Kumekucha blog
Tanga, JESHI la Polisi kituo kikuu cha
Chumbageni Tanga, kinamshikilia Said Khamis (28) mkazi wa Pongwe kwa tuhuma za kupatikana na kilo 1 na misokoto 7 ya bangi wakati wa msako wa
safishasafisha wauzaji na walaji wa madawa ya kulevya.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Kaimu
kamanda wa polisi Mkoa, Juma Ndaki, alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa juzi saa
5 asubuhi baada ya jaribio lake la kuwatoroka polisi kushindikana.
Alisema polisi iko katika msako wa kuwatokomeza watumiaji na
wauzaji wa madawa ya kulevya na kuwafikisha mahakamani lengo likiwa ni
kutokomeza magenge ya uvutaji na uuzaji wa madawa hayo.
“Unajua kuwa kipindi hiki ni cha harakati nyingi zikiwemo za
kuelekea sikukuu ya krismas na mwaka mpya----polisi inalazimika kuweka
mazingira mazuri ya wananchi kusherehekea” alisema Ndaki
“Polisi imezidisha doria usiku na mchana na hata ninyi
waandishi wa habari nadhani huko mitaani kwenu munawaona vijana wetu
wakipita----ila niwaambie wananchi wasitishike wakiona askari wako na mbwa na
mabunduki begani” alisema Ndaki
Akizungumzia hali ya uhalifu, Ndaki alisema polisi wameweza
kuzima matukio ya uporaji wa kutumia nguvu nyakati za usiku ukiwemo wa pikipiki
na baskeli pamoja kuharibu mitambo ya utengenezaji wa pombe aina ya gongo.
Alisema jumla ya mitambo mitano katika maeneo tofauti
walitekeleza na kuiharibu na wamiliki kufikishwa mahakamani jambo ambalo limesaidia kuwepo kwa hali ya
usalama mitaani.
Alisema magenge hayo ya unywaji wa pombe imekuwa ikizalisha
magenge ya kihalifu na kusababisha
wazazi kuongozana na watoto wao wadogo katika vilabu na kuwa chanzo cha kuacha
masomo shuleni.
“Jumla ya mitambo mitano ya utengenezaji wa pombe aina ya
moshi imetekelezwa na kuharibiwa katika kipindi hiki cha safishasafisha utumiaji
wa madawa ya kulevya na wauzaji” alisema Ndaki
Akitoa wito kwa wananchi kaimu huyo kamanda, aliwataka kutoa
taarifa kwa jeshi hilo wanapona matukio pamoja na watu ambao hawatambuliki
wakijihusisha na vitendo vinavyohusiana na uhalifu.
Kumekucha blog
No comments:
Post a Comment