Katika hali isiyokuwa ya kawaida mzee
mwenye umri wa miaka 80, ameomba msaada wa Serikali kuingilia kati
kuzuia shamba lake lisiuzwe na mtoto wake ambapo shamba ambalo mtoto
huyo analiuza lina kaburi lake alilolchimba zaidi ya miaka 35 iliyopita.
Shamba la mzee huyo liko Mathira, Kenya ambapo mzee huyo amesema kuwa
mtoto wake wa kiume amekuwa akiuza sehemu ya shamba hilo kidogo kidogo.Amesema tofauti na matarajio yake alikuwa akiamini Mtoto huyo angekuja kumsaidia uzeeni lakini mtoto huyo, amekuwa akiuza shamba hilo bila ruhusa yake na kuhofia kuwa anaweza kuuza hata kipande cha Shamba ambacho amechijimbia kaburi lake.
No comments:
Post a Comment