Kumekucha blog
Tanga, ZOEZI la uhesabuji kura Serikali za
mitaa katika vituo mbalimbali halmashauri ya jiji la Tanga limegubikwa na
vitimbi vya uvunjifu wa amani na kulazimika vyombo vya usalama kuingilia kati.
Katika kituo cha upigaji kura cha Madina halmashauri
ya jiji la Tanga mtu mmoja ambaye hakujulikana jina alichukua sanduku la kupiga
kura na kuzimwaga chini hali ambayo ilizusha tafrani na baadhi ya watu
kupigana.
Jeshi la polisi lilifika na kurejesha usalama na zoezi
kuendelea huku kukiwa na ulinzi wa askari polisi wakiwa na silaha za kuzuia
vitendo vyovyote vya uharibifu wa amani.
Tukio hilo limedaiwa kufanyika baada ya mwanachama
huyo kuona chama chake kuona mazingira ya kuelemewa na hivyo kukimbilia sanduku
la kura na kulitupa chini hali iliyozusha kizaazaa.
Katika kituo cha Mikanjuni mama mmoja alimpiga mtoto
wake baada ya kukaidi kupiga kura kwa madai kuwa zoezi hilo lilitawaliwa na vitendo
vya vurugu na mamluki na baadhi ya watu kupiga kura zaidi ya mara moja.
Tukio hilo lilitokea wakati mama huyo ambaye hakutaka
kujitambulisha jina lake, alisema aliweza kufika katika kituo chake cha kupigia
kura toka alfajiri lakini hadi kufikia saa 9 mchana jina lake halikutajwa na
hivyo kuwataka watoto wake nao waondoke katika kituo hicho.
“Jina langu katika ubao lipo na ni la mwanzo mwanzo
chakushangaza wenzangu ambao wamekuja muda kuchelewa wanaingia ndani na kupiga
kura na kuondoka---mimi napigwa na jua hadi muda huu” alisema
“Kwa ukiritimba huu bora mimi na watoto wangu sote
tusipige----uamuzi wa kumpiga ni kukaidi agizo langu na ndio nikachukua uamuzi
wa fimbo” alisema
Wakati wa zoezi la kupiga kura wananchi wengi wamelalamikia
mfumo wa kuita majina na kuacha
utaratibu uliozoeleka wa foleni na hivyo kuzusha hali ya sitofahamu.
Mwisho
No comments:
Post a Comment