Saturday, December 13, 2014

MGOMBEA WA CUF AWATAKA WAPIGA KURA KIJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA KESHO



KUMEKUCHA BLOG
Tanga,CHAMA Cha Wananchi (CUF) Tanga, kimewataka wananchi waliojiandikisha kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za mitaa unaofanyika kesho (leo) kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kupigia kura.
Akizungumza katika mkutano wa mwisho wa kampeni jana, mgombea nafasi ya Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Chuda, Suleiman Idd (CUF) aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi na kuichagua CUF.
Aliwataka kujitokeza kwa wingi na kupiga kura kwa amani na kisha kurejea katika sehemu zao za kujiletea maendeleo na kusubiri matokea na kuwataka kukipia kura chama hicho kwa wingi ili kuweza kuichukua nafasi hiyo.
“Ndugu zangu wananchi wa Chuda wa CUF na CCM munaonisikiliza hapa katika mkutano huu wa funga kampeni----nawaomba kwa heshima na taadhima munipigie kura nyingi ili niwe kiongozi wenu” alisema na kuongeza
“Kwa sera ambazo nimezinadi toka siku ya kwanza ya kampeni nadhani hakuna chama chengine kilicho na mwelekeo wa kuwaletea maendeleo kama CUF” alisema Idd
Akiwazungumzia wanawake kujitokeza kwa wingi, mgombea huyo aliwataka kujitokeza kwa wingi na kuacha shughuli nyengine ili kuweza kumpatia kura kwa wingi na kuahidi kuwachangia matibabu kwa kila nyumba kaya moja katika mtaa wake.
Alisema atatoa kipaumbele kwa wanawake wajawazito katika upatikanaji wa matibu kwa mfumo wa bima ya afya ikiwa na pamoja na wazee wanaume na wanawake.
“Nikiwa kiongozi wenu wa mtaa jambo la kwanza nitatoa kipaumbele kwa wanawake wajawazito na wazee katika matibabu kwa nay a biama ya afya----kila nyumba nitachangia kaya moja” alisema Idd
Alisema katika mtaa wake atahakikisha kila kaya inajiunga na mfuko wa bima ya afya na kuweza kupata matibabu bure mwaka mzima kwa kuchangia kiasi kidogo cha fedha.
Alisema pamoja na mambo mengine pia atahakikisha mtaa wake unakuwa katika mazingira mazuri ya usafi na kuweka sheria ndogo ndogo ili kuweza kutokomeza magonjwa ya miripuko zikiwemo homa za matumbo na malaria.
                                                  Mwisho

No comments:

Post a Comment