Saturday, December 13, 2014

KAMPENI USALAMA BARABARANI YAZINDULIWA DAR



 Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe (watatu kutoka kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto,wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga,mwenyekiti wa usalama barabarani wilaya ya Kinondoni Hua Tluway,wapili (kushoto) na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Hamza Kassongo na Henry  Bantu
 Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe (watatu kutoka kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto,wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga,mwenyekiti wa usalama barabarani wilaya ya Kinondoni Hua Tluway,wapili (kushoto) na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Hamza Kassongo na Henry  Bantu
 Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe (wapili kutoka kulia) Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga,mwenyekiti wa usalama barabarani wilaya ya Kinondoni Hua Tluway,wapili (kushoto) na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Hamza Kassongo na Henry  Bantu (kulia) wakishangilia baada ya uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.
 Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, wakati alipokuwa akimuelezea matumizi ya pete maalumu za kidoleni ambazo huwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva Kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Hamza Kassongo na Henry M. Bantu (kulia)  na  Mjumbe wa  baraza hilo Hamza Kasongo.
 Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia, wakati alipokuwa akimuelezea matumizi ya pete maalumu za kidoleni ambazo huwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva Kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani Hamza Kassongo na Henry M. Bantu (kulia)  na  Mjumbe wa  baraza hilo Hamza Kasongo.
 Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe (kushoto)  akimuonyesha  dereva wa pikipiki  pete zenye ujumbe wa “Wait to Send” wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga
 Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe (kushoto)  akishuhudia  dereva wa pikipiki  akivalishwa  pete zenye ujumbe wa “Wait to Send” wakati  wa  uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga
 Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe (kushoto)  akishuhudia  dereva wa pikipiki  akivalishwa  pete zenye ujumbe wa “Wait to Send” wakati  wa  uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga
 Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe (kushoto)  akishuhudia  dereva wa pikipiki  akivalishwa  pete zenye ujumbe wa “Wait to Send” wakati  wa  uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani uliofanyika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Mohammed Mpinga akijadiliana jambo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani iliyozindiliwa  na Waziri wa Mambo ya Ndani  Mh.Mathias Chikawe katika eneo la Mwenge makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi jijini  Dar es Salaam leo, uzinduzi huo uliambatana na  upimaji wa kiwango cha pombe mwilini kwa madereva na ugawaji wa pete maalumu za kuwakumbusha madereva kuacha kutumia simu za mkononi wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.


Waziri wa habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dr Fenela Mukangara akipiga mkwaju wa penati kuashiria  uzinduzi rasmi wa mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 15 ya Copa Coca-Cola ngazi ya Taifa, jijini  Dar-es-salaam leo

