|
HADITHI
KISIWA CHA HARISHI (9)
ILIPOISHIA TOLEO
LILILOPITA
Mwenzetu aliishiwa na
nguvu kabisa. Akawa amemkodolea macho Harishi.
“Mimi nasikia harufu
zenu tangu jana”
Mwenzetu kimya. Sasa
mwili wake ulikuwa ukitetemeka waziwazi.
“Sheikh nisamehe
sana…” Sauti yake ikasikika kwa mbali ikiomba.
“Chombo chetu
kiliharibika jana”
Harisha alikuwa
akimtazama kama vile alikuwa hamuelewi.
“Wasemaje?”
“Nisamehe
sana…nakuomba” jamaa alikuwa analia.
“Kwani wewe huna
damu?. Ngoja nione”
Hapo hapo Harishi
akamuinua juu mwenzetu huyo kwa mkono mmoja tu. Akamgeuza kichwa chini.
Kiasi cha kufumba na
kufumbua tu alishamtoboa utosi kwa ncha ya upanga wake.
Yasmin alipoona hivyo
alikimbilia nje. Akatuona tumeinamia dirisha.
“Jamani balaa gani
hili?” akajisemea peke yake.
SASA ENDELEA
Idadi yetu sasa
tulikuwa watu watano, wenzetu wawili walikuwa wameshauawa. Na sisi pia
hatukuwa na matumaini kuwa tungebaki.
Tulijua kuwa kama
hatutakufa kwa njaa, tutauliwa na lile jini la Yasmin. Kila mmoja wetu
alikuwa ameshikwa na hofu na fadhaa. Tulitamani angalau kipite chombo
kituokoe kuliko vile tulivyokuwa matumatu tukisubiri kufa.
Tulitamani tusifike
tena katika lile jumba la Yasmin lakini tungekula nini, wakati kwa Yasmin
ndiko tunakotarajia kupata riziki yetu. Kusema kweli tulichanganyikiwa na
hatukujua la kufanya.
Tulikaa pale chini ya
mti kwa karibu saa mbili. Ghafla tuliona mwanamke akiambaa na ufukwe wa
bahari akija upande wetu. Mkono mmoja alikuwa ameshika kapu.
“Jamani ni nani yule?”
Mwenzetu mmoja akauliza.
“Naona ni kama Yasmin”
nikajibu.
Mjadala ukaanza.
“Ni Yasmin kweli!”
“Amefuata nini huku?”
“Labda anatutafuta
sisi”
“Mmoja wetu atokeze
ili atuone au aende akampokee lile kapu. Labda anatuletea chakula”
“Hatujui Harishi yuko
wapi. Unaweza kujitokeza ukajikuta unakamatwa!”
“Bila shaka Harishi
ameshaondoka, Yasmin asingeweza kuja huku. Ngoja nimfuate” Mimi ndiye
niliyesema hivyo. Nikanyanyuka na kuanza mwendo kuelekea upande ule aliotokea
Yasmin.
Yasmin akaniona.
“Nawatafuta nyinyi,
mko wapi?” akaniuliza tangu akiwa mbali.
“Tuko huku chini ya
mti. Tumekuona tangu ukiwa mbali”
“Nimewaletea chakula”
Nilikuwa
nimeshamfikia. Nikampokea lile kapu.
Tukawa tunatembea
pamoja kuelekea kule waliko wenzetu
“Lile shetani
limeshaondoka, ndio maana nimeweza kutoka” Yasmin akaniambia’
“Halitarudi tena kwa
leo?”
“Halitarudi labda kwa
kesho”
“Yule mwenzetu ndio
ameuawa?”
“Ndio aliuawa. Si
mliona wenyewe akikamatwa”
Nikatikisa kichwa
changu kusikitika.
“Wakati anabisha
mlango niliona ile chupa ya Harishi inajaa moshi. Nikajua kuwa Harishi
anakuja. Nikawahi kutoka ili niwambie muondoke. Wakati nasemeshana na yule
mwenzenu, Harishi akasikia akawahi kutoka na kumkamata” Yasmin aliendelea
kunieleza.
“Sasa yule jinni
atatumaliza sote. Tulikuwa watu saba sasa tumebaki watano tu”
“Basi msije kule”
“Sasa tusipokuja
utatuletea chakula?”
“Nitawaletea. Na leo
ameshakula mtu mmoja harudi tena hadi kesho”
Tukawa tumefika
walipokuwa wenzetu.
“Leo tumepata msiba
mwingine” Mtu mooja akamwambia Yasmin.
“Nilishawambia tangu
mapema kuwa usalama hapa ni mdogo sana kwa sababu ya Harishi. Sasa mnaona
wenyewe, na ijui mtafanya nini ndugu zangu”
“Jamani kwanza tuleni
chakula. Yasmin ametuletea chakula. Tukanawe mikono kwa maji ya chumvi.
Mazungumzo baadaye” nikawambia wenzangu.
Tukaenda kunawa maji
ya bahari kisha tukarudi pale chini ya mti, tukaketi. Yasmin naye akaketi.na sisi. Tukaanza kula.
“Kwani Harish
ameshaenda zake?” Mtu mmoja akamuuliza Yasmin.
“Ameshaondoka”
nikamjibu mimi. “Angekuwepo Yasmin asingeweza kuja huku”
Fuatiliakisahiki hapo na usikose
ITAENDELEA KESHO
|
|
|
|
No comments:
Post a Comment