladbach Vs Manchester City
Malmo FF Vs Real Madrid
Manchester United Vs VfL Wolfsburg
Atletico MadridVs Benfica
Shakhtar Donetsk Vs Paris Saint-Germain
Luis Suarez akishangilia baada ya kuifungia bao la ushindi Barcelona dakika za mwishoni dhidi ya Bayer Leverkusen

MABINGWA watetezi, Barcelona wamepata ushindi mwembamba wa mabao 2-1 usiku huu katika mchezo wa Kundi E Ligi ya Mabingwa Ulaya, dhidi ya Bayer 04 Leverkusen ya Ujerumani Uwanja wa Camp Nou.
Katika mchezo huo, ambao wenyeji walianza kuikosa huduma ya Mwanasoka Bora wa Ulaya, Lionel Messi ambaye ni majeruhi, wageni walitangulia kupata bao kupitia kwa Kyriakos Papadopoulos dakika ya 22.
Hata hivyo, Sergi Roberto Carnicer aliisawazishia Barca dakika ya 80 kabla ya Luis Suarez kufunga la pili dakika mbili baadaye.
Mchezo mwingine wa kundi hilo, BATE Borisov imeshinda 3-2 nyumbani dhidi ya Roma, mabao yake yakifungwa na Igor Stasevich na Filip Mladenovic mawili, wakati ya wapinzani wao yamefungwa na Gervais Kouassi na Vasilis Torosidis.



Mshambuliaji wa Bayern Munich, Robert Lewandowski ameendelea kutisha kwa mabao baada ya kufunga hat-trick

Bayern Munich imeshinda 5-0 dhidi ya Dinamo Zagreb mchezo wa Kundi F, Uwanja wa Allianz Arena mabao yake yakifungwa na Douglas Costa de Souza dakika ya 13, Robert Lewandowski matatu dakika za 21, 28 na 55 na Mario Gotze dakika ya 25.
Mchezo mwingine wa kundi hilo, Arsenal imefungwa mabao 3-2 nyumbani Uwanja wa Emirates na Olympiakos. Mabao ya The Gunners yamefungwa na Theo Walcott dakika ya 35 na Alexis Sanchez dakika ya 65, wakati ya Olympiakos yamefungwa na Felipe Pardo dakika ya 33, David Ospina aliyejifunga dakika ya 40 na Alfred Finnbogason dakika ya 66.
Chelsea imechapwa mabao 2-1 ugenini na FC Porto katika mchezo wa Kundi G Uwanja wa. Mabao ya Porto yamefungwa na Andre Filipe Bras Andre dakika ya 39 na Maicon Pereira Roque dakika ya 52, wakati bao pekee la The Blues limefungwa na Willian Borges Da Silva dakika ya 47.
Mchezo mwingine wa kundi hilo, Maccabi Tel Aviv imefungwa 2-0 nyumbani na Dynamo Kyiv, mabao ya Andriy Yarmolenko na Aluisio Chaves Ribeiro Moraes Junior Uwanja wa Bloomfield.
Cesc Fabregas (kulia) na Diego Costa (katikati) wakiwa taabani baada ya kipigo. Kushoto ni Maicon
Zenit St Petersburg imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya KAA Gent katika mchezo wa Kundi H mabao yake yakifungwa na Artem Dzyuba dakika ya 35 na Oleg Shatov dakika ya 67, wakati bao la wageni limefungwa na Thomas Matton dakika ya 56 Uwanja wa Petrovski.
Mchezo mwingine wa kundi hilo, Valencia ya Hispania imeshinda ugenini 1-0 dhidi ya Lyon ya Ufaransa bao pekee la Sofiane Feghouli dakika ya 42 Uwanja wa Stade de Gerland. 
David Ospina akisikitika baada ya kuwaruhusu Olympiakos kupata bao

Michuano hiyo itaendelea leo n Jumatano, FC Astana ikiikaribisha Galatasaray Uwanja wa Astana Arena, CSKA Moscow ikiikaribisha PSV Uwanja wa Arena Khimki, Juventus ikiikaribisha Sevilla Uwanja wa Juve, Borussia Monchengladbach ikiwakaribisha Manchester City Uwanja wa Borussia-Park, Malmo FF ikiwakaribisha Real Madrid Uwanja wa Swedbank, Manchester United ikiwakaribisha VfL Wolfsburg Uwanja wa Old Trafford , Atletico de Madrid ikiwakaribisha Benfica Uwanja wa Vicente Calderon na Shakhtar Donetsk wakiwakaribisha Paris Saint-Germain Uwanja wa Lviv. 

