Monday, December 15, 2014

MTOTO ADONDOKA JUU YA FRIJI NA KUFARIKI

Hekaheka ya leo Desemba15 iko hapa, inahusu Mtoto aliyedondoka juu ya friji na kufariki.


Hekaheka ya leo Desemba15 iko hapa, inahusu Mtoto aliyedondoka juu ya friji na kufariki.

candle-lightHekaheka ya leo Desemba 15 imetokea Dar inahusu mtoto mdogo mwenye umri wa miezi tisa kufariki baada ya kuanguka kutoka juu ya friji akiwa na babu yake ambaye inasemekana kahusika kuanguka kwa mtoto huyo.
Baba wa mtoto huyo amesema alipata taarifa za kuumia kwa mtoto wake na alipofika Hospitali alikuta hali ya Mtoto ikiwa mbaya na akilia sana kwa maumivu, baada ya kupatiwa matibabu waliruhusiwa na kurudi nyumbani.
Siku iliyofuata mtoto alizidiwa na kesho yake wakamrudisha tena Hospitali ya Amana,  baada ya uchunguzi kufanyika  ilionekana Mtoto aliumia sehemu ya kichwani na kushauriwa kumhamishia Hospitali ya Muhimbili kwa matibabu zaidi na kabla yakupatiwa matibabu akafariki.
Mwili wa Mtoto huyo umehifadhiwa katika Hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi zaidi na Babu ambaye oinasemekana amehusika kuanguka kwa mtoto huyo anashikiliwa na Jeshi la Polisi.

No comments:

Post a Comment