Sunday, October 11, 2015

KLOPP AANZA KUINGIZA MKWANJA

Du!!! kabla ya kuanza kuifundisha Liverpool, Jurgen Klopp kaanza kuiingizia mkwanja Liverpool

Ikiwa ni siku moja imepita toka klabu ya Liverpool wamtambulishe kocha wao mpya Jurgen Klopp mbele ya waandishi wa habari na kuanza kufanya mahojiano na kocha huyo wa Kijerumani, mengi yaliandikwa ila kauli yake imegeuka fursa ya kibiashara na tayari imeanza kuzalisha fedha.
Jurgen Klopp ambaye hadi anaondoka katika klabu ya Borussia Dortmund alikuwa na heshima kubwa kutokana na mambo mazuri aliyoifanyia klabu hiyo, licha ya kuwa nyakati za mwishoni hakuwa akifanya vizuri na timu kiasi cha kushika nafasi za chini katika msimamo wa Ligi Kuu Ujerumani. Kama ambavyo tumezoea kuona mchezaji mpya au kocha mpya akitambulishwa huwa kuna interview fupi pamoja na kuongea na mashabiki wa klabu husika.
Kwa upande wa Jurgen Klopp alizungumza kauli kadhaa ila moja kati ya kauli alizoongea kuwa yeye ni kocha wa kawaida na angependa aitwe ‘the normal one’ ni jina ambalo tofauti kidogo na kocha wa Chelsea Jose Mourinho ambaye hupenda kujiita ‘the special one’. Jina hilo ambalo angependwa kuitwa limeandikwa katika fulana na kuanza kuuzwa kwa mashabiki wa Liverpool, ikiwa ni chini ya masaa 24 toka atamke kauli hiyo.
download (2)
Hizi ni tisheti za kiume ambazo zina msemo wa ‘the normal one’ na tovuti ya Liverpool imeanza kuuza tisheti hizo.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment