Thursday, December 11, 2014

HADITHI ----KISIWA CHA HARISHI,


HADITHI
 
KISIWA CHA HARISHI (8)
 
ILIPOISHIA TOLEO LILILOPITA
 
Mara kwa mara nilikuwa nikitupa macho kila upande wa chumba hicho kwa hisia kwamba Harishi angeweza kutokea mle chumbani.
 
Asubuhi kulipokucha Yasmin alikuja kutugongea mlango.
 
“Amkeni. Kumeshakucha” Alikuwa akituambia wakati akigonga. Tukatambua kuwa alikuwa ni yeye.
 
Tukafungua mlango.
 
“Mmeamkaje?” akatuuliza.
 
“Tunashukuru tumeamka salama” nilimjibu kwa niaba ya wenzangu.
 
Wenzetu waliolala chumba kingine walikuwa hawana habari ya tukio lililotokea usiku. Nikawaeleza mbele ya Yasmin. Wakasikitika sana na kupata hofu.
 
“Sasa nendeni mkaoge halafu niwaandalie chai” Yasmin akatuambia.
 
Tukaenda kuoga. Kwanza waliingia watu wanne kwa vile vyoo vilikuwa vine. Walipotoka nikaingia mimi na mwenzangu.
 
Yasmin akatuandalia chai pale sebuleni. Ilikuwa chai iliyotengezwa kwa maziwa ya unga na iliyoungwa kwa iliki, tangawizi na bdalasini. Pia alitupa mikate iliyotengezwa kwa mayai.
    
SASA ENDELEA
 
Yeye mwenyewe alikunywa chai pamoja na sisi. Nikamuona amefurahi na kuchangamka licha ya kwamba usiku wa jana yake tu tulishuhudia machungu ya kuuawa mwenzetu.
 
“Ningekuwa nakula na wageni kila siku namna hii ningechangamka, lakini mh!” Yasmin alisema kama aliyekuwa akisema pek yake.
 
“Ni kweli Yasmin lakini tutafanyaje? Tunapenda kukusaidia lakini hatuna uwezo. Kama hivyo umeona mwenzetu ameshauawa na sisi hatujui maish yetu yatakuwaje!” nikamwambia Yasmin kwa huzuni.
 
“Kusema ukweli napenda niendelee kuwa na nyinyi hapaili nipate wenzangu wa kuzungumza nao. Lakini haitawezekana nyinyi muwepo hapa mkiwa hai.”
 
“Na pia hatuna mahali pengine pa kwenda” nikamwambia Yasmin.
 
“Huu ni mtihani. Sijui mtatumia mbinu gani muwe salama”
 
“Labda tuendelee kujifichaficha humu ndani” Mwenzetu mmoja akaingilia yale mazungumzo.
 
“Humu ndani atawagundua tu” Yasmin akamjibu.
 
“Sasa tutakwenda wapi jamani!”
 
“Mimi sijui niwambie nini ndugu zangu!” Yasmin akatuambai.
 
Tulipomaliza kunywa chai Yasmin aliondoa vyombo. Alituacha tumekaa tukiendelea kujadiliana. Baadaye kidogo alirudi akiwa na karata.
 
“Hizi karata ziko siku zote. Huyu mwendawazimu ananiletea. Lakini sina mwenzangu wa kucheza naye”
 
Tulipoona karata tukazunguka duara. Yasmin akakaa na kutugawia.
 
“Tunacheza mchezo gani?” nikamuuliza Yasmin.
 
“Tunacheza mchezo wa arbasitini”
 
Mchezo huo ulikywa maarufu kule Zanzibara na Comoro.
 
Tukaanza kucheza karata. Tukasahau kabisa habari ya Harishi. Mchezo ulinoga sana. Kelele zetu zikawa zinasikika hadi nje.
 
Ilipofika saa tano Yasmin akavunja mchezo na kutuambia tukatembee tembee. Tukiona jua la saa saba ndio turudi kula chakula. Mda ule alitaka kwenda kupika chakula.
 
“Niwapikie nini?” akatuuliza.
 
“Tupikiechochote tu utakachopenda” nikamwambia.
 
“Basi nitawapikia pilau”
 
“Tutashukuru sana”
 
“Sasa mtakapokuja, kwanza mchungulie na kusikiliza. Mkimuona Harishi msiingie ndani, rudini huko huko mtakakotoka. Anaweza kuja ghafla”
 
“Tumekuelewa” nilimjibu.
 
Baada ya hapo tulitoka tukarudi kule kwenye boti letu.
 
Ni tabia ya maumbile ya binaadamu kutokata tama na kujaribu kubahatisha kila mara hasa kwa watu kama sisi ambao tulikuwa katika hatari. Kwa mara nyingine tulijaribu tena kuliwasha lile boti. Kila mmoja wetu alijaribu kuliwasha bila mafanikio.
 
Tukakaa chini ya mti na kuanza kujadiliana. Hata hivyo mjadala wetu ulikuwa kama usio na maana yoyote kwani haukutupa ufumbuzi wa jinsi ya kusalimisha maisha yetu.
 
Kikubwa tulichokizingatia ni kujaribu kumkwepa Harish kadiri itakavyowezekana. Tuliona kama tutafanikiwa kumkwepa tunaweza kuendelea kuishi.
 
Tuliendelea kukaa pale chini ya mti hadi saa saba tulipoamua kurudi kwa Yasmin. Tulimtuma mmoja wetu aingie akachunguze kama Harishi yuko ndani aje atuambie.
 
Mwenzetu huyo akaingia ndani. Sisi tukawa tunamchungulia kwenye dirisha. Alinyata hadi ndani. Tukawa hatumuoni tena. Tukahamia kwenye dirisha jingine. Tukamuona amesimama pembeni mwa ukumbi akiangalia huku na huku. Akaenda jikoni kuchungulia kisha akatoka.
 
Alipotoka jikoni alikwenda moja kwa moja kwenye mlango wa chumba cha Yasmin na kutega masikio yake kwenye mlango. Alisikiliza kwa muda kidogo kisha akaanza kugonga mlango taratibu.
 
Mlango ukafunguliwa ghafla. Aliyetoka alikuwa Yasmin. Alitoka haraka haraka akaufunga mlango kisha akamuashiria yule jamaa aondoke. Nikajua kuwa hapakuwa salama.
 
“Moshi unajaa kwenye chupa, Harishi anakuja!” Yasmin alimwambia.
 
Yule mwenzetu aliposikia vile aligeuka ili aondoke lakini ghafla tena mlango ukafunguliwa. Harish akaibuka mbele ya yule mtu. Alikuwa ameshika upanga wake. Akamshika yule jamaa kwa mkono mmoja.
 
“Unataka ukimbie wapi wewe?” akamuuliza akiwa amemtolea macho.
 
ITAENDELEA KESHO
 USIPITWE NA KISA HIKI CHA KUSISIMUA KESHO NI KITATOKEA

No comments:

Post a Comment