Hii ni adhabu iliyotolewa kwa Wanajeshi wa Nigeria baada ya kugoma kupigana na Boko Haram
Wakili wa wanajeshi hao 54 alisema kuwa wanajeshi hao watauawa kwa kupigwa risasi huku wengine watano wakiachiliwa huru baada ya kukutwa hawana makosa.
Zaidi ya watu 2000 wameuwawa katika mashambulizi yaliyofanywa na kundi hilo hadi sasa na tayari maelfu zaidi ya watu wamelazimishwa kuhama makwao kutokana na vita vinavyoendelea.
Wakili aliyesimamia kesi hiyo Femi Falana, alisema kuwa wanajeshi hao wote walituhumiwa kupanga njama ya kuasi dhidi ya mamlaka ya kikosi cha Divisheni ya 7 cha jeshi ya Nigeria.
Wanajeshi wote walikataa mashtaka hayo na sasa hukumu hiyo inasubiri idhini ya Maafisa wa ngazi za juu wa Serikali hiyo kabla yakutekeleza adhma yao.
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,kumekucha blog
No comments:
Post a Comment