Monday, December 15, 2014

HADITHI KISIWA CHA HARISHI

SIMULIZI
 
KISIWA CHA HARISHI (12)
 
ILIPOISHIA TOLEO LLILOPITA
 
Hakukuwa na aliyemjibu. Sote tulikuwa tumeshikwa na fadhaa.
 
“Si niliwambia mtoke alfajiri, mmelala hadi saa hizi wakati niliwambia kuwa Harishi atakuja  leo”
 
“Ni kweli ulituambia” nikamkubalia.
 
“Sasa mbona hamkutoka alfajiri?’
 
“Tumepitiwa”
 
“Mtanilaumu mimi bure jamani!”
 
Hatutakulaumu hata kidogo. Umetufanyia wema sana”
 
“Harishi alikuja mapema sana akaniambia anasikia harufu ya kimtumtu. Nikamwambia mtu ni mimi. Akaniambia hebu ngoja. Akatoka kuja kuwatafuta”
 
“Siku hizi atakuwa anakuja kila siku kwa sababu ameona anapata mlo anaoutaka. Ni lazima mjihadhari”
 
“Mimi naona tuondoke tu humu ndani” Mwenzangu akasema kwa woga.
 
“Lakini amekwishakwenda zake. Kwa leo hatarudi tena” Yasmin akatuambia.
 
“Itabidi tuondoke tu” Mwenzangu alizidi kusisitiza.
 
“Kwani wenzenu wengine wako wapi?”
 
ITAENDELEA  
 
“Bado wamelala hadi sasa?” Yasmin akauliza kwa mshangao.
 
“Naona bado wamelala” nikamjibu.
 
“Kumbe nyinyi hamuwezi kuamka alfajiri?”
 
“Tatizo ni kuwa usingizi wenyewe unakuja wakati wa alfajiri” nikamwambia Yasmin.
 
“Basi ni balaa. Sasa itabidi usiku mwende mkalale sehemu nyingine, mjaribu bahati yenu”
 
“Tutafanya hivyo”
 
“Kuna nyumba nyingi hazina watu. Mnaweza kutafuta nyumba nzuri yenye vitanda mfanye makazi yenu. Hapamtakuwa mnakuja mchana tu, muda ambao nitawambia mimi”
 
“Tumekue;lewa, ngoja niwaamshe hawa mabwana”
 
Tukatoka pamoja mle chumbani. Tulipotoka tukawaona wenzetu nao wametoka.
 
“Hivi ndio mnaamka jamani?” Yasmin akawauliza.
 
“Dadayetu si unajua usingizi hautabiriki?” Mtu mmoja akamjibu.
 
“Hamkumbuki jana niliwambiaje? Si niliwambia muamke alfajiri muondoke?” Yasmin akawauliza.
 
“Ni kweli ulituambia lakini ndio tumepitiwa”
 
“Shakiri ameuliwa leo na Harishi!” nikawambia.
 
“Unasema kweli?” wakaniuliza kwa pamoja kwa mshituko.
 
“Ni kwa sababu ya kuchelewa kuamka. Sisis tumeponea chupuchupu baada ya kuingia mvunguni mwa kitanda”
 
“Basi utakwisha!”
 
“Yasmin ametupa wazo. Badala ya kulala hapa tutafute nyumba nyingine tuweke makazi yetu. Hapa tutakuwa tunakuja kula chakula mchana katika muda atakaotuambia Yasmin”
 
“Hivyo itakuwa vizuri” Mmoja wa wenzetu hao akasema.
 
“Sasa mjitayarishe, ninaenda kuwaandalia chai” Yasmin akatuambia.
 
Wakati Yasmin anakwenda jikoni, wenzetu wawili waliokuwa wamelala chumba cha pili ilivyokuwa hadi mwenzetu akauliwa.Tukawaeleza.
 
Kwa kweli walipata hofu.
 
“Sasa tukishakunywa chai tutoke tukatafute hiyo nyumba” nikawambia wenzangu.
 
Ilipofika saa nne tayari tulikuwa tumeoga na kunywa chai. Tukamwambia Yasmin tunataka kwenda kutafuta nyumba ya kukaa kwa maana tayari tulishakuwa wakazi wa kisiwa kile na hatukuwa na mategemeo ya kuondoka.
 
“Kwani mpaka mwende nyote”Yasmin akaniuliza.
 
“Unataka twende wangapi?” nikamuuliza.
 
“Mnaweza kwenda wawili, wawili mkabaki”
 
Mimi na wenzangu tukatazamana lakini sote tulionekana kutoliafikiwazo la Yasmin.
 
“Acha tu twende sote” nikamwambia Yasmin.
 
“Basi ngoja niwasindikize, msiniache peke yangu”
 
“Tukizunguka na wewe itakuwa vizuri” nikamwambia.
 
“Kwanini?’
 
“Kwa sababu wewe ndiye mwenyeji wetu, utaweza kutuongoza vizuri”
 
“Haya basi twendeni”
 
Tukatoka na Yasmin. Yasmin alikuwa akikijua vyema kisiwa hicho. Alituzungusha mitaa mbalimbali tukiangalia nyumba. Mwisho alitupeleka katiaka nyumba moja ambayo alituambia ilikuwa ya mtu mmoja tajiri wa kisiwa kile.ambaye naye naye aliuawa na Harishi.
 
Ilikuwa nyumba nzuri lakini ilikuwa imechakaa kwa vile ilikuwa haiishi watu. Tulipoingia ndani tulikuta mavumbi yalikuwa yameenea nyumba nzima.
 
Tukaanza kazi ya kuisafisha nyumba. Yasmin alitusaidia kufanya usafi. Ilikuwa kazi iliyotuchukua saa kadhaa.
 
Tulipomaliza tulichota maji kwenye kisima tukaoga kisha tukapumzika. Hapo ndipo tulipoanza kugawana vymba
 
Nyumba yenyewe ilikuwa ya vyumba vine na sisi wenyewe tulikuwa wanne. Kila mmoja alijichagulia chumba chake alichokipenda. Tulifungua makabati tukatoa mashuka na kutandika vitanda tulivyovikuta humo ndani.
 
Wakati ninatandika kitanda Yasmin aliniambia nimpe shuka atandike yeye. Nikampa.
 
“Natamani sana ningekuwa hapa pamoja na nyinyi” Yasmin akaniambia wakati anatandika.
 
“Ukiwa hapa utatuponzea sote”
 
“Ninasema tu lakini najua haitawezekana. Unajua katika nyinyi nyote nimekupenda wewe zaidi. Ninatamani ungekuwa mume wangu”
 
“Hata mimi natamani ungekuwa mke wangu lakini ndio tupo jela. Uhai wetu unahisabika”
 
“Ni kweli. Usikumbushiie hayo. Tuswali tuombe nusura itufikie”
 
“Wewe unaswali?” nikamuuliza Yasmin.
 
“Ninaswali lakini kwa siri sana. Harishi hataki niswali. Swala ndiyo inayonipa matumaini ya kuishi”
 
“Umenikumbusha jambo zuri sana na sisi tutaanza kuswali”
 
“Kila mara ninaota kunamtu atakuja kumuangamiza Harish na mtu huyo atakuwa mume wangu”
 
 
ITAENDELEA KESHO, USIKOSE MTU WANGU

No comments:

Post a Comment