Kumekucha blog
Tanga,WANAFUNZI wa shule za msingi na
sekondari Tanga, wameitaka Serikali kuweka utaratibu maalumu wa nauli za mabasi
kama ilivyo kwa daladala ili kuwa msaada
vipindi vya mwisho wa mwaka kujumuka na
familia zao katika sherehe mbalimbali zikiwemo za sikukuu za Krismass.
Wakizungumza na waandishi wa habari jana kituo kikuu cha
mabasi yaendayo Mikoani cha Kange, walisema wanashindwa kusafiri kujumuka na familia
zao kutoka na gharama kubwa za nauli za mabasi.
Walisema hiyo inatokana na baadhi ya familia kuwa na uwezo
mdogo wa kutuma nauli na hivyo kukosa nafasi kuungana katika mambo mbalimbali
muhimu kama misiba na sherehe za sikukuu ya Krismass na Idd kwa Waislamu.
“Hapa sisi tunaelekea Mwanza na nauli iko elfu sitini utadhani
ni ya ndege---wazazi wetu ni masikini hawana uwezo wa nauli ya kwenda na kurudi
na ndio mara nyingi likizo huwa tunajikalia shule” alisema Gosper Mwalilino
“Kama Serikali ingeweka utaratibu wa nauli kwa wanafunzi kama
ilivyo kwa daladala ingekuwa msaada sana----hali hii inawaumiza wazazi wetu na
sisi wenyewe hasa sie tunaokaa mbali” alisema
Alisema vipindi vya likizo kubwa mashuleni wanafunzi wamekuwa
wahanga wakubwa wa nauli za mabasi na hivyo kuitaka Serikali kuliangalia kwa
upande wao wa wanafunzi.
Kwa upande wake mwanafunzi
shule ya Gallanosi , Vicky Kimario,anaetokea Arusha alisema mara nyingi
vipindi vya likizo hujikalia shuleni baada ya kushindwa kumudu gharama za nauli
za mabasi.
Alisema hali hiyo inakuja baada ya nauli kupanda maradufu na
hivyo kuwa katika mazingira magumu ya kuweza kuishi shuleni hapo baada ya
huduma zote muhimu kusitishwa ikiwemo ya upatikanaji wa chakula.
“Mwaka jana sikuweza kwenda nyumbani kwani nilishindwa
kutokana na nauli kupanda maradufu---na mwaka huu naona yametokea yele yale na
baba amenitumia elfu ishirini na ukitoa kuna makato ambayo sitioweza kukata
tikiti” alisema Kimario
Ameitaka Serikali kuwawekea utaratibu wa nauli kwa wamiliki
wa mabasi yaendayo Mikoani wanafunzi vipindi vya likizo na kuweza kujumuika na
familia zao katika vipindi vya sikukuu.
Mwisho
No comments:
Post a Comment