Wednesday, May 31, 2017

MANCHESTER UNITED KLABU YENYE THAMANI ZAIDI DUNIANI

Man United ndio klabu yenye thamani kubwa UlayaManchester United ndio klabu yenye thamani kubwa barani Ulaya ikiwa na thamani ya Yuro bilioni 3 kulingana na kampuni ya biashara ya KPMG.
Mabingwa hao wa kombe la Yuropa wanaongoza katika orodha ya thamani ya Kampuni ya KPMG, ikiwa mbele ya mabingwa wa Uhispania Real Madrid na Barcelona.
Utafiti huo uliangazia haki za kupeperusha matangazo, faida, umaarufu, uwezo kimchezo na umiliki wa uwanja.
Katika utafiti huo uliofanyiwa timu 32, vilabu vya Uingereza vilitawala orodha hiyo vikijaza nafasi sita kati ya 10 bora.
Andrea Sartori ambaye ni mkurugenzi wa maswala ya michezo katika kampuni ya KPMG amesema kuwa kwa jumla thamani ya soka imekuwa katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.
''Huku hilo likielezewa kufuatia kuimarika kwa matangazo, operesheni za biashara za kimataifa, uwekezaji wa vifaa vya umiliki wa kibinafsi, vifaa vya kisasa pamoja na usimamizi mzuri ni vigezo muhimu vya ukuaji huo'', alisema.
Kuhusu haki za matangazo, ligi kuu ya Uingereza inaongoza ligi nyengine za Ulaya ijapokuwa ligi nyengine zimeweka mikakati kupigania mashabiki wa kimataifa.
Vilabu kumi bora vyenye thamani ya juu kibiashara
  • 1.Manchester United -Euro3.09bn
  • 2.Real Madrid - Euro2.97bn
  • 3.Barcelona - Euro2.76bn
  • 4.Bayern Munich - Euro2.44bn
  • 5.Manchester City - Euro1.97bn
  • 6.Arsenal - Euro1.95bn
  • 7.Chelsea - Euro1.59bn
  • 8.Liverpool - Euro1.33bn
  • 9.Juventus - Euro1.21bn
  • 9.Tottenham - Euro1.01bn
  • Duru: KPMG

BIASHARA FUTARI BARABARA YA 10 TANGA



Wafanyabiashara wa vitafunwa nje ya Msikiti mkuu wa Ijumma barabara ya 10  Tanga, wakiwauzia wateja na waumini   waliofunga mfungo wa Ramadhani.





Tuesday, May 30, 2017

SIMULIZI, NILIKIONA CHA MOTO USRITHI WA BABU SEHEMU YA 33

ZULIA LA FAKI
 
NILIKIONA CHA MOTO URITHI WA BABU 33
 
ILIPOISHIA
 
“Kumbe babu  yako alikuwa na mke jini, ndiyo  maana alipata utajiri ghafla! Lakini hakuwahi kunieleza hata siku moja. Alikuwa  msiri sana”
 
“Huyo jini sasa amejitokeza kwangu na anataka nimrithi ili anipe utajiri aliokuwa nao  babu yangu”
 
“Sasa ulitaka nikupe ushauri gani?”
 
“Nimkubalie au nimkatalie?”
 
Mganga baada ya kutafakari aliniambia.
 
Umefanya vizuri kuja kwangu. Mimi nitakupa ushauri mzuri”
 
“Nitakushukuru sana”
 
“Usikubali. Huyo  jini atakusumbua sana na pengine atakuja kukuua. Sasa nimeanza kugundua kuwa hata babu yako aliuawa na huyo jini”
 
SASA ENDELEA
 
Maneno ya mganga huyo yakanishitua.
 
“Kumbe hivi viumbe vina madhara makubwa?” nikamuuliza
 
“Wewe hujui tu. Hawa viumbe si wazuri. Uliona wapi jini akaolewa na binaadamu?”
 
“Sijawahi kuona”
 
“Sasa ujue kuwa hicho kitu hakiwezekani. Huyo jini anakilazimisha kwa nia mbaya. Amemuua babu yako, sasa anataka kukuua wewe”
 
Nikabaki nimepigwa na butwaa la mshangao.
 
“Wewe angalia vituko na miujiza aliyokufanyia ndipo utajua ana madhara ya kiasi gani”
 
“Sasa nifanye nini ili niweze kuepukana naye?”
 
“Njoo kesho asubuhi, nitajua jinsi ya kukusaidia. Huyo hawezi kuondoka mwenyewe mpaka  nimuondoe mimi”
 
“Sasa hapo kesho utakuja kumuondoa?”
 
“Nitamuondoa na utaishi kwa usalama. Wewe ni binaadamu, wajibu wako ni kuoa binaadamu mwenzako mzae watoto na sio jini. Kama utaoana  na jini mtazaa watoto gani? Mtazaa binaadamu au majini?”
 
Mganga aliniuliza swali hilo  lakini sikuwa na jibu. Nikaona kweli ushauri wa kumrithi yule jini haukuwa na maana.
 
“Kama ulivyoniambia nitakuja kesho unishighulikie” nilimwambia mganga huyo kabla ya kuagana naye.
 
Nilipoondoka nyumbani kwa mganga huyo niliona  mawazo yake yalikuwa sahihi. Si tu ningejitafutia  matatizo  mimi mwenyewe kwa kukubali kuishi  na jinni bali pia sikuwa na uhakika tungezaa watoto wa aina gani.
 
Kama tungezaa watoto wa kijini wasingekuwa na manufaa kwangu na hata kama watoto hao wangekuwa ni binaadamu bado wasingekuwa binaadamu kamili, wasingeweza kuishi na watu wengine.
 
Lakini kulikuwa na kitu kilichojificha ambacho nilikuwa sikijui. Nilikuwa sijui  kwamba yale maneno ya yule mganga yalikuwa  ni ya roho mbaya. Alikuwa akitia  fitina ili mimi nisimrithi yule mwanamke wa kijini kwa kuona kwamba nitaidi utajiri wa bure.
 
Lengo lake la kuniambia niende kesho lilikuwa ni kutafuta  mbinu  ili amchukue yeye jini huyo.
 
Asubihi ya siku ya pili yake nikaenda tena kwa mganga huyo.
 
“Sasa mwanangu unajua hii kazi haitafanyika hapa. Itafanyika shanbani kwangu. Itabidi twende shamba” akaniambia.
 
“Sawa. Tunaweza kwenda. Gari lipo”
 
Mganga akaandaa vifaa vyake. Akawachukua wasaidizi wake wawili ambao bila shaka alishawaeleza tunakwenda shamba kufanya nini.Tukaondoka  na  gari.
 
Shamba hilo lilikuwa kule kule  Chanika lakini lilikuwa mbali kidogo.  Akaniambia tuingize gari ndani ya shamba hilo. Nikaliingiza gari na kulisimamisha mbele ya nyumba yake ya miti na udongo iliyokuwa katikati ya shamba.
 
Tukashuka na kuingia kwenye ile nyumba.
 
Kwa  jinsi  nilivyofahamu baadaye ni kuwa ili aweze kumchukua Maimun alitaka kwanza aniue mimi na ndiyo madhumuni ya kunipeleka huko shamba.
 
Baada ya kuniua alitaka achukue damu yangu na kuioga mwilini mwake kisha ajipake mafuta ya waridi.
 
Tulipoingia kwenye ile nyumba nikaambiwa nikae chini. Kwanza  kilianza kisomo. Nilisomewa na watu watatu bila  kuambiwa ninasomewa nini.
 
Baada ya kisomo hicho mganga alikoroga dawa kwenye kikombe akanipa ninywe.
 
“Kunywa hii dawa” alinaimbia kisha akaongeza.
 
“Nitakupa na dawa nyingine ya kuoga”
 
Kumbe ile haikuwa dawa. Ilikuwa sumu! Alitaka niinywe ili  nife pale pale na kisha wanitoe damu kabla haijakauka.
 
Kile  kikombe nilikipokea nikakisogeza midomoni mwangu ili ninywe ile dawa niliyoambiwa. Hapo hapo niliona kikombe kinabetwa. Kikanitoka mkononi na kuanguka chini.  Sumu iliyokuwamo ikamwagika. Yule mganga na wasaidizi wake walikuwa wameshangaa. Aliyenibeta kikombe hakuonekana!
 
Ghafla nikasikia mganga anapigwa kibao  cha nguvu na kuanguka chini. Alivyoanguka alinza kutokwa  na povu mdomoni. Wale wasaidizi wake walipoona hivyo walitimua mbio.
 
Nikabaki nimekaa nikiwa sijui kinachoendelea. Ikabidi niinuke na kumtazama yule mganga. Nikaona amekauka. Tukio hilo likanishitua.
 
Nikatoka nje ya ile nyumba kuwatazama wale waliokimbia lakini sikuwaona.  Nikasikia ninaitwa ndani ya gari langu. Niliposogea kwenye mlango nikamuona Maimun amekaa kwenye siti ya upande wa pili wa dereva.
 
“Ingia twende zetu” akaniambia.
 
Nikafungua mlango wa gari na kujipakia.
 
“Washa gari tuondoke”
 
Nikawasha gari.
 
“Umeuona  upuuzi wako?” Maimun akaniuliza.
 
Kwa vile nilikwenda pale  kwa ajili ya kumfukuza yeye, sikujibu kitu. Nilihisi pengine upuuzi aliokusudia ulikuwa ni huo.
 
“Sisi tunakubaliana kitu vizuri halafu wewe unakwenda kwa mganga! Ulikwenda kwa mganga kufanya nini?” Maimun akaniuliza.
 
