Ndege ya KDF yaanguka Somalia
Ndege ya jeshi la KDF nchini Kenya imeanguka katika eneo la Kismayu nchini Somali.
Ndege
hiyo ilianguka siku ya Alhamisi mwendo wa saa tisa na robo ilipokuwa
ikirudi Kenya baada ya kutekeleza mashambulizi katika eneo la Jamaame
kusini mwa Somalia.
Kulingana
na msemaji wa Jeshi kanali david Obonyo: ''Ndege ya KDF iliokuwa
ikirudi nchini Kenya baada ya kufanya mashambulizi katika eneo la
Jamaame kusini mwa Somali,ilikumbwa na matatizo ya kiufundi na kuanguka
katika eneo la Kismayu .
Kanali Obonyo hata hivyo hakusema iwapo kulikuwa na majeruhi yoyote.
Jeshi la
Kenya limesema kuwa ndege hiyo ilianguka kutokana na hitilafu za
kimitambo baada ya kufanya oparesheni katika eneo la Jamaane Kusini mwa
Somalia
No comments:
Post a Comment