Simba yaongeza nguvu kwa kusajili beki, unajua anatoka timu gani?
Katika usiku wa jana ambao umekuwa na movement
nyingi za wachezaji na makocha , klabu ya Simba imekamilisha usajili wa
beki wa pembeni toka timu ya Mtibwa Sugar, Hassan Kessy.
Beki huyo ambaye ametokea kuwa mmoja
kati ya wachezaji wa kutumainiwa kwenye klabu hiyo ya wakata miwa wa
huko Manungu Turiani mkoani Morogoro, anaungana na wachezaji wapya
waliosajiliwa katika kipindi hiki cha dirisha dogo ambao ni Simon
Sserunkuma, Danny Sserunkuma, na Juko Murshid wote kutoka Uganda.
Kessy ambaye ametajwa kuwa moja kati ya
wachezaji wanaokaribia kuwa mmoja ya wachezaji wa Timu ya Taifa Stars
alichezea Mtibwa kwa mara ya mwisho katika mchezo wa kirafiki ambao
ilifungwa na Azam Fc 3-1.
Beki huyu anasajiliwa baada ya
mazungumzo ya muda mrefu yaliyofanyika chini ya usimamizi wa viongozi wa
Simba wakiongozwa na Geoffrey Nyange Kaburu na Kiongozi wa Mtibwa,
Jamal Bayser.
Tetesi zaidi zinasema kuwa Simba imemsajili beki huyo kwa thamani ya shilingi milioni 30.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia, kumekucha blog
No comments:
Post a Comment