Monday, December 15, 2014

MAXIMO ADAIWA YUKO NJIANI KUIACHA YANGA

Zimeanza tetesi na swali likafuatia, Marcio Maximo anaondoka Yanga ?


Zimeanza tetesi na swali likafuatia, Marcio Maximo anaondoka Yanga ?

Maximo huenda akajiuzulu kuifundisha Yanga .
Taarifa ambazo bado hazijathibitishwa zinasema kuwa kocha Mbrazil Marcio Maximo huenda akaondoka ndani ya klabu ya Yanga kufuatia kushindwa kuelewana na uongozi wa klabu hiyo .
Habari zaidi zinasema kuwa kocha huyo amefikia hatua ya kuanza kuwaaga baadhi ya wachezaji alio nao karibu akisema kuwa anaondoka kwani amekiri kuwa ni vigumu kuiongoza klabu ya Yanga.
Hali ilianza kuwa ngumu kwa Maximo baada ya kocha huyo kuishuhudia timu yake ikifungwa kwenye mchezo wa Mtani Jembe dhidi ya mtani wake wa jadi Simba .
Maximo huenda akajiuzulu kuifundisha Yanga .
Maximo huenda akajiuzulu kuifundisha Yanga .
Inasemekana kuwa kikosi alichokipanga Maximo kwenye mchezo huo ambacho kilionekana kuwa cha kujihami sana kama ambavyo imetokea kuwa kawaida ya Mbrazil huyo kwenye mechi kubwa kilizua minong’ono miongoni mwa wachezaji wake hali ambayo ilifanya viongozi wa timu hiyo kutopendezwa na timu hiyo kufungwa 2-0.
Maximo inadaiwa amepinga kitendo cha uongozi wa Yanga kuwa na mpango wa kumuajiri mkurugenzi wa ufundi akiamini kuwa anapaswa kupewa uhuru wa kufanya kazi yake bila kuingiliwa na mtu .
Mdachi Hans Van Der Pluijm ametajwa kuwa mbioni kuchukua nafasi ya Marcio Maximo .
Mdachi Hans Van Der Pluijm ametajwa kuwa mbioni kuchukua nafasi ya Marcio Maximo .
Tetesi zaidi zinasema kuwa kocha wa zamani wa klabu hiyo Mholanzi Hans Van Der Pluijm tayari yuko nchini Tanzania na ameandaliwa kuchukua mikoba ya Maximo endapo Mbrazil huyo ataamua kuondoka kama ilivyoanza kusikika .

No comments:

Post a Comment