Mambo na Vijambo, Sikia hii
Hekaheka ya leo imetoka Kunduchi, ambapo
mama mmoja amesema alikuwa na mtoto ambaye aliumwa Malaria, baada ya
kumuuguza muda mfupi baadaye akafariki ambapo ajabu yake baadaye alikuwa
akisikia sauti ya mtoto huyo akilia kwa mbali mara kwa mara wakati wa
usiku hali iliyomshangaza na baada ya kuwasimulia marafiki zake
wakamwambia kuwa kama anaisikia sauti ya mtoto huyo akilia basi huenda
hajafa kweli atakuwa amechukuliwa kwenye mazingira ya ushirikina.
Mama huyo akakutanishwa na mganga ambaye
alisema ana uwezo wa kumrudisha mtoto wake na kumtajia gharama ambapo
kiasi cha pesa kilichotakiwa kwa kazi hiyo ni shilingi milioni mbili na
shilingi mia moja.
Baada ya kukubaliana siku moja alimpigia
simu akamwambia aende Mlandizi ambako alimkuta mtoto huyo, ambaye
alipomwangalia alithibitisha kuwa ni mtoto wake japo mganga hakumruhusu
arudi naye.
Baadaye alipigiwa simu tena na mganga
huyo akimwambia aende Kijiji kimoja kilichopo njiani kama unaelekea
Dodoma, akapewa mtoto wake lakini ukiangalia picha za mtoto huyo kabla
hajafariki na baada ya kurudishwa na mganga huyo inaonekana ni watoto
wawili tofauti japo mama wa mtoto anasema huyo ndiye mtoto wake.
Hupitwi na jambo ukifungua Kumekucha blog
No comments:
Post a Comment