TIMU ya soka ya mkoa wa Simiyu imeanza vibaya mashindano ya Copa-Coca-Cola ngazi ya taifa baada ya kupokea kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa vijana wa Mkoa wa Kigoma kwenye mchezo wa ufunguzi uliochezwa katika uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam jana.
Kigoma walipata bao la kwanza mapema kwenye dakika ya nane kupitia kwa Juma Swalehe, huku Juma Zuberi akiongeza bao la pili dakika ya 30 na Idrisa Akilimali alihitimisha karamu ya mabao kwa Kigoma kwa kufunga bao safi mnamo dakika ya 57, bao la kufutia machozi la Simiyu lilifungwa na Kaluona Abdallah katika dakika ya 88 ya mchezo huo.
Michuano hiyo ilizinduliwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mh. Fenella Mukangara ambaye aliwashauri makocha wa timu kutumia michuano ya Copa-Coca-Cola kama changamoto ya kuibua vipaji vipya katika timu zao kwa wasichana na wavulana.
Mukangara aliwaasa vijana kuhakikisha wanajituma kulitangaza taifa la Tanzania katika michuano mabalimabli ya  kimataifa. “Nina furaha sana kuona wasichana pia wakijumuishwa katika michuano hii ya Copa-Coca-Cola na pia natoa shukrani zangu za dhati kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) kwa kuhakikisha kuwa soka la wanawake linakuwa hapa nchini”, Mukangara alisema.
Mukangara pia aliwasisitiza washiriki wote wa michuano hiyo kuhakikisha kuwa wanazingatia nidhamu ya mchezo uwanjani. “Tuna imani kuwa washiriki wote mtazingatia sheria za mchezo huu kama inavyagizwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA)”, Aliongeza Mukangara.
Naye Meneja wa Coca-Cola nchini  Yebeltal Getachew alielezea nia yao ya dhati katika kuendeleza michuano hiyo ya Copa-Coa-Cola nchini. Wachezaji wanaofanya vizuri katika michuano hii hupelekwa nchini Afrika Kusini kwa mafunzo zaidi.
Copa-Coca-Cola ni michuano pekee ambayo huanzia ngazi ya chini kabisa na baadaye ngazi ya Taifa ikishirikisha mikoa yote ya Tanzania bara pamoja na Zanzibar.
Kwa upande wake Rais wa TFF Jamal Malinzi aliwaonya viongozi wa timu zote zinazodanganya umri na kusisitiza kuwachukulia hatua za kinidhamu. “Katika kuonesha umakini katika michuano hii tumewaondoa wachezaji 87 kutoka katika mikoa ya Mbeya na Lindi kutokana na kudanganya umri”, Malinzi alisisitiza.
Michuano ya Copa-Coca-Cola itafikia tamati mnamo Desemba 20, mwaka huu, katika Uwanja wa kumbukumbu ya Karume jijini Dar es salaam.

TIMU YA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KUTOKA OFISI YA RAIS, TUME YA MIPANGO YATEMBELEA MELI YA KIHISTORIA YA MV LIEMBA

Wakaguzi wa Miradi ya Maendeleo toka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wamepata fursa adhimu ya kutembelea meli kongwe kupita zote nchini, MV Liemba iliyo kwenye Ziwa Tanganyika, mkoani Kigoma.

Wakizungumza mara walipofika katika meli hiyo baadhi ya wakaguzi hao hawakuficha bashasha waliyokuwa nayo mara baada ya kuingia ndani ya meli hiyo kongwe iliyo na umri zaidi ya miaka 100.

Mmoja wa wakaguzi hao Bibi Zena Hussein, alisema kuwa anajisikia furaha sana kuingia na kushuhudia mandhari ya meli hiyo ya kihistoria nchini Tanzania.

“Nimefurahi sana kufika leo hii kwenye meli hii yenye miaka zaidi ya 100, licha ya ukongwe wake bado inaonekana imara na yenye uwezo wa kufanya kazi miaka mingi zaidi,” alisema.

MV Liemba ni meli ya Kitanzania inayohudumia pwani za Ziwa Tanganyika. Ni chombo cha usafiri wa majini chenye umri mkubwa kuliko kingine chochote nchini na kipo tangu mwaka 1914. Meli hii kama zilivyo meli ningine inasukumwa na injini ya diseli na ina urefu wake ni mita 67, upana mita 10 na uzito wa tani 1500.

Kwa mujibu wa Nahodha wa meli hiyo, Kapteni Mathew Mwanjisi, meli hiyo ina uwezzo wa kubeba abiria 600 na tani za mizigo 200.

“Katika daraja la kwanza meli ina uwezo wa kubeba abiria 20, daraja la pili abiria 30 na daraja la tatu abiria 550,” alisema. 

Meli ya MV. Liemba inamilikiwa na Kampuni ya MSCL na kusajiliwa na Mamlaka ya Usafiri Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kwa namba ya usajili KP/P001. Meli hiyo ilijengwa katika Bandari ya Kigoma mwaka 1913 na mjenzi kutoka Ujerumani kwa ajili ya usafirishaji wa mizigo na abiria.

Mv. Liemba ilitengenezwa nchini Ujerumani mwaka 1913 ikiwa ikiitwa kwa Kijerumani "Graf von Goetzen" kwenye kiwanda cha meli cha Meyer huko Papenburg.
Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikiwa ndani ya MV Liemba mara walipofika kujionea mandhari ya meli hiyo kongwe duniani.
Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) akisaini kitabu cha wageni ndani ya MV Liemba. Kulia ni Nahodha wa Meli hiyo, Kapteni Mathew Mwanjisi.
Nahodha wa MV Liemba, Kapteni Mathew Mwanjisi (Watatu kushoto) akitoa maelezo kwa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango.
Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Wapili Kulia) akiiongoza Timu yake kusikiliza kwa umakini namna ya kusoma radar inayotumika ndani ya Meli ya MV Liemba. Anayewapa maelezo ni Nahodha wa Meli hiyo, Kapteni Mathew Mwanjisi.

Nahodha wa Meli ya MV Liemba, Kapteni Mathew Mwanjisi (Kulia) akitoa maelezo ya namna ya kutumia chombo cha kuokolea kwa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango. Wanaomsikiliza ni Kiongozi wa Timu hiyo, Bibi Florence Mwanri (Kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Mipango na Ufuatiliaji (Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango), Bw. Omary Abdallah.
Mhandisi Mkuu wa Meli ya MV Liemba, Eng. Justine Joachim (Mwenye fulana nyeusi) akiwapa maelezo Wakaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipongia kujionea mitambo ya kuendeshea meli hiyo.

Kazi inaendelea! Watumishi wa Meli ya MV Liemba wakiendelea na kazi ya kushusha shehena ya mahindi kutoka kwenye meli hiyo. PICHA NA SAIDI 

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katka picha ya pamoja na wanachama waj Umoja wa wake wa viongozi ( New Millenium Women Group) katika chakula cha jioni kilichoambatana na burdani mbalimbali kwenye ukumbi wa Kardinal Rugambwa, Oysterbay jijini  Dar es salaam, Desemba 12, 2014.  Chakula hicho  kiliandaliwa ili kuchangisha fedha kwa ajili ya maboresho ya kituo cha  kulea watoto yatima cha Buhangija mkoani Shinyanga.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda picha ya juu akiwa katka picha ya pamoja na washiriki wa maonyesho ya mavazi yaliyoandaliwa na  Umoja wa wake wa viongozi ( New Millenium Women Group) katika chakula cha jioni kilichoambatana na burdani mbalimbali kwenye ukumbi wa Kardinal Rugambwa, Oysterbay jijini  Dar es salaam, Desemba 12, 2014.  Chakula hicho  kiliandaliwa ili kuchangisha fedha kwa ajili ya maboresho ya kituo cha  kulea watoto yatima cha Buhangija mkoani Shinyanga.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) unnamed4 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda picha ya juuakiwa katka picha ya pamoja na washiriki wa maonyesho ya mavazi yaliyoandaliwa na  Umoja wa wake wa viongozi ( New Millenium Women Group) katika chakula cha jioni kilichoambatana na burdani mbalimbali kwenye ukumbi wa Kardinal Rugambwa, Oysterbay jijini  Dar es salaam, Desemba 12, 2014.  Chakula hicho  kiliandaliwa ili kuchangisha fedha kwa ajili ya maboresho ya kituo cha  kulea watoto yatima cha Buhangija mkoani Shinyanga.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) unnamed5 
Baadhi ya  washiriki wa maonyesho ya mavazi yaliyoandaliwa na  Umoja wa wake wa viongozi ( New Millenium Women Group) katika chakula cha jioni kilichoambatana na burdani mbalimbali kwenye ukumbi wa Kardinal Rugambwa, Oysterbay jijini  Dar es salaam, Desemba 12, 2014 wakijitambulisha baada ya onyesho hilo.  Chakula hicho  kiliandaliwa ili kuchangisha fedha kwa ajili ya maboresho ya kituo cha  kulea watoto yatima cha Buhangija mkoani Shinyanga.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 

No comments:

Post a Comment