MANNY PACQUIAO KUDUNDANA NA AMIR KHAN

Manny Pacquiao kurejea ulingoni mwakani, atapigana na nani? jibu lipo hapa…


Bondia wa kimataifa wa Filipino Manny Pacquiao ambaye mwezi May mwaka 2015 alidundwa na bondia mwenye rekodi ya kutopigwa Floyd Mayweather, ameanza kurejea katika hali yake ya kawaida baada ya kufanyiwa upasuaji katika bega la kulia. Manny Pacquiao mara ya mwisho kuingia ulingoni ilikuwa dhidi ya Floyd Mayweather .
2CE3279F00000578-0-image-a-40_1443517091461
Manny Pacquiao baada ya kushindwa pambano hilo alitoa sababu kuwa moja kati ya vitu vilivyochangia kupoteza pambano hilo ni bega lake ambalo lilikuwa na mauvu, hivyo alipaswa kufanyiwa upasuaji ila ilimlazimu kuingia ulingoni baada ya maandalizi ya pambano hilo, yalikuwa yamekamilika kwa kiwango kikubwa hivyo ilikuwa ngumu kuhairisha.
2CE3279300000578-0-image-a-39_1443517088399
Stori zilizoandikwa jana September 29 ni kuwa bondia huyo atarudi ulingoni mwakani dhidi ya Amir Khan, taarifa hizi zinakuja baada ya Manny Pacquiao kufanyiwa kipimo cha MRI Scan na kugundulika kuwa anaendelea vizuri. Promota wa bondia huyo Bob Arum alithibitisha wiki iliopita kuwa yupo katika mazungumzo na timu ya Amir Khan na mambo yanaenda vizuri.
2CE0076E00000578-0-image-a-37_1443517077500
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

NANI UTAMUOKOA ?

Utamuokoa nani, mama au mpenzi wako?

  • Wazimamoto Kazan, Urusi
Ungelazimishwa kuamua nani utakayemuokoa, ungemuokoa mama au mpenzi wako kutoka kwa jumba linaloteketea?
Hili ni swali tata linaloulizwa sana Uchina. Na mwaka huu, lilikuwa kwenye mtihani wa kitaifa wa uanasheria, likiulizwa mawakili na majaji wa siku za usoni. Wanaopita mtihani huo ndio pekee huruhusiwa kuhudumu kama wanasheria nchini Uchina.
Wajua jibu sahihi lilikuwa lipi? Wizara ya Haki nchini Uchina baadaye ilichapisha jibu “sahihi”: kwamba watahiniwa wana wajibu wa kuwaokoa mama zao. Litakuwa “kosa la kutochukua hatua” kwa mtu kuamua mapenzi kwanza badala ya damu.
Lakini jibu hilo si rahisi sana kwa watumiaji wa mtandao Uchina, ambao wamekuwa wakijibizana kuhusu jibu sahihi. “Ni jambo la kushangaza kulinganisha jukumu la kuwasaidia wazazi na jukumu la kusaidia wengine wakati wa dharura,” alilalamika mmoja.
“Kwa mujibu wa sharia, mwana wa kiume lazima amuokoe mamake,” alilalamika mwingine. “Lakini sharia haisemi lazima amuokoe mamake iwapo kuna watu wengine ambao wamo hatarini pia.”
Wengine walipoulizwa wangemuokoa nani, penzi la mama lilionekana kuongoza. “Wasichana wamejaa kila pahali, lakini nina mama mmoja pekee,” kijana mmoja alisema. “Bila shaka ningemuokoa mamangu kwanza,” alisema mwingine. “Kando na sababu za kisheria, mamangu alinilea. Isitoshe, mpenzi wangu ni mchanga, na ina maana kwamba ana uwezekano wa juu kujiokoa bila usaidizi”
Jambo la kushangaza ni kwamba hakuna yeyote mtandaoni Uchina aliyeonekana kugundua mwegemeo wa kijinsia wa swali hilo. Labda kungelikuwa na swali la ni nani mwanamke anayefaa kumuokoa kwanza, babake au mvulana mpenzi wake.

