Tuesday, December 16, 2014

MASHIKA YASIYO YA KISERIKALI YAFUNGIWA KWA TUHUMA

 Mashirikayasiyo ya Kiserikali yafungiwa, yahusishwa kushirikiana na magaidi


Mashirikayasiyo ya Kiserikali yafungiwa, yahusishwa kushirikiana na magaidi

NEWSTumesikia kuhusu nchi ya Kenya kukumbwa na misukosuko kadhaa hivi karibuni ambayo inahusiana na masuala ya mashambulizi ya kigaidi.
Serikali ya Kenya jana December 16 ilitangaza kyafutia leseni mashirika yasiyo ya kiserikali zaidi ya 510, kutokana na kutofuata kanuni za Mashirika hayo huku mengine 15 yakifutwa kutokana na kusemekana kuwa yanahusika kufadhili shughuli za kigaidi nchini humo ambapo maelfu ya wafanyakazi wakiwa na wasiwasi wa kukosa ajira.
Taarifa kutoka Kenya zinasema kuwa mashirika mengi yamekuwa yakikiuka kanuni zilizowekwa ikiwa ni pamoja na kutumia njia inayofaa kupata vibali vya wafanyakazi wanaotoka nchi za nje na pamoja na kuipa Serikali nakala ya matumizi ya fedha wanazopata kutoka kwa wafadhili.
Hatua hiyo inaonekana kama juhudi za Serikali kukabiliana na ukosefu wa usalama nchini humo huku uchunguzi ukiwa unaendelea.

No comments:

Post a Comment