Kwa kweli nilitahayari aliponiuliza hivyo. Nikaendelea kubaki kimya.
USIKOSE Uhondo huu kesho hapahapa

Monday, May 29, 2017

ARSENAL WENGER MGUU MMOJA NDANI MGUU MMOJA NJE

Kroenke (kulia) amewahi kumtaja Wenger kama kocha bora kwa klabu hiyoIdadi ya vikombe Wenger alivyofanikiwa kuvibeba akiwa ArsenalKocha wa Arsenal Arsene Wenger amefanya mkutano muhimu na mmliki wa klabu hiyo Stan Kroenke Jumatatu ambapo mustakabali wa mfaransa huyo ulitarajiwa kujadiliwa.
Matokeo ya mkutano huo bado hayajawekwa wazi, lakini maamuzi yanabaki baina ya Wenger na Kroenke na yatategemea pia kikao cha bodi kitakachojadili suala hilo leo hii.
Bado haijajulikana kama Wenger ataongeza mkataba baada ya kudumu katika klabu hiyo kwa miaka 21.
Masharti ya mkataba mpya yalikubaliwa miezi kadhaa iliyopita, lakini hakuna kilichofanyiwa kazi mpaka hivi sasa.

Sunday, May 28, 2017

SHOMO BARABARA YA 19 NGAMIANI TANGA



Wakazi wa barabara ya 19 Ngamiani Kusini wakiangalia shimo lililobomoka katikati ya barabara na kuhatarisha usalama wa watumiaji wa vyombo vya moto na wapita kwa miguu.





ARSENAL WENGER MMOJA WA WAKUFUNZI BODA DUNIANI

Conte anasema kuwa Wenger ni miongoni mwa makocha bora dunianiArsene Wenger atasalia kuwa mmoja kati ya wakufunzi bora duniani hata iwapo Arsenal itapoteza fainali ya kombe la FA kulingana na mkufunzi wa Chelsea Antonio Conte.
Wenger mwenye umri wa miaka 67 amekuwa kocha wa Gunners tangu 1996 na mkataba wake unakamilika mwisho wa msimu huu.
Wenger alisema kuwa hatma yake itaamuliwa na mkutano wa bodi ya klabu hiyo baada ya fanaili ya kombe la FA dhidi ya Chelsea.

POUL POGBA AFANYA ZIARA YA KIUHUJAJI MECCA

Paul Pogba in MeccaMchezaji soka aliye ghali zaidi duniani amefanya ziara ya kihujaji kwenda katika mji mkatatifu zaidi wa Kiislamu, Mecca, wakati wa mwanzo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa Paul Pogba alipakia mtandaoni picha yake akiwa Mecca siku ya Jumapili na kuandika "kitu cha kupendeza zaidi nilichowahi kukitazama maishani mwangu."
Aidha, aliandika ujumbe kwenye Twitter kutakia kila mtu "Ramadhani jema."
BBC

ARSENAL WENGER ADAI KUHUJUMIWA

Arsene Wenger amesema kuwa amehujumiwa sana msimu huuk KOCHA Mkuu wa Arsenal ametaja ukosoaji ambao amekuwa akipata msimu huu kuwa hujuma ambayo hatosahau.
Raia huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 67 ankabiliwa na shutuma kali kutoka kwa mashabiki kwa kumtaka kuondoka katika klabu hiyo ambayo ameingoza tangu 1996.
''Sijali ukosoaji kwa sababu tunafanya kazi ya umma'', aliambia BBC kabla ya mechi ya fainali kati ya Arsenal na Chelsea katika uwanja wa Wembley.
''Ninaamini kuna tofauti kati ya kukosolewa na kuchukuliwa hali ambayo hairuhusu kwa mwanadamu''.

CHALES MWIJAGE AFUNGUA MAONYESHO YA TANO YA BIASHARA TANGA



Meneja Mkuu Idara ya Masoko kiwanda cha saruji cha  Rhino Tanga, William Malonza, akimuonyesha moja ya bidhaa zizalishwazo na kiwanda hicho, Waziri wa Viwanda na Biashara, Chales Mwijage, wakati wa maonyesho ya tano ya Kimataifa ya biashara yanayofanyika katika viwanja vya Mwahako Tanga.
Mwijage ameyafungua maonyesho hayo leo katika viwanja ya maonyesho Mwahako ambayo yamezishirikisha mataifa mbalimbali ya Barani Afrika na Asia.


Waziri wa Viwanda na Biashara, Chales Mwijage, akisalimiana na Afisa Masoko kiwanda cha saruji cha  Rhino Tanga, Carolina Hillary wakati alipotembelea banda la maonyesho ya tano ya Kimataifa yalifunguliwa jana Tanga katika viwanja vya maonyesho Mwahako.

 Waziri wa viwanda na Biashara, Chales Mwijage, akibadilishana mawazo na Meneja Mkuu Idara ya Masoko kiwanda cha Saruji cha Rhino Tanga, William Malonza wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika Tanga.
 Waziri wa Viwanda na Biashara, Chales Mwijaga akipata maelekezo ya namna mkonge unavyoweza kutengeneza dawa  pamoja na mafuta aina mbalimbali.


 Simba ni moja katika wanyama ambao wameletwa kwa ajili ya maonyesho Tanga

Wakazi wa Tanga wakiangalia Kobe ambaye ni moja ya vivutio katika maonyesho ya tano ya Kimataifa yanayofanyika Tanga.