AFUNGUA MLANGO WA KUTOKEA BADALA WA TOILET WAKATI NDEGE IKO ANGANI

Abiria kakosea mlango Ndege ikiwa angani, badala ya chooni akaenda kwenye mlango wa kutokea nje..

Ndege ya Shirika la KLM ilikuwa katikati ya safari kutoka Edinburgh kwenda Amsterdam, Uholanzi… ilibaki kidogo mambo yaharibike katikati ya safari.. abiria mmoja akakosea mlango, badala ya kufungua mlango wa kuingia chooni, yeye akaenda moja kwa moja kwenye mlango wa kutokea nje huku ndege ikiwa juu angani na safari inaendelea !!
Ingekuwa mlango huo ni mwepesi kuufungua kama mlango wa gari basi mambo yangekuwa tofauti, jamaa huyo James Gray, baada ya ndege kutua Uwanja wa Schiphol Airport alikamatwa na Askari na kuwekwa ndani kwa saa kadhaa alafu akaachiwa baada ya kupigwa faini ya Pound 440 ambazo ni kama Tshs. Milioni 1.4.
james-gray
Huyo ndio James Gray mwenyewe, na picha nyingine anaonekana alivyokamatwa na Polisi baada ya kutua uwanja wa Ndege.
Adhabu yake haijaishia hapo, jamaa kazuiwa pia kusafiri kwa Ndege za KLM kwa kipindi cha miaka mitano… Kwa vile yeye ni raia wa Scotland, ilibidi atumie usafiri wa Ndege nyingine kurudi kwao huku akijitetea kwamba yeye hata hakujua kwamba huo mlango ni wa kutokea nje.
Upande wa kushoto hapo ni mklango wa Choo ndani ya ndege, upande wa kulia ni mlango wa kutokea nje ya ndege.. hapo ndipo jamaa alipochanganyikiwa.
Upande wa kushoto hapo ni mlango wa Choo ndani ya ndege, upande wa kulia ni mlango wa kutokea nje ya ndege.. hapo ndipo jamaa alipochanganyikiwa.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

MAJENGO YALIYOWEKA REKODI KWA UREFU DUANIANI

Unayajua majengo yaliyoweka rekodi kwa urefu zaidi duniani? Nimekusogezea hapa…


Dubai, Shanghai, New York City ndio miji inayoongoza kuwa na mpangilio mzuri wa majengo duniani na ndiyo inayoongoza kwa kujenga  majengo marefu yaliyoweza kuingia kwenye rekodi za dunia.
Ukuaji wa miji hii mikubwa ndio matokeo ya teknolojia iliyowezesha kuwa na miundombinu bora na iliyoweka rekodi duniani.
Nimekusogezea majengo 10 yaliyovunja rekodi kwa urefu zaidi duniani…
burj
1. Burj Khalifa

shanghai
2. Shanghai Tower

maka
3. Makkah Clock Royal Tower

jengo4
4. One World Trade Center

jengo5
5. CTF Finance Centre

jengo6
6. Taipei 101

jengo7
7. Shanghai World Financial Center

jengo8
8. International Commerce Centre

jenho9 na 10
9 na 10 Petronas Towers, hili ni jengo pacha
Maelezo yake nimekuwekea hapa..
# Building City Floors Height Year
1
Burj Khalifa Dubai 163 828 m 2010
2
Shanghai Tower Shanghai 121 632 m 2015
3
Makkah Clock Royal Tower Makkah 120 601 m 2012
4
One World Trade Center New York City 104 541 m 2014
5
CTF Finance Centre Guangzhou 116 530 m 2016
6
Taipei 101 Taipei 101 509 m 2004
7
Shanghai World Financial Center Shanghai 101 492 m 2008
8
International Commerce Centre Hong Kong 118 484 m 2010
9
Petronas Tower 1 Kuala Lumpur 88 452 m 1998
10
Petronas Tower 2 Kuala Lumpur 88 452 m 1998

Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog