KUMEKUCHA BLOG
Korogwe,WATU kumi wanaosadikika kuwa wezi
wamekata nguzo tatu za umeme kwa kutumia msumeno aina ya Chensoo kisha kuiba
nyaya za umeme aina ya kopa kijiji cha Magoma Wilayani Korogwe Mkoani Tanga.
Tukio hilo lilitokea jana saa 8 usiku baada ya wakazi
kijiji cha magoma kusikia kishindo kikubwa kilichoambatana na kukatika umeme na
hivyo kuingiwa na hofu jambo ambalo liliwasukuma kuamshana na kwenda uelekeo wa
mshindo huo.
Wakizungumza katika eneo la tukio, wakazi hao walisema
baada ya kishindo hicho waliamshana kwa kuamini kuwa kuna kitendo cha kihalifu
na hivyo kupiga simu kituo cha polisi Korogwe na wao kuzifuatiliza nguzo za umeme moja baada ya
moja.
“Kilipiga kishindo kikubwa kilichoambatana na kukatika
umeme kitu ambacho si cha kawaida kwetu----tuliamshana kwa kutumia simu na tukakutana kwa kiongozi wetu wa Serikali”
alisema Mohammed Nassour Bodo
“Tuliamini kuwa kishindo kilichoambatana na kukatika
umeme ni hujuma imefanyika na hivyo kuzifuatilia nguzo moja baada ya
nyengine----tulipofika katika shamba la mahindi tulisikia sauti za watu
wazungumza kwa kutoa vitisho” alisema Bodo
Bodo alisema wakati wamefika katika nguzo ambazo
zimeangushwa hawakuona nyaza za umeme kitendo ambacho kinamaanisha wezi hao
walishazikata na kutoweka nazo.
Wakati maofisa wa Shirika la Umeme Tanzania Tanesco
Mkoa na Wilayani wakiongozwa na Meneja wake wa Korogwe, Bakary Suleiman,
aliendesha msako katika vijiji vya jirani kwa lengo za kuzitafuta nyaya hizo
kwa kuamini kuwa bado hazijatoweka kijijini hapo.
Wakati za zoezi hilo pia likiwashirikisha maofisa
usalama wa Wilaya walifanikiwa kuzikuta roli mbili zikiwa zimefichwa katika
pori jirani eneo la tukio.
“Tukio hili ni kubwa na halijawahi kutokea katika
Wilaya yangu----kwa kweli kwanza niwashukuru wakazi wa kijiji cha Magoma kwa
ushirikiano wao na umoja waliouonyesha kwa Tanesco” alisema Suleiman
Aliwataka kuwa na umoja na mshikamano katika mambo
mbalimbali yakiwemo ya kimaendeleo pamoja na kuwa na ada ya kutoa taarifa za
kihalifu kama ambavyo wamefanya kwa shirika hilo.
Wakati wa zoezi hilo la kuwatafuta wezi waliofanya
hujuma hizo, Afisa Uhusiano na Wateja Mkoa wa Tanga, Monica Mabada, amezitaka
mamlaka za Serikali za vijijini na vitongoji kuunda vikosi askari jamii lengo
likiwa ni kuyaweka maeneo yao kuiusalama.
Alisema kuwepo kwa askari jamii katika maeneo yao
kunaweza kuwa msaada wa usalama wao pamoja na mali zao na hivyo kuwataka
kulitekeleza jambo hilo ambalo litaepusha vitendo vya kihalifu nahujuma.
Mwisho
No comments:
Post a Comment