Kumekucha blog
Korogwe,POLISI Wilayani Korogwe Mkoani Tanga
imewakamata wahamiaji haramu 12 wenye
asili ya Kiethopia wakiwa wamefichwa katika gari wakisafirishwa kuelekea Dar
esSalaam na hali zao kukutwa zikiwa mbaya.
Akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake,
kamanda wa polisi Mkoani hapa, Freisser Kashai, alisema tukio hilo lilitokea
juzi saa 10 jioni katika kizuizi cha polisi kijiji cha Bwiko barabara ya Mombo
Segera.
Akiwataja watu hao kuwa ni, Kashoma Bayen(24), Berchano
Gamada(32), Awal Jamal(23),Yanis Gatiso(28), Metson Sipril(21), Tashona
Hayalis(30), Adino Samiru(20)Kengeny Siyun(22),Charnes Egesa(20),Abdi
Badru(21), Siumanda Samadu(26) na Malako Abuu (23) wote wakiwa ni raia wa
Ethopia.
“Hawa watu walikamatwa wakiwa wamefichwa katika gari aina ya
scania wakiwa hali zao ni dhaifu na kutia huruma----ukiwaangalia utwaonea huruma kwani
hata kuzungumza hawawezi kwa njaa” alisema Kashai na kuongeza
“Tunapowakamata wahamiaji haramu kwanza tunawabana
waliowasfirisha ninani lengo ni kuwatia mbaroni----tatizo lililojitokeza kwa a
hawa hawajui kuzungumza Kiswahili wala
kiingereza na zaidi kusema pia ni tabu kwa kuumwa na njaa” alisema
Alisema wakati wa mahojiano ilikuwa vigumu kufahamiana baada
ya watu hao kutojua kuzungumza Kiswahili wala kiingereza na hivyo kupata majina
yao na kuwa vigumu kupata maelezo ya watu waliowasafirisha.
Alisema kwa sasa polisi inaendelea kufanya upelelezi na mara
baada ya kukamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma za kuingia nchini
bila kibali.
Akizungumzia kuhusu watu wanaofanya biashara ya kusafirisha
watu, kamanda Kashai alisema polisi itaendelea kufanya upelelezi kwa baadhi ya
watu ambao wanatuhumiwa kujihusisha na biashara hiyo haramu.
Alisema polisi iko na taarifa kutoka kwa watu mjini na maeneo
ya mipakani mwa nchi jirani ya Kenya hivyo kuamini kuwa itawakamata na
kuwafikisha katika vyombo vya sheria.
“Tuko na majina ya baadhi ya watu na tunayafanyia uchunguzi na
ukikamilika kama itabainika tutawakamata kwa mahojiano-----tunataka kudhibiti
mianya yote ya upitishaji wa mali za magendo na wahamiaji haramu” alisema
Kashai
Akitoa wito aliwataka wananchi kushirikiana na polisi katika
mambo mbalimbali ya kiusalama pamoja na kupeana taarifa za matukio ya kihalifu
pamoja na kuwafichua watu wanaofanya biashara haramu ya kusafirisha binadamu
No comments:
Post